Kigoma iko mbele kwa saa moja!

Kigoma iko mbele kwa saa moja!

Haiwezekani kamwe kwa Kigoma kuwa saa moja mbele. Latitudes na longitudes za Kigoma zinaweza kuifanya Kigoma kuwa saa moja nyuma na sio mbele kama unavyosema Mh Red Giant .

Halafu time zones hazifuati longitudes na latitudes pekee. Geographical boundaries zinahusika pia na ndio maana muda (time) wa Kigoma ni sawa na muda (time) wa Tanzania kwa ujumla na si vinginevyo .
nazungumzia kwa sasa kigoma wako saa moja mbele. ni kweli hizi time wana set kwa mipaka na kurahisisha mambo.
 
tanzania tunatumia masaa ya kwenye longitudo 45 mashariki ya greenwich. mji wa kigoma upo nyuzi 29 mashariki. hapo pana tofauti ya nyuzi 16. kwenye masaa, nyuzi 15 ni sawa na saa 1. hivyo masaa wanayotumia kigoma na masaa halisi kunatofauti ya saa moja.
inabidi wana kigomamuanze kutumia masaa yenu halisi.

Upo sahihi kwamaba kuna tofauti ya saa moja lakini Kigoma itakuwa nyuma sio mbele!
 
tanzania tunatumia masaa ya kwenye longitudo 45 mashariki ya greenwich. mji wa kigoma upo nyuzi 29 mashariki. hapo pana tofauti ya nyuzi 16. kwenye masaa, nyuzi 15 ni sawa na saa 1. hivyo masaa wanayotumia kigoma na masaa halisi kunatofauti ya saa moja.
inabidi wana kigomamuanze kutumia masaa yenu halisi.
mbele au nyuma mkuu?
 
Kwani kuna mtu huwa anabadili saa akitoka dar kwenda kigoma?!
 
Kimahesabu ni sahihi. Kutokana na matumizi ya pamoja ya muda ktk taifa, ndipo mambo ya time zone yanapohusika.
Kinyume na hivyo, kungekuwa na tofauti ya dakika tano, saba, kumi, n.k baina ya maeneo kadhaa ya (mikoa na wilaya) nchi moja, hasa nchi kubwa kama Tanzania. Mataifa yenye majimbo makubwa kama USA wanayo tofauti ya masaa baina ya majimbo.
 
ninamaanisha kwa sasa kigoma wako mbele. nimetumia kigoma yenyewe kama reference. wako saa moja mbele kuliko walivyotakiwa kuwa.

wala cyo kigoma tu! kuanzia tabora, shinyanga, mwanza, kagera ukiamka saa 12 unadhani saa 10 usiku. lakini dar saa 11 jua linachomoza.
 
tanzania tunatumia masaa ya kwenye longitudo 45 mashariki ya greenwich. mji wa kigoma upo nyuzi 29 mashariki. hapo pana tofauti ya nyuzi 16. kwenye masaa, nyuzi 15 ni sawa na saa 1. hivyo masaa wanayotumia kigoma na masaa halisi kunatofauti ya saa moja.
inabidi wana kigomamuanze kutumia masaa yenu halisi.

kigoma ibaki kama ilivyo ila dar isogezwe muda. ili saa saa 11 alfajiri iwe saa 12asub!
 
ukiweza kutofautishi kati ya longtude time na time zones, utapata jibu kwa nini kigoma inatumia saa za east africa
 
Mleta maada geography imekupiga chenga sana. Hujua mashariki wala magharibi na wapi muda unakuwa mbele au nyuma. Usilete uzi kama huna maarifa nao. Utaishia kuaibika maana jf ina watalaam wa kila aina
 
Kigoma iko magharibi mwa Malawi lakini Kigoma ipo mbele lisaa limoja kwa muda na tujue kua chanzo cha kua hivi ni kurahisisha utawala katika nchi moja. Rwanda na Burundi zingekua sehemu ya Tanzania kama ilivyokua enzi za ukoloni wa Ujeruman basi nazo pia zingetumia longitudo 45. DRC pamoja na ukubwa wake wote lakini inatumia nyuzi 30 yaan Lubumbashi ni sawa na Kinshasa.
 
Mleta maada geography imekupiga chenga sana. Hujua mashariki wala magharibi na wapi muda unakuwa mbele au nyuma. Usilete uzi kama huna maarifa nao. Utaishia kuaibika maana jf ina watalaam wa kila aina
naomba unisahihishe nilipokosea.
 
Kigoma sio Tanzania Nyerere aliuiba mkoa wa Burundi. Ndio maana ata watu wa huko hatufanani nao.
 
Back
Top Bottom