Suphian Juma
Senior Member
- Apr 2, 2019
- 133
- 546
KIGWANGALA NA BASHIRU NI MAPACHA!!
Jana Desemba 04, 2022 kwenye mitandao ya kijamii pameibuka mjadala kuhusu Mabehewa ya Reli yetu tarajiwa ya kisasa ulioanzishwa na Mbunge wa Chama chetu cha Mapinduzi CCM wa Jimbo la Nzega, Mheshimiwa Dkt Hamis Kigwangala.
Niseme tu kama Mwanachama wenzake wa CCM nimeshtushwa sana, kwani dhambi aliyoifanya Dkt Bashiru dhidi ya mafanikio makubwa ya Rais Dkt Samia, ndiyo dhambi hiyo hiyo aliyoifanya Dkt Kigwangala. Hii dhambi inaitwa UNAFIKI WA KISIASA.
Naomba nizungumze kidogo na Mhe. Kigwangala kwani sio tu hoja zake juu ya hayo Mabehewa lakini pia uhalali (legitimacy) wake wa kuzodoa HADHARANI juhudi hizi zisizomithilika za Rais wetu Samia za kutekeleza miradi hii ya mikakati iliyoanishwa kwenye Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 inatia MASHAKA makubwa kwenye umma.
Dkt Kigwangala,
Unashangaa mabehewa kuletwa yaliyotumika (used) huku unasema huna shida na Rais wetu Dkt Samia wala Baraza la Mawaziri kwamba una shida na TRC;
1) Tuseme hujaona ripoti ya TRC na Serikali kuhusu hadhi ya Mabehewa hayo kupitia tovuti na mitandao ya kijamii kwamba hayo mabehewa yaliyowasili nchini ni MAPYA yametengenezwa na kampuni ya Sung Shin Rolling Stock Technology Limited ya nchini Korea Kusini na kwamba ni kwa ajili ya ECONOMY CLASS? Huiamini TRC? Humwamini Waziri Mbarawa? Humwamini Msemaji Mkuu wa Serikali Msigwa? Kwako mabehewa mapya unataka hadi yameremete kama vito vya thamani?
2) Na hata kama tuseme hayo mabehewa ni "used", je ni kitu cha kushangaa? Tuseme hukuisikia Hotuba ya Rais Dkt Samia aliposema; "... Sitaki kuficha hapa, tutanunua vya kuanzia, tutanunua vilivyotumika (used) lakini vyenye hali nzuri, tutavitengeneza reli ifanye kazi."? Halafu bado unasema huna shida na Rais? Unaona sahihi kutomwamini na kupingana na Mwenyekiti wako wa Chama hadharani? Unadhani sote ni watoto wa 'vidudu' hatuwezi kutafsiri?
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alienda hadi kiwandani huko Korea ya Kusini yanapotengenezwa mabehewa na injini za treni na akathibitishia umma wa dunia kwamba mabehewa yote yana viwango vya kimataifa vya treni ya kisasa na kuruhusu yaletwe nchini, wewe unasema ishu ya mabehewa si ya Baraza la Mawaziri wala Rais, ni ya TRC unamhadaa nani? Humwamini Waziri Mkuu, Humwamini Rais na Mwenyekiti wako wa Chama? Ooops!!
Hapo Twitter naona umeweka magazijuto lukuki ukihangaika kuonesha Mabehewa ya treni yaliyoletwa si yenye hadhi ya kutumiwa na treni ya kisasa tuliyoahidiwa, unamaanisha hujui utofauti wa madaraja katika vyombo hivi vya usafiri? Unataka First Class na Economy Class ziwe Sawa? Nauli zitakuwa Sawa? Mbona wewe kama Mbunge una Bima ya daraja la kwanza tofauti kabisa na wapiga kura wako wa Nzega wenye bima ya Afya ya elfu 30? Mbona huwa hutuwekei msururu wa posts kuonesha utofauti wa bima hizo na kupigania usawa?
Dkt Kigwagala,
Hold on:
Kupitia maandiko yako umesema mabehewa yaliyonunuliwa ni ya masafa marefu wakati kipande cha reli kilichokamilika ni cha Dar es Salaam hadi Morogoro; ulitaka Serikali ya Chama chetu cha Mapinduzi CCM inunue treni ya masafa mafupi halafu baadae reli ya Dar es Salaam hadi Mwanza ikikamilika Serikali iingie tena gharama ya kununua treni ya masafa marefu? Procurement ya Chuo gani hii umesomea Dkt?
Dkt Kigwangala, kwenye suala la manunuzi Usijifiche kwenye kivuli cha Shirika la Reli (TRC) Kaka yangu, wewe mtaje unayetaka kumtaja tujue moja, usizunguke mbuyu.
LEGITIMACY.
Kaka yangu Kigwangala unajua wazi implications za wewe Mbunge, Kigogo wa zamani wa Chama na Serikali tena wa ngazi ya juu kabisa (Baraza la Mawaziri) kukosoa juhudi za Serikali ya Chama chako hadharani; una immunity ya Bunge kusema Bungeni hujasema, unaogopa? Kuna Umoja wenu wa Wabunge wa CCM hujasema, kuna kuandika barua straight kwa Katibu Mkuu na hata Mwenyekiti wa Chama chetu hujaandika; UNAKUJA KUANDIKA TWITTER unataka tukuone una nia njema na Rais na Serikali yetu?
Dkt Kigwangala,
UNAFIKIRISHA!!
Suphian Juma Nkuwi,
Kada-CCM
Desemba 05, 2022.
Jana Desemba 04, 2022 kwenye mitandao ya kijamii pameibuka mjadala kuhusu Mabehewa ya Reli yetu tarajiwa ya kisasa ulioanzishwa na Mbunge wa Chama chetu cha Mapinduzi CCM wa Jimbo la Nzega, Mheshimiwa Dkt Hamis Kigwangala.
Niseme tu kama Mwanachama wenzake wa CCM nimeshtushwa sana, kwani dhambi aliyoifanya Dkt Bashiru dhidi ya mafanikio makubwa ya Rais Dkt Samia, ndiyo dhambi hiyo hiyo aliyoifanya Dkt Kigwangala. Hii dhambi inaitwa UNAFIKI WA KISIASA.
Naomba nizungumze kidogo na Mhe. Kigwangala kwani sio tu hoja zake juu ya hayo Mabehewa lakini pia uhalali (legitimacy) wake wa kuzodoa HADHARANI juhudi hizi zisizomithilika za Rais wetu Samia za kutekeleza miradi hii ya mikakati iliyoanishwa kwenye Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 inatia MASHAKA makubwa kwenye umma.
Dkt Kigwangala,
Unashangaa mabehewa kuletwa yaliyotumika (used) huku unasema huna shida na Rais wetu Dkt Samia wala Baraza la Mawaziri kwamba una shida na TRC;
1) Tuseme hujaona ripoti ya TRC na Serikali kuhusu hadhi ya Mabehewa hayo kupitia tovuti na mitandao ya kijamii kwamba hayo mabehewa yaliyowasili nchini ni MAPYA yametengenezwa na kampuni ya Sung Shin Rolling Stock Technology Limited ya nchini Korea Kusini na kwamba ni kwa ajili ya ECONOMY CLASS? Huiamini TRC? Humwamini Waziri Mbarawa? Humwamini Msemaji Mkuu wa Serikali Msigwa? Kwako mabehewa mapya unataka hadi yameremete kama vito vya thamani?
2) Na hata kama tuseme hayo mabehewa ni "used", je ni kitu cha kushangaa? Tuseme hukuisikia Hotuba ya Rais Dkt Samia aliposema; "... Sitaki kuficha hapa, tutanunua vya kuanzia, tutanunua vilivyotumika (used) lakini vyenye hali nzuri, tutavitengeneza reli ifanye kazi."? Halafu bado unasema huna shida na Rais? Unaona sahihi kutomwamini na kupingana na Mwenyekiti wako wa Chama hadharani? Unadhani sote ni watoto wa 'vidudu' hatuwezi kutafsiri?
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alienda hadi kiwandani huko Korea ya Kusini yanapotengenezwa mabehewa na injini za treni na akathibitishia umma wa dunia kwamba mabehewa yote yana viwango vya kimataifa vya treni ya kisasa na kuruhusu yaletwe nchini, wewe unasema ishu ya mabehewa si ya Baraza la Mawaziri wala Rais, ni ya TRC unamhadaa nani? Humwamini Waziri Mkuu, Humwamini Rais na Mwenyekiti wako wa Chama? Ooops!!
Hapo Twitter naona umeweka magazijuto lukuki ukihangaika kuonesha Mabehewa ya treni yaliyoletwa si yenye hadhi ya kutumiwa na treni ya kisasa tuliyoahidiwa, unamaanisha hujui utofauti wa madaraja katika vyombo hivi vya usafiri? Unataka First Class na Economy Class ziwe Sawa? Nauli zitakuwa Sawa? Mbona wewe kama Mbunge una Bima ya daraja la kwanza tofauti kabisa na wapiga kura wako wa Nzega wenye bima ya Afya ya elfu 30? Mbona huwa hutuwekei msururu wa posts kuonesha utofauti wa bima hizo na kupigania usawa?
Dkt Kigwagala,
Hold on:
Kupitia maandiko yako umesema mabehewa yaliyonunuliwa ni ya masafa marefu wakati kipande cha reli kilichokamilika ni cha Dar es Salaam hadi Morogoro; ulitaka Serikali ya Chama chetu cha Mapinduzi CCM inunue treni ya masafa mafupi halafu baadae reli ya Dar es Salaam hadi Mwanza ikikamilika Serikali iingie tena gharama ya kununua treni ya masafa marefu? Procurement ya Chuo gani hii umesomea Dkt?
Dkt Kigwangala, kwenye suala la manunuzi Usijifiche kwenye kivuli cha Shirika la Reli (TRC) Kaka yangu, wewe mtaje unayetaka kumtaja tujue moja, usizunguke mbuyu.
LEGITIMACY.
Kaka yangu Kigwangala unajua wazi implications za wewe Mbunge, Kigogo wa zamani wa Chama na Serikali tena wa ngazi ya juu kabisa (Baraza la Mawaziri) kukosoa juhudi za Serikali ya Chama chako hadharani; una immunity ya Bunge kusema Bungeni hujasema, unaogopa? Kuna Umoja wenu wa Wabunge wa CCM hujasema, kuna kuandika barua straight kwa Katibu Mkuu na hata Mwenyekiti wa Chama chetu hujaandika; UNAKUJA KUANDIKA TWITTER unataka tukuone una nia njema na Rais na Serikali yetu?
Dkt Kigwangala,
UNAFIKIRISHA!!
Suphian Juma Nkuwi,
Kada-CCM
Desemba 05, 2022.