Kiini Macho Kingine cha TUME ya Bunge

mizambwa

JF-Expert Member
Oct 8, 2008
4,422
1,790
Tanzania tumekuwa na utitiri wa TUME zinazoundwa kuchunguza mambo mbalimbali lakini majibu ya TUME hizo hayawekwi hadharani.

Tume inpoundwa inatangzwa na pia muda wa uchunguzi unawekwa wazi lakini matokeo yake hayawekwi hadharani.

Kuna umuhimu gai wa kuunda Tume zinazotumia pesa nyingi ya walalahoi ambayo ingelisaidia huduma za jamii???

ANGALIA KITUKO KINGINE HIKI CHA BUNGENI!!!!

========================================================================================================

Wingu laigubika Ripoti ya Ngwilizi - Habari - mwananchi.co.tz

WINGU LAIGUBIKA RIPOTI ya NGWILIZI


Waandishi Wetu, Dodoma
WAKATI Bunge likianza mkutano wake wa Tisa leo, zipo taarifa Ripoti ya Kamati ndogo iliyoundwa kuchunguza tuhuma za wabunge kujihusisha na vitendo vya rushwa haitasomwa na kisha kujadiliwa.
Badala yake, kwa mujibu wa watoa habari wetu, Kamati ya Uongozi, iliyokutana jana iliamua kwamba litatolewa tamko kuhusu ripoti ya kamati hiyo, hivyo haitasomwa wala kujadiliwa kama ambavyo wabunge wamekuwa wakitaka.

Kwa maana hiyo Spika wa Bunge, Anne Makinda huenda akatumia kanuni nyingine kutoa tamko kuhusu uchunguzi huo, hali ambayo haitatoa fursa kwa wabunge kuijadili kama ambavyo baadhi yao wamekuwa wakishinikiza.
Miongoni mwa kanuni ambazo Spika anaweza kuzitumia ni pamoja na ile ya 33 (2) ambayo inasema: "Wakati wa kikao, Spika anaweza kutoa taarifa nyinginezo kadri atakavyoona inafaa."

Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, John Joel jana alikataa kuzungumzia suala hilo akiahidi kulitoa ufafanuzi leo... "Ratiba ya shughuli za Bunge bado iko kwenye ngazi ya Kamati ya Uongozi. Sasa pengine tusubiri kesho (leo) ikiwa tayari kila kitu kitakuwa wazi, hakuna haja ya kuwa na haraka."
Jana, Kamati ya Uongozi wa Bunge ilikutana mjini Dodoma kujadili mambo mbalimbali na habari zinasema kwamba suala la Ripoti hiyo ya Ngwilizi, pia lilijadiliwa.

Agosti 2 mwaka huu, Spika Makinda aliunda kamati hiyo ndogo kuchunguza tuhuma za rushwa zilizokuwa zikiwakabili baadhi ya wabunge ambao walidaiwa kwamba walihongwa ili kuikwamisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.

Kuundwa kwa kamati hiyo, kulitanguliwa na tukio la kuvunjwa kwa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Julai 28, mwaka huu pia kutokana na tuhuma hizohizo.
Tayari kumekuwa na taarifa kwamba ripoti hiyo imevuja na maudhui yake kuchapishwa katika baadhi ya vyombo vya habari, hali ambayo ilisababisha Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai kuonya kwamba waliohusika na kuvuja huko huenda wakajikuta matatani kwani ni kosa la kisheria.

"Kitendo cha kuchambua na kuchapisha maudhui ya taarifa hiyo katika vyombo vya habari ni kinyume cha sheria na kinaingilia uhuru, haki na madaraka ya Bunge kwa mujibu wa Kifungu cha 31 (1) (g) cha Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge Sura 296," alisema Ndugai katika mkutano wake na waandishi wa habari hivi karibuni.

Mmoja wa wabunge ndani ya kamati iliyochunguza suala hilo (jina tunalihifadhi kwa sasa), ndiye anayedaiwa kwamba aliivujisha ripoti hiyo ya uchunguzi kwa makusudi, lengo likiwa ni kumshinikiza Spika Makinda aitoe hadharani ili kuwasafisha watuhumiwa.

Mbunge huyo alifanya hivyo kwa msukumo wa baadhi ya wabunge waliotuhumiwa kujihusisha na rushwa, pamoja na baadhi ya waliokuwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kabla ya kuvunjwa.
Kadhalika, Ndugai katika mkutano wake na vyombo vya habari alisema suala la ripoti hiyo kusomwa bungeni au vinginevyo linategemea uamuzi wa Kamati ya Uongozi ya Bunge.

Ndugai alisema baada ya kamati kuwasilisha ripoti kwa Spika, Kamati ya Uongozi ya Bunge itakaa kujadili na kama itaona kuna umuhimu wa kuingizwa katika ratiba ya vikao vya Bunge ijadiliwe.
Alisema Vifungu 114 (17) na 119 (1) hadi (6) vya Kanuni za Bunge, Toleo la 2007 kwa pamoja vinampa madaraka Spika kuhusu utaratibu wa kufuata katika uwasilishaji wa taarifa bungeni.
Kamati hiyo iliyoundwa na Spika ilikuwa chini ya Ngwilizi ambaye ni Mbunge wa Mlalo, ina wajumbe; Said Arfi (Mpanda Kati), John Chiligati (Manyoni Mashariki), Goesbert Blandes (Karagwe) na Mbunge wa Viti Maalumu, Riziki Omary Juma. Kamati hiyo ilimaliza kazi yake na kuiwasilisha kwa spika tangu Septemba 20 mwaka huu.

Kamati za vyama

Kamati za vyama bungeni zinatarajiwa kufanya vikao vyake leo asubuhi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Ofisa Habari wa Bunge, Prosper Minja alisema
Kamati nyingine za Bunge hazijakutana kutokana na wabunge wengi kuwa safarini kwenda mjini Dodoma kuhudhuria kikao cha Bunge.

"Kwa taarifa tulizopokea sasa ni kwamba kamati zimeshindwa kukutana kutokana na wabunge wengi kuwa njiani kuja mjini hapa, hivyo kwa vyovyote kesho (leo) Bunge litakuwa ni fupi ili wabunge wapate nafasi ya kuandaa utaratibu mzima wa ratiba za vikao," alisema Minja.
Alisema leo mara baada ya kuanza kwa kikao hicho, Bunge litatoa nafasi ya maswali na majibu ambayo Serikali itayajibu kabla ya kuahirishwa.

Mara baada ya kuahirishwa saa nne asubuhi, kamati za vyama zitakutana kupitia mambo mbalimbali kabla ya kuingizwa kwenye kamati mbalimbali za bunge.
Moja ya mambo yanayotarajiwa kutawala katika kamati za vyama ni pamoja na wabunge wa CCM kujiweka sawa kwa ajili ya kusaidia kupitishwa kwa ripoti ya Kamati ya Ngwilizi.
Kingine kitakachojadiliwa katika Mkutano huu wa Bunge ni muswada binafsi kuhusu fao la kujitoa la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Tayari Mbunge wa Kisarawe, Suleiman Jaffo na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika wamewasilisha miswada yao kwa Katibu wa Bunge, Tomas Kashillilah.
===================================================================================================
 
Hata mimi nmshangaa Spika na Kamati yaker ya uongozi. Inaelekea lengo lao ni kulindana kwani walioonekana kujihusisha na rushwa ni wabunge wa CCM. Katiba mpya iruhusu mwananchi ye yote kumfikisha mahakama kuu Spika kama atapindisha haki kwa kanununi yo yote ile. Kwani hayuko juu ya Katiba huyo.
 
Mimi binafsi naungana na baadhi ya Wabunge wa Upinzania ambao walipendekeza kuna Kanuni za Bunge zimepitwa na wakati, ziliandaliwa wakati wa Chama Kimoja.

Ni wakati sasa kuzipitia tena na baadhi zifutwe kabisa.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Sidhani kama sheria kweli zimepitwa na wakati,ni tatizo la viongozi wetu waliomadarakani kuzitumia vibaya.Nina uhakika kanuni hizo hizo zingeweza kulipeleka taifa letu hatua kumi mbele kama zingetumiwa kiadilifu na kwa muogopa mungu aliyetupa uhai.
Spika anauwezo wa kutumia sheria hizo vizuri kwa manufaa ya taifa letu badala ya kuogopa watu na kuficha uovu.Ifike mahali Spika wetu Anna Makinda aangalie miguu yake na roho yake je ana uhalali wa kwenda kanisani kila siku asubuhi wakati anachokifanya kinahalalisha uovu?Ajipime halafu achukue hatua!:confused:
 
Ripoti ya kamati ya Ngwilizi imewasafisha wabunge na tuhuma za ukaji Rushwa,na wanataka kuibana Serikali kua ina makosa hasa Waziri Prof .Muhongo,kwa upande wake yenyewe Serikali (Muhongo) imedai inao ushaidi usio na shaka kua wabunge walikula Rushwa.
Hivyo Spika anataka kuikalia hiyo Ripoti akitaka kuwaokoa wabunge wenzake,kwasababu anajua Prof Muhongo huwa hakurupuki mara nyingi anaongea kile anachomaanisha.
Wabunge wanajaribu kulindana kabla ripoti hiyo ilivyoandaliwa.
 
Hata mimi nmshangaa Spika na Kamati yaker ya uongozi. Inaelekea lengo lao ni kulindana kwani walioonekana kujihusisha na rushwa ni wabunge wa CCM. Katiba mpya iruhusu mwananchi ye yote kumfikisha mahakama kuu Spika kama atapindisha haki kwa kanununi yo yote ile. Kwani hayuko juu ya Katiba huyo.
Ni vema ukapeleka maoni kwenye tume ili yaingizwe,badala ya kulalamika!
 
Wanajamvi kuna yeyote ambae ana nakala ya ripoti hiyo?..ninaamini ni haki yetu sisi walipakodi kuelewa hawa wanatume walikuwa wanafanya nini na pia tujue walichobaini lakini muhimu sana ni kutumia taarifa za tume hyo kuona weledi, umakini na uzalendo wa hawa wenzetu walioshiriki katika tume. La mwisho ambalo ninahisi ni kubwa ni hili lakuona bunge kama chombo chetu cha uwakilishi kinatuwakilisha kweli katika kuisimamia serikali iliyoko madarakani.
 
Ripoti ya kamati ya Ngwilizi imewasafisha wabunge na tuhuma za ukaji Rushwa,na wanataka kuibana Serikali kua ina makosa hasa Waziri Prof .Muhongo,kwa upande wake yenyewe Serikali (Muhongo) imedai inao ushaidi usio na shaka kua wabunge walikula Rushwa.
Hivyo Spika anataka kuikalia hiyo Ripoti akitaka kuwaokoa wabunge wenzake,kwasababu anajua Prof Muhongo huwa hakurupuki mara nyingi anaongea kile anachomaanisha.
Wabunge wanajaribu kulindana kabla ripoti hiyo ilivyoandaliwa.
Ndiyo ukweli huo mkuu,wameitafutia sababu ili isisomwe.Kama ni madhara ya kuilikisha waliyajuwa,na wamefanya makusudi,halafu kweli sisi ni wadanganyika,certainly ni upepo tu utapita!
 
Sidhani kama sheria kweli zimepitwa na wakati,ni tatizo la viongozi wetu waliomadarakani kuzitumia vibaya.Nina uhakika kanuni hizo hizo zingeweza kulipeleka taifa letu hatua kumi mbele kama zingetumiwa kiadilifu na kwa muogopa mungu aliyetupa uhai.
Spika anauwezo wa kutumia sheria hizo vizuri kwa manufaa ya taifa letu badala ya kuogopa watu na kuficha uovu.Ifike mahali Spika wetu Anna Makinda aangalie miguu yake na roho yake je ana uhalali wa kwenda kanisani kila siku asubuhi wakati anachokifanya kinahalalisha uovu?Ajipime halafu achukue hatua!:confused:

Zimepitwa na wakati kwasababu zinatoa mwanya wa viongozi wetu kuzitumia vibaya. zirekebishwe ili zisitoe nafasi kama hii
 
Mi sina hamu na kinachojadiliwa huko kama hawajarudisha fao la kujuitoa wafie wote humo humo ndani ya mjengo.Tume za nini kwani Tanzania imeanza kuibiwa leo, waachane na mambo ya tume wajadili mambo yanayowagusa direct wananchi kama fao la kujitoa
 
Wanajamvi kuna yeyote ambae ana nakala ya ripoti hiyo?..ninaamini ni haki yetu sisi walipakodi kuelewa hawa wanatume walikuwa wanafanya nini na pia tujue walichobaini lakini muhimu sana ni kutumia taarifa za tume hyo kuona weledi, umakini na uzalendo wa hawa wenzetu walioshiriki katika tume. La mwisho ambalo ninahisi ni kubwa ni hili lakuona bunge kama chombo chetu cha uwakilishi kinatuwakilisha kweli katika kuisimamia serikali iliyoko madarakani.

Ndugu ili kuficha ukweli Bwana Ndugu ai akatoa kitisho kuwa HAIRUHUSIWI KUWEKA REPORT HADHARANI kabla ya kupitishwa Bungeni.

Hivyo kila mmoja ataogopa kwa muda huu, na ndio Serikali yetu kila kitu wanafanya SIRI ili wananchi wasijue uozo wao.

Lakini yote yana mwisho tu haya.



MIZAMBWA
IANNIUMA SANA!!!
 
wale wabunge nagamba waliokuwa wanapiga kelele kwamba zito ndiyo amekula rushwa sasa hivi kimya wanaangalia ni jinsi gani ya kuficha uozo wa magamba wenzao,spika anataka kuwasevu,naibu spika kaweka mkwara,hao ndiyo ccm,tunasubiri watetezi wao watuambie humu jamvini nini kinaendelea
 
Repoti ya tume si sawa na research report ambayo inaweza wekwa hadharani for public use. Report ya tume hupelekwa kwa alieiunda. Labda huyo kama atataka kuiweka hadharani ndio public mtaiona lakini pia anaweza kutoiweka hadharani na akaamua kuchukua hatua kimyakimya. Ndio sheria na utaratibu wa tume. Tumlaumu aliyeunda tume na si tume kama tutafichwa matokeo.
 
Kwa utaratibu huu ilipaswa hata wakati wanauda Tume wasitutangazie kuwa kuna tume imeundwa kuchunguza jambo fulani. Wafanye siri pia kwa sababu haituhusu kuijua, kwa mtindo huo.

Na kama ikitangazwa basi i9na maana ni kwa manufaa ya umma wa Watanzania.



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Back
Top Bottom