Kigoma sio ndondocha

Kigoma sio ndondocha

hatuko tayari kuongozwa na mnafiki

Haya bana, endeleeni kuongozwa na Viongozi wenye kuithamini Kaskazini tu!

Katika miaka yote ya siasa mkoani Kigoma, jimbo la Zitto K limekuwa na maendeleo kupita majimbo mengine ya KG, ninatamani Ubunge ungekuwa wa mikoa Zitto akawa mbunge wa mkoa na yakafanyika yaliyofanyika jimboni kwake.

Siasa ni siasa tu, umewahi kujiuliza hela za Sabodo za visima zilienda wapi? Maana hakuna kisima hata kimoja kilichochimbwa na wala chama hakikutoa mrejesho wa matumizi ya ile fedha.

Hakuna mwanasiasa atakayekuneemesha mkuu, wanatetea matumbo yao tu.
 
Haya bana, endeleeni kuongozwa na Viongozi wenye kuithamini Kaskazini tu!

Katika miaka yote ya siasa mkoani Kigoma, jimbo la Zitto K limekuwa na maendeleo kupita majimbo mengine ya KG, ninatamani Ubunge ungekuwa wa mikoa Zitto akawa mbunge wa mkoa na yakafanyika yaliyofanyika jimboni kwake.

Siasa ni siasa tu, umewahi kujiuliza hela za Sabodo za visima zilienda wapi? Maana hakuna kisima hata kimoja kilichochimbwa na wala chama hakikutoa mrejesho wa matumizi ya ile fedha.

Hakuna mwanasiasa atakayekuneemesha mkuu, wanatetea matumbo yao tu.

wewe una matatizo na huijui Kigoma. Hakuna lami unayoweza kujenga kuunga mkoa bila kupita Mwandiga.

Ni sawa na kusema huwezi kuunga Dar kwa lami bila kupitia mkoa wa Pwani
 
wewe una matatizo na huijui Kigoma. Hakuna lami unayoweza kujenga kuunga mkoa bila kupita Mwandiga.

Ni sawa na kusema huwezi kuunga Dar kwa lami bila kupitia mkoa wa Pwani

Barabara ya Kigoma Kasulu inapiata Mwandiga? Au pale kwenye junction ndo unapaita Mwandiga!

Ukizungumzia kwenda Manyovu sawa ila sio Kasulu. Na kwa nini lami iishie Kidahwe?
 
ujumbe wako wana kigoma wameusikia lakini kuingia chama kingine kwa kutumia utashi wako huo sio undondocha kukaa kwenye chama bila kutumia utashi wako huo ndo undondocha by the way una define vipi undondocha????

Dada uko vizuri sana, umenigusa na hayo maneno yako machache. Big up sana. Watu wengine wanaleta thread ambazo ni za kumlazimisha mtu kuendelea kuwa mtumwa wa kikundi Fulani ambacho kimeanza kupoteza mvuto.
 
Kila mtu atawashangaa watu wa Kigoma akisikia kuwa watu wa Kigoma wamejiunga kwa wingi na chama kipya cha siasa cha ACT. Ingawa kila mtu anayo haki ya kujiunga na chama chochote cha siasa katika mfumo wa vyama vingi lakini haki hiyo lazime iwe na uhalisia ndani yake. Zitto alipata umaarufu kupitia chadema chama ambacho sasa kimekuwa hadi kufikia kuwa chama kikuu cha upinzani nchini ambacho kinaogopwa sana na chama cha CCM pamoja na watu wengine ambao wanadhani kuwa kama CCM kitashindwa na maslahi yao nayo yatakuwa yako hatarini.

Chadema pamoja na Zitto ndani ya chadema na mikakati yao walikuwa wanakaribia sana kulishika makalio dume la nyati. Juhudi hizi za kulipapasa dume makalio zinadhoofishwa na akina Zitto na washirika wake kwa kuanzisha tuhuma nzito kwamba chama ambacho alijiunga nacho akiwa na umri wa miaka 16 tu eti hakina demokrasia. Hii sio kweli hizo ni juhudi mahususi za kulikwepesha dume na aibu ya kushikwa makalio yake kirahisi japo kwa kuondoa angalau hata kura 100 tu kutoka kwa wapinzani.

Wananchi wa Kigoma kujiunga na chama kinda cha ACT kwa kumfuata Zitto watakuwa wanaingia kwenye historia ya watanzania waliopinga na kuchelewesha kuondoa dhuluma nchini sawa na akina Zuberi Mtemviu enzi za TANU na Nyerere. Zitto anatumia ukabila (U-Kigoma) na uelewa mdogo wa wananchi katika kufanya biashara ya kuchelewesha kuing'oa CCM madarakani.

Hakuna mtu mwenye akili lazini ambaye ataamini kuwa Zitto amefanya yale aliyoyafanya ya kudai uongozi ndani ya chadema kwa njia za pembeni na kukipeleka chama mahakamani kwasababu ndani ya chadema hakukuwa na demokrasia ya kutosha, hii sio bahati mbaya tu, bali kuna jambo.

Kigoma kuweni macho na wanasiasa hawa wanaowarudisha nyuma juhudi zenu za kutafuta nafuu za kisiasa kwa kuanzisha vyama vipya vitakavyowachelewesha kuwafikisha nchi ya ahadi. Kataeni kuwa ma-ndondocha. Binafsi ninawasikitikia wananchi watakaonaswa na mtego wa kitoto kama huu kwa kujiunga na ACT.

haya sasa matusi, zile dharau zenu na chama chenu ndo mnaanza kututafuta tena? Tuacheni watu wa Kigoma tufanye mabadiliko
 
Data zipo, lakini data ambayo wewe ni rahisi kuielewa na kuikumbuka ni hii hapa: Zitto amedai kuwa chadema hakuna demokrasia ya kweli, inahubiri mambo ambayo itayatekeleza itakapokamata dola ambayo yoyo yenyewe haiyatekelezi ndani ya chama, hivyo chadema itawezaje kuchukua nchi?. Kwani chadema ni nini? chadema ni mkusanyiko wa viongozi, wanachama na wapenzi wake, Zitto alikuwa mwanachama na kiongozi muhimu wa chadema ambaye alipaswa kusikika kwa viongozi, wanachama na wapenzi wote wa chadema akishauri chama kuhusu mambo yasiofaa kwa demokrasia ndani ya chama kwa kutumia vikao halali vya chadema. Badala yake Zitto amesikika pale tu alipokuwa anajiandaa kufanya mapinduzi ya uongozi kwa njia zisizo rasmi. Ndiyo maana tunasema Zitto alikosea kwa makusudi sio kwa bahati mbaya, maana "kunguru hana kibiongo ukiona kibiongo ameinama anaokota kitu na kitu hicho kinaweza kuwa kijiti, kijiwe, nyama yako, nguo yako ya ndani, au kitu kingine cha thamani, hivyo wahi kumkurupusha kabla hajaruka nacho ukapata hasara". Ndiyo maana nawapongeza chadema kumkurupusha kunguru kabla hajasababisha uharibifu mkubwa.

Njia rasmi kwenu ni zipi? Mwaka 2009 alitaka kugombea kihalali na kikatiba mkamwomba ajitoe eti amwachie Mbowe amalize vipindi viwili kama katiba inavyosema, baada ya yeye kukubali kuondoa jina mkabadili katiba na kuamua kwamba Mbowe awe mwenyekiti mpaka atakapoamua mwenyewe (Hiyo ni demorasia?).

Tena mabadiliko yalifanyika bila vikao rasmi, leo hii mmemfukuza amekubali kuwapisha sasa mnaweweseka wa kuwatungia majina mbalimbali watu wanaoamua kumfata Zitto, ni ubaguzi mbaya huu.

Ubaguzi unaanza na kupeana majina mabaya, kama hayo ya usaliti, ndondocha, wapumbavu etc.

Kama wewe sio ndondocha kaa nalo moyoni, by the way hujui kesho itakuwaje maana huyu unayemwamini leo kesho anaweza kukushangaza!

In short CDM imejaa ubaguzi wa kidini na kikanda, ulafi wa madaraka na mali kwa viongozi wakuu, ujivuni na maringo, hela za mzee Sabodo wamegawana badala ya kuchimba visima.

Hii ACT iliyoanzishwa leo haitakuja kuwa na tofauti na vyama vingine, ni wale wale tu, wanasiasa kutaka kula kwa kutudanganya eti wanatusaidia, wote waongo waongo tu.

Sasa nyie kalieni ushabiki huku wenzenu wananeemeka.
 
Nikipewa maelezo leo na kiongozi mkubwa wa vijana Wilaya ya BUHIGWE ameonesha kufurahi sana kumunasa zito na kufanikiwa kufitinisha chama cha Chadema
amesema
Cdm ilikuwa imetukalia koo tukaona wakumukamata ili vuluge chama ni zzk sasa hv tunaenda kushinda bila ubishi
Ameongeza kuwa Ccm walikuwa hawaja amini kama kweli anatenda yaliyo yao.Leo ndo napata ukwel inauma sana
 
ujinga mtupu,okiwa chadema safi,ukiwa ACT unakuwa mkabila.kusini ina wabunge wengi wa ccm maendeleo yako wapi,inaonesha ni jinsi gani gani jiti lilivyo wachoma na sasa mnahangaika nalo.
 
mkuu nilikua sijajua hivi kumbe zito kabwe ni muanzilishi wa chama cha ACT??
naomba vizibitisho,napenda kulifahamu hili

Bado unaomba uthibitisho??? nyinyi tunawaambia kila siku akili zenu hazina akili hamwezi kuona jambo likiwa bado sio dhahiri, aibu yako. Noa ubongo sio mapanga dada.
 
Back
Top Bottom