Kigoma mwisho wa reli

http://www.flickr.com/photos/74938124@N00/6352175925/
4286324462_32b4fab6bd_b.jpg
spaceball.gif


4286407112_814d4078f2_b.jpg
spaceball.gif
4285583445_76ea6af2a4_b.jpg
spaceball.gif
 
Kama shirika la reli lingekuwa linaendeshwa kwa uadilifu, Kigoma ingeweza kuwa "terminal" ya biashara yoye ya Congo Mashariki. Ni swala la kutokutumia rasilimali ya miundombinu na nafasi ya kijiografia vizuri. Badala ya umaskini na kuzorota kiuchumi, Kigoma ingeweza kuwa "gateway" ya biashara. Umaskini wa Tanzania ni wa kujitakia. Cha kusikikisha ni kuwa hatutaweza kuondoa umaskini kama tukiendelea kwa mwendo na mtimdo huu. Anagalau sasa barabara ya Tabora Kigoma inawekwa lami.
 
Jambo moja ambalo wengi hatulijui ni kuwa Vijiji vya Kigoma vimendelea sana vikilinganishwa na sehemu nyingine hapa nchini.Kwa mfano maeneo ya Manyovu, Kalinzi, Mwandiga n.k. yako juu sana kulingana au kukaribia maeneo ya Uchagani. Tatizo lililokuwa linasumbua ni nishati ya umeme na miundombinu ya barabara za kuunganisha mkoani na nje ya mkoa.Mwelekeo ulioko ni mzuri kwani Kigoma mjini sasa wana umeme angalau wa kuaminika na nafikiri kwa wakati huu wilaya za Kasulu na Kibondo zitakuwa zimeshapatta umeme. Ikumbukwe kuwa wananchi wa vijijini kama Kalinzi na Manyovu tangu zamani wana mwamuko wa kutumia jenereta na umeme wa jua. Kwa upande wa barabara, iko ya lami kutoka Kigoma mjini nadhani kwa wakati huu itakuwa imeishafika Manyovu hadi mpakani na Burundi. Kwa upande wa ile ya Kigoma kuunganisha na mikoa ya Magharibi, lami imefikia Kazuramimba. Ukweli ni kuwa Kigoma iko juu na wananchi wana mwamko wa maendeleo tofauti na taswira iliyoko kwa baadhi ya watu wengi ambao hawajawahi kufika Kigoma hususan maeneo ya vijijini.
 

Mkuu umenikumbusha mbali sana. Hapa panaitwa Katonga,nje kidogo ya mji maeneo yenye shughuli za uvuvi watu huwa wapo busy 24/7( nimekumbuka hicho kibanda chenye katani hapo juu.Kipo mwanzoni mwanzoni upande wa kulia as you approach the shore) . Wavuvi wanaamka saa moja usiku hadi saa moja asubuhi then wachuuzi wanaingia mzigoni. Fascinating lol!!
 
Back
Top Bottom