MKEHA
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 716
- 1,144
Kuna wakati huwa nawaza na kufikiria nyuma kidogo naanza kufurahi. Miaka ishirini iliyopita Kigoma ilikuwa kama si sehemu ya Tanzania.
Umeme ulikuwa makao makuu tu ya mkoa yaani Kigoma Ujiji. Tena ukiwaka mara mbili tu kwa wiki.
Nilikuwa najua ratiba ya umeme kuwaka kuanzia Gungu, Masanga, SIDO, Mwanga sokoni,Kibilizi, Katubuka, Mlole,Majengo na Kilimahewa. Waliokuwa na uhakika wa umeme ni mjini kati na Mji mwema kwakuwa kule waliishi wanene.
Kutoka Kigoma kwenda Kasulu na Kibondo ilikuwa ni Safari ya kutwa nzima na mabasi yetu ya Adventure na Saratoga za wakati ule.
Kutoka Kigoma kwenda Manyovu na Muyama hakukuwa na mabasi bali magari ya mizigo tena ya kuvizia.
Kasulu pamoja na kuwa Mji mkubwa zilitawala kalabai, chemli na vibatali tu,huku Kibondo ikiwa kama mji wa kale wa enzi za ustaarabu wa Kichina yaani China Dynasty.
Hakuna aliyepangiwa kufanya kazi Kigoma aliyekubali kirahisi.
Sasa Kigoma imenza kuwa sehemu nzuri sana kwa kuishi. Barabara ya kuiunganisha na Tabora itakamilika muda si mwingi.
Hata ile ya kuiunganisha na Nyakanazi inaenda vizuri nimepita pale mpakani na mkoa wa Kagera daraja kubwa linajengwa na litaisha muda si mwingi.
Nimeona umeme ukiwaka kuanzia Kakonko, Kibondo yote,Kasulu na vijiji vyake,Heru juu,Kabanga, Muganza, Mwanga,Kasumo,Kalege, Muyama,Biharu,Nyamgali,Buhigwe,Muhaluro,Mnanila na kwingineko.
Mgao haupo tena,
Siku hizi hatusubirii tiketi za kulangua za train maana mabasi tele ya kwenda DSM,Mwanza,Bukoba,Arusha,Tabora,Mpanda na Sumbawanga.
Siku hizi kwenda Kasulu na Kibondo ni muda wowote.
Nimeona maji vijijini yakimwagika mitaani, barabara za vijijini zimeboreshwa sana.
Tunaweza kuwa tunaenda taratibu lakini tunasonga mbele.
Japo bado mkoa wote wa Kigoma tunatumia umeme wa generator lakini unatosheleza mahitaji ya umeme.
Kuishi kwingi ni kuona mengi, kuna vitu vimetokea mazingira yetu sikutarajia kama vingetokea nikiwa bado niko hai.
Mwezi uliopita nimekuta viguzo vya kuonyesha mwisho wa barabara vikiwa nyuma ya choo chetu badala ya kusikitika kwani nyumba yetu yote imeangukia kwenye hofadhi ya barabara lakini nilicheka kwa furaha kwani inawezekana nikaona barabara nzuri sana ya lami ikipita kijijini kwetu
And this happens once in life time.
Mungu nijalie nione mengi zaidi ambayo sikuyategemea kutokea nikiwa bado hai.
Umeme ulikuwa makao makuu tu ya mkoa yaani Kigoma Ujiji. Tena ukiwaka mara mbili tu kwa wiki.
Nilikuwa najua ratiba ya umeme kuwaka kuanzia Gungu, Masanga, SIDO, Mwanga sokoni,Kibilizi, Katubuka, Mlole,Majengo na Kilimahewa. Waliokuwa na uhakika wa umeme ni mjini kati na Mji mwema kwakuwa kule waliishi wanene.
Kutoka Kigoma kwenda Kasulu na Kibondo ilikuwa ni Safari ya kutwa nzima na mabasi yetu ya Adventure na Saratoga za wakati ule.
Kutoka Kigoma kwenda Manyovu na Muyama hakukuwa na mabasi bali magari ya mizigo tena ya kuvizia.
Kasulu pamoja na kuwa Mji mkubwa zilitawala kalabai, chemli na vibatali tu,huku Kibondo ikiwa kama mji wa kale wa enzi za ustaarabu wa Kichina yaani China Dynasty.
Hakuna aliyepangiwa kufanya kazi Kigoma aliyekubali kirahisi.
Sasa Kigoma imenza kuwa sehemu nzuri sana kwa kuishi. Barabara ya kuiunganisha na Tabora itakamilika muda si mwingi.
Hata ile ya kuiunganisha na Nyakanazi inaenda vizuri nimepita pale mpakani na mkoa wa Kagera daraja kubwa linajengwa na litaisha muda si mwingi.
Nimeona umeme ukiwaka kuanzia Kakonko, Kibondo yote,Kasulu na vijiji vyake,Heru juu,Kabanga, Muganza, Mwanga,Kasumo,Kalege, Muyama,Biharu,Nyamgali,Buhigwe,Muhaluro,Mnanila na kwingineko.
Mgao haupo tena,
Siku hizi hatusubirii tiketi za kulangua za train maana mabasi tele ya kwenda DSM,Mwanza,Bukoba,Arusha,Tabora,Mpanda na Sumbawanga.
Siku hizi kwenda Kasulu na Kibondo ni muda wowote.
Nimeona maji vijijini yakimwagika mitaani, barabara za vijijini zimeboreshwa sana.
Tunaweza kuwa tunaenda taratibu lakini tunasonga mbele.
Japo bado mkoa wote wa Kigoma tunatumia umeme wa generator lakini unatosheleza mahitaji ya umeme.
Kuishi kwingi ni kuona mengi, kuna vitu vimetokea mazingira yetu sikutarajia kama vingetokea nikiwa bado niko hai.
Mwezi uliopita nimekuta viguzo vya kuonyesha mwisho wa barabara vikiwa nyuma ya choo chetu badala ya kusikitika kwani nyumba yetu yote imeangukia kwenye hofadhi ya barabara lakini nilicheka kwa furaha kwani inawezekana nikaona barabara nzuri sana ya lami ikipita kijijini kwetu
And this happens once in life time.
Mungu nijalie nione mengi zaidi ambayo sikuyategemea kutokea nikiwa bado hai.

