ELIFURAHA MAKOMBE
Senior Member
- Dec 22, 2012
- 176
- 22
Nyie wenyewe hamna umoja! hivi watu kumi wanaweza kusumbua mtaa mzima mkiamua kuwashughulikia? mbona hawaendi kuiba Kitunda!? acheni uoga!
sio kwamba wapo 10 na wanajulikana, ila mara nyingi wanatembea kundi la watu kama kumi hivi usiku wakiwa na silaha za visu, halafu kuna wezi wengi sana kana kwamba tupo Mogadishu kumbe tupo Kigamboni Tanzania yaani wezi huku wanachekewa. labda umoja unaongelea wewe basi na wanafunzi wawe wanatembea kwa makundi kama wenyewe wakiwa 10 basi wanafunzi wawe 20 pamoja na silaha za visu, na wakitoka chuo watoke kwa makundi na silaha zao. na wakienda kutafuta mahitaji basi waende kwa makundi na silaha zao. ndio umoja unaomaanisha!? tumekuja kusoma na sio kupambana na wezi! jukumu la kupambana na wezi ni la polisi.