Kigoma iko mbele kwa saa moja!

Kigoma iko mbele kwa saa moja!

Tanzania tunatumia masaa ya kwenye longitudo 45 mashariki ya greenwich. Mji wa Kigoma upo nyuzi 29 mashariki. Hapo pana tofauti ya nyuzi 16. Kwenye masaa, nyuzi 15 ni sawa na saa 1. Hivyo masaa wanayotumia Kigoma na masaa halisi kunatofauti ya saa moja.
Inabidi wana Kigoma muanze kutumia masaa yenu halisi.
Khaa!! Walimu wetu walikuwa wavumilivu kwelikweli. Kigoma ni nini na Tanzania ni nini?? Unajua sheria ya nchi moja kuwa na nyanda 2 za wakati zikoje? Tuwe tunajifunza kwanza ili tujitoe ujinga
 
Ningekuwa mimi ni mkuu wa mkoa wa Kigoma ningetumia udikteta kubadili majira ya saa.
 
Haitakua mbele lisaa limoja itakua saa moja nyuma na ndio masaa yanayotumika burundi.hivyo kigoma inapaswa kutumia masaa sawa na burundi
 
Kigoma Haiko Tanzania Kiukweli Nyerere Alifanya Yake
 
kwa hiyo ndo iko mbele au nyuma mkuu? ni jiografia gani unatumia?
 
Nice discussion so far maana wenye kujifunza ama kujikumbusha tumefanya hivyo. Well done mleta mada👏👏👏✌✌
 
Nchi za Afrika Mashariki zinatumia longitudo nyuzi 45 katika ku calculate muda. Kila nchi/ukanda kunakuwa na standard time na time zone zinazotumiwa na nchi/kanda nzima, hii inasaidia kutokuwa na saa/nyakati tofauti katika nchi moja. Kwa hiyo eneo lolote ndani ya Afrika Mashariki litakuwa na muda unaofanana bila kujali lipo katika nyuzi ngapi. Bila standard time ingetupasa kubadili majira yaa saa kila tunapotoka eneo moja hadi lingine ndani ya nchi husika.
 
Back
Top Bottom