Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,639
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 33
Profesa Mshana akiwa amechanganyikiwa kabisa, akaamua kumpigia simu Dk. Rwegoshora ili wajaribu kucheza na sheria waweze kuwatoa wake zao pamoja na Genesis, lakini majibu aliyopewa na Dk. Rwegoshora yalimchanganya sana, alimwambia kila mmoja ahangaike na msalaba wake mwenyewe!
Hilo lilimchanganya Profesa Mshana lakini halikutosha, simu ilikatwa akiwa bado anajaribu kumshawishi! Kitendo cha kukatiwa simu, kikazidi kumtibua na kuzidisha giza nene katika wazo la kumtoa mwanaye pamoja na mkewe kwenye mkono wa sheria.
Je, nini kitatokea? Genesis na mama yake, mama Bianca, Dulla, Festo, Patrick na Farida watatoka? SONGA NAYO...
“AMENIKATIA simu?” Profesa Mshana akatamka kwa sauti kubwa.
“Haiwezekani!” Akajijibu tena mwenyewe.
Tukio lile lilimchanganya sana kichwa chake, likatoa taswira mpya kabisa katika safari yake ya kumtoa mwanaye pamoja na mkewe jela! Kitanzi kilionekana waziwazi mbele ya familia yake, jambo ambalo hakutaka kuliruhusu litokee.
“Lazima nifanye jambo fulani hapa,” akawaza tena.
Ni kweli ilikuwa lazima afikirie jambo fulani la kufanya kwa ajili ya mkewe na mwanaye. Yeye kama baba wa familia, alitakiwa kuumiza kichwa ili aweze kuiondoa familia yake katika hatari ambayo ilikuwa wazi kabisa.
Ubongo wake ukafanya kazi zaidi ya kawaida, hapo akawaza sana lakini mwisho wa kikomo cha mawazo yake ukagonga kwa Dk. Rwegoshora ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwamba yeye ndiye kila kitu.
Kama ni kweli alitaka kufanikiwa kuwatoa mtoto wake pamoja na mkewe ndani, lazima muunganiko wao ufanye kazi sawasawa, vinginevyo ingekuwa ndoto kwake kufanikiwa!
“Lazima nizungumze naye...” akawaza.
Wazo lake lilikuwa na nguvu sana, kitu pekee alichoona kinafaa kufanyika ilikuwa ni kumpigia simu. Mara moja akanyanyua simu yake haraka na kubonyeza tena namba za Dk. Rwegoshora. Simu iliita kwa muda mfupi sana, ikapokelewa.
“Sema nakusikiliza!” Alikuwa ni Dk. Rwegoshora akizungumza kwa sauti iliyosoma majonzi na kisasi.
“Ndugu yangu tuliza hasira!”
“Hasira?”
“Ndiyo naona una hasira sana!”
“Unahisi sikutakiwa kuwa nazo siyo?”
“Sijasema hivyo Rwegoshora ndugu yangu. Unajua kama ni maji kumwagika yameshamwagika, sasa tuangalie namna ya kuwatoa hawa watu kwenye matatizo.”
“Tunawatoa akina nani?”
“Tuliza moyo ndugu yangu, naamini unajua nazungumzia akina nani, lakini hasira ndiyo inakufanya unijibu hivyo!”
“Sikiliza Mshana, sina muda wa kuendelea kupoteza kwenye simu, nina mambo mengi sana muhimu ya kufanya. Kikubwa ambacho unatakiwa kufahamu, juu ya suala hili, kila mmoja ahangaike kivyake!”
“Sisi ni ndugu lakini?”
“Undugu wetu ndiyo usababishe mwanangu afe?”
“Hapana!””Mke wangu awekwe ndani?”
“Hayo yameshatokea, tunatakiwa kuangalia mbele kwa sasa.”
“Sina mbele nyingine na wewe, naona hata huo urafiki wetu wa kinafiki uishie hapa, kila mtu ahangaike kivyake!” Akasema Dk. Rwegoshora kwa kumaanisha.
“Lakini sikikiliza rafiki yangu, unajua...” akasema Profesa Mshana hata hivyo hakusikia dalili yoyote ya Dk. Rwegoshora kuwa hewani.
“Halooo...halooo...” alikuwa akiita, lakini baadaye akagundua kwamba Dk. Rwegoshora alikuwa amemkatia simu.
Hili ni tukio la pili la aina hiyo kufanywa na Dk. Rwegoshora, rafiki yake mkubwa ambaye walishibana. Hakuhitaji mtu yeyote wa kujitokeza kumwambia kwamba harufu ya urafiki wao kufikia tamati ilikuwa inanukia. Kila kitu kilikuwa wazi kabisa, kwamba hasira ya Dk. Rwegoshora zilikuwa kali na hakuona taabu yoyote kuvunja urafiki wao.
“Si neno, nitajua cha kufanya...ni mwanaume, mwenye elimu, siyo lazima kila kitu kitafanikiwa kupitia kwake. Nitatumia uzoefu wangu kuhakikisha hili tatizo linaisha. Najua nitaweza!” Akajipa moyo Profesa Mshana.
***
Simu ya mezani kwake iliita kwa muda mrefu sana, bila kuipokea. Kwa kawaida, OCID Wambura kila anapoingia ofisini kwake asubuhi, hujiandaa kwa ajili ya kikao na Waandishi wa Habari kwa lengo la kuwapa matukio yote yalitokea kwa saa 24 zilizopita.
Ilikuwa ni saa 3:35 za asubuhi, ikiwa ni dakika 25 tu, kabla ya kikao chake na waandishi, simu ile ilikuwa na usumbufu mkubwa sana kwake. Akaamua kuipokea baada ya kujishauri kwa muda.
“Ofisini kwa OCID hapa, naomba nikusaidie!”
“Ni mimi Zena afande!” Sekretari wake Zena akazungumza kwenye chombo kwa sauti laini sana.
“Zena mara hii umesahau ratiba yangu ya asubuhi?”
“Sijasahau afande ila kuna simu muhimu sana kutoka Makao Makuu!”
“Wapi?”
“Central!”
“Niunganishe tafadhali!”
“Ok!” Zena akasema kisha akapotea hewani.
Sekunde kadhaa zikapita hewani muziki ukisikika kutoka upande wa pili, kisha sauti nzito ya kukwaruza ikasikika.
“Haloo!”
“Haloo!”
Sauti aliyoisikia kwenye simu, bila kujitambulisha, OCID Wambura alishaitambua kwamba alikuwa akizungumza na Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Ben Kitalilo.
“Jambo?” Kamanda Kitalilo akasema.
“Jambo afande!”
“Hao watuhumiwa wa madawa ya kulevya kutoka Saudi Arabia, wahamishie huku makao makuu asubuhi hii!”
“Nimekusoma afande!”
“Lazima nione ripoti nzima ya mwenendo wa hilo sakata kutokea Saudi Arabia hadi hapo ofisini kwako!”
“Umesomeka afande.”
Simu zikakatwa. Bila kupoteza muda OCID akaamua kumpa kazi ya kuzungumza na waandishi wa habari msaidizi wake, yeye akaagiza watuhumiwa wote watolewe selo kisha wakaingizwa kwenye gari na safari ya kwenda makao makuu ya polisi ikaanza, yeye akifuatia nyuma kwa gari lake.
***
Saa 3:45 asubuhi, Dk. Rwegoshora alikuwa akiingia ofisini kwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Ben Kitalilo baada ya kuruhusiwa na sekretari wake. Alipokelewa na tabasamu la kutengeneza na Kamanda Kitalilo.
“Karibu bwana!”
“Ahsante!”
“Najua unafahamu ni kwanini nipo hapa. Shida yangu ni kuona unafanya jambo fulani kwa gharama yoyote, mke wangu atoke kwenye hii kesi ya madawa ya kulevya ya Farida Mbaraka!”
“Farida Mbaraka?”
“Ndiyo, yule binti aliyekamatwa Saudi Arabia na Genesis kwenda kumuokoa huko!”
“Aisee sitaweza!”
“Kwanini? Tusaidiane tafadhali, sitaki mke wangu aozee ndani!”
“Lingekuwa limefika kwangu kama mtu wa mwisho, ningejua cha kufanya, lakini limetokea kwa IGP mwenyewe, amesisitiza nihakikishe nasimamia hili suala kikamilifu. Nakushauri ucheze na sheria, tafuta wanasheria wasimame mahakamani, lakini lazima wawe wazuri kweli kweli, maana ni kesi ngumu sana!” Akasema Kamanda Kitalilo.
Maneno ya Kamanda Kitalilo yalimkatisha tamaa kabisa Dk. Rwegoshora, kwa vyovyote vile, hakuwa na msaada wowote kwake. Hakusema chochote zaidi ya kusimama na kutoka nje ya ofisi.
Akiwa anatoka nje, kwenye ngazi akawaona mke wake, mke wa rafiki yake Profesa Mshana, Genesis, Farida na vijana watatu wakiwa chini ya ulinzi wa polisi wakipanda ngazi nyuma yao mitutu ya bunduki ikiwasindikiza!
Akawatazama wote kwa zamu, lakini macho yake yalipofika kwa mkewe, yaligota hapo! Mkewe akaanza kulia kwa uchungu! Macho ya Dk. Rwegoshora yakabadilika rangi na kuwa mekundu kabisa!
ILIKUWA ni sawa na sinema ya kusisimua iliyofikia sehemu ambayo mtazamaji asingeweza kubanduka kwenye kiti kuiacha ikiendelea. Hivyo ndivyo ilivyokuwa katika ulimwengu mwingine kichwani mwa Dk. Rwegoshora.
Kwa hakika alitamani sana kile alichokiona kiwe ndoto lakini haikuwa hivyo, kila kitu kilikuwa ni kweli na halisi. Mke wake aliendelea kulia huku askari wakiwasukuma kuwapandisha ngazi haraka kwenda kituoni.
Dk. Rwegoshora hakuwa na la kufanya zaidi ya kushuka ngazi huku akigeuza shingo yake akimshuhudia mkewe akipelekwa msobemsobe. Moyo ulimuuma sana lakini hakuwa na la kufanya. Kitu pekee kilichokuwa mbele yake ilikuwa ni kwenda haraka sana ofisini kwa IGP.
Akaingia kwenye gari lake kisha akawasha na kuingiza gia namba moja, akaliondoa kwa kasi sana kama gari lililoibiwa! Alikuwa anakwenda kwa IGP. Mke wake alikuwa na thamani kuliko kitu kingine chochote katika maisha yake.
***
“Genesis ndiye yupi hapa?” IGP aliuliza kwa sauti nzito iliyoonesha ukali.
“Ni mimi Mkuu,” Genesis akasema kwa kujiamini.
“Yaani kijana mzuri namna hii unaweza kufanya vitu vya ajabu kama hivi?”
“Mkuu kila kitu kina sababu, unaweza kushangazwa na kitu nilichokifanya, lakini nimekifanya kwa sababu.”
“Kwani umefanya nini?”
“Aaaah! Afande mara hii umesahau kwamba nimeua?” Akajibu Genesis akitabasamu.
Jibu lile liliwashtua wote mle ofisini, IGP na wenzake wakaangaliana.
“Hivi umeua?”
”Ndiyo nimeua afande!”
“Umemuua nani?”
“Mtoto wake na yule pale...” akasema Genesis akisonta kidole alipokuwa amekaa mama Bianca.
“Huyu?” Insp. Sebastian akamuuliza akimgusa bega mama Bianca.
“Ndiyo!”
“Bi. Rwegoshora ni yupi?”
“Ni mimi!”
“Bi Mshana?”
“Nipo!”
“Festo?”
“Afande!”
“Patrick!”
”Mkuu!”
”Dullah!”
“Afande!”
“...bila shaka Farida ni wewe!” Aliuliza IGP akimtulizia macho Farida.
“Ndiyo afande!”
Baada ya hapo kilichofuata ilikuwa ni kila mmoja kuandika maelezo katika karatasi maalum. Kitu cha kushangaza Genesis alikuwa akiropoka hovyo na kusisitiza kwamba ni kweli alimuua Bianca na alifanya hivyo baada ya kugundua njama aliyofanya kwa kushirikiana na watu waliokuwa wamekamatwa ili kumpa kesi Farida.
“Genesis hebu njoo huku,” alimwita Insp. Sebastian akiondoka huku Genesis akimfuata nyuma.
Safari yao iliishia kwenye chumba maalumu cha mahojiano.
“Genesis kumbuka kwamba ukweli wako ndiyo ambao utakutoa katika haya matatizo.”
“Nafahamu Mkuu!”
“Sasa hebu naomba uwe mkweli, unajua nini kuhusu kesi hii?”
“Maelezo yangu ni yale yale sidhani kama kuna sehemu nitabadilisha. Siogopi kusema ukweli huu na nipo tayari kufa kwa kuusimamia. Ukweli ni kwamba nimemuua Bianca siku ile ile ya ndoa kwa kumchoma na kisu kifuani mwake.
“Kikubwa kilichosababisha nimuue ni baada ya kugundua mchezo mchafu uliofanyika. Mama yangu hafai kabisa na hata huyu mama yake Bianca. Ni hatari maana wanalazimisha yafanyike wanayoyataka kwa kutoa uhai wa mtu.
“Sikuwa tayari kuona Farida anakufa, mwanamke ninayempenda kuliko wote duniani. Nikaamua kwenda Saudi Arabia kumuokoa, nashukuru nilifanikiwa kumuondoa katika mikono ya kifo. Najua pesa inaweza kutumika kumrudisha Farida kwenye matatizo lakini mimi ninao ushahidi wa kutosha na nipo tayari kuwaonesha.”
“Ushahidi gani huo?” Insp. Sebastian akamuuliza akionekana kumsikiliza kwa makini sana.
“Ipo anwani ya barua pepe ambayo ina kila kitu, inaonesha mchezo mzima ulivyofanyika.”
“Ni ya nani?”
“Marehemu Bianca!”
“Unadhani hawawezi kufuta hayo maelezo?”
“Sidhani maana Bianca mwenyewe ameshafariki na ni yeye ambaye angeweza kufuta.”
“Uko tayari kunionesha sasa hivi?”
“Nipo tayari.”
Muda ule ule wakaongozana hadi kwenye chumba cha mtandao wa Internet, kisha Genesis akataja anwani ya barua pepe ya Bianca kisha akaingiza maneno ya siri, akamuonesha mawasiliano na maelezo yote ya jinsi mchezo mzima ulivyofanyika.
“Mungu wangu!” Akashtuka Insp. Sebastian.
“Usishtuke huo ndiyo ukweli wenyewe, naomba kwanza u-save huo ukurasa kwenye kompyuta yako halafu pia uchape ili ushahidi usipotee.”
“Usinifundishe kazi kijana, hebu twende huku.”
Wakaongozana tena hadi walipokuwa watuhumiwa wengine ambapo wote kwa pamoja waliingizwa selo.
***
Katika chumba hiki kidogo chenye meza ya kioo walikuwa wamekaa wapelelezi watatu kwenye kikao cha dharura wakijadili namna ya kupambana na kesi ya akina Genesis. Wote walikuwa na mafaili mikononi mwao tayari kwa kuanza kikao.
“Nadhani kila mmoja ameona hali ilivyo, bila shaka tuna mahali pa kuanzia,” alisema Insp. Sebastian ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa kikao.
“Ndiyo Inspekta, lakini lazima nikiri kwamba sijawahi kukutana na kesi ngumu kama hii.”
“Lakini kwa kuwa ni kazi yetu tunapaswa kuikabili. Nahitaji mawazo yenu... ni akina nani tunaweza kuwaengua kwenye hii kesi?”
“Kwa ripoti ya Saudi Arabia, Farida hana cha kujibu,” alisema Insp. Mchele.
“Ni kweli kabisa, ushahidi wote mimi ninao, nadhani Farida atabaki kuwa shahidi lakini ni lazima tumtoe.”
Wakakubaliana kwa pamoja na hicho ndicho kilichotokea. Muda mfupi baada ya kikao kuisha Farida aliachiwa huru, lakini katika hali ya kushangaza alikataa kuondoka.
“Kwa nini hutaki kuondoka? Unataka kuozea jela?” Askari alimuuliza Farida.
“SIWEZI KUONDOKA BILA GENESIS WANGU, NIPO TAYARI KUFA NAYE KAMA YEYE ALIVYOKUWA TAYARI KUFA KWA AJILI YANGU, SIONDOKI!” Alisema Farida akionekana kumaanisha kilichotoka kinywani mwake.
***
IGP alikuwa makini sana kumsikiliza Dk. Rwegoshora. Kwa namna alivyokuwa akimsikiliza alionekana wazi kuwa na nia ya kumsaidia lakini cha ajabu Dk. Rwegoshora alipomaliza kuzungumza aliongea maneno ya kukatisha tamaa kabisa.
“Lipo nje ya uwezo wangu, hili suala lipo mezani kwa waziri mwenyewe.”
“Kwa waziri?”
“Ndiyo ni yeye ndiye aliyeagiza nisimamie.”
“Acha nikamuone!”
Dk. Rwegoshora akaondoka moja kwa moja hadi ofisini kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Silvanus Misiga. Katibu muhtasi wake alipomuona hakuwa na haja ya kumchelewesha, akamruhusu aende ofisini kwa waziri. Alimkuta waziri akiwa ametulia ofisini kwake. Bila kupoteza muda akamueleza kilichompeleka.
“Tafadhali sana najua hili lipo ndani ya uwezo wako naomba unisaidie. Nampenda mke wangu kuliko kitu chochote na sipendi heshima yangu iharibike!”
“Kwa masikitiko makubwa rafiki yangu napenda kukwambia kwamba hili suala lipo nje ya uwezo wangu, rais amesema nilisimamie kikamilifu.”
Dk. Rwegoshora alishtuka sana, ilikuwa ni vigumu sana kuonana na Rais hasa katika suala linalogusa maslahi ya taifa kama lile, alimuona kabisa mke wake akiwa amevaa nguo za jela akitumikia kifungo chake!
Je, nini kitaendelea?
Profesa Mshana akiwa amechanganyikiwa kabisa, akaamua kumpigia simu Dk. Rwegoshora ili wajaribu kucheza na sheria waweze kuwatoa wake zao pamoja na Genesis, lakini majibu aliyopewa na Dk. Rwegoshora yalimchanganya sana, alimwambia kila mmoja ahangaike na msalaba wake mwenyewe!
Hilo lilimchanganya Profesa Mshana lakini halikutosha, simu ilikatwa akiwa bado anajaribu kumshawishi! Kitendo cha kukatiwa simu, kikazidi kumtibua na kuzidisha giza nene katika wazo la kumtoa mwanaye pamoja na mkewe kwenye mkono wa sheria.
Je, nini kitatokea? Genesis na mama yake, mama Bianca, Dulla, Festo, Patrick na Farida watatoka? SONGA NAYO...
“AMENIKATIA simu?” Profesa Mshana akatamka kwa sauti kubwa.
“Haiwezekani!” Akajijibu tena mwenyewe.
Tukio lile lilimchanganya sana kichwa chake, likatoa taswira mpya kabisa katika safari yake ya kumtoa mwanaye pamoja na mkewe jela! Kitanzi kilionekana waziwazi mbele ya familia yake, jambo ambalo hakutaka kuliruhusu litokee.
“Lazima nifanye jambo fulani hapa,” akawaza tena.
Ni kweli ilikuwa lazima afikirie jambo fulani la kufanya kwa ajili ya mkewe na mwanaye. Yeye kama baba wa familia, alitakiwa kuumiza kichwa ili aweze kuiondoa familia yake katika hatari ambayo ilikuwa wazi kabisa.
Ubongo wake ukafanya kazi zaidi ya kawaida, hapo akawaza sana lakini mwisho wa kikomo cha mawazo yake ukagonga kwa Dk. Rwegoshora ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwamba yeye ndiye kila kitu.
Kama ni kweli alitaka kufanikiwa kuwatoa mtoto wake pamoja na mkewe ndani, lazima muunganiko wao ufanye kazi sawasawa, vinginevyo ingekuwa ndoto kwake kufanikiwa!
“Lazima nizungumze naye...” akawaza.
Wazo lake lilikuwa na nguvu sana, kitu pekee alichoona kinafaa kufanyika ilikuwa ni kumpigia simu. Mara moja akanyanyua simu yake haraka na kubonyeza tena namba za Dk. Rwegoshora. Simu iliita kwa muda mfupi sana, ikapokelewa.
“Sema nakusikiliza!” Alikuwa ni Dk. Rwegoshora akizungumza kwa sauti iliyosoma majonzi na kisasi.
“Ndugu yangu tuliza hasira!”
“Hasira?”
“Ndiyo naona una hasira sana!”
“Unahisi sikutakiwa kuwa nazo siyo?”
“Sijasema hivyo Rwegoshora ndugu yangu. Unajua kama ni maji kumwagika yameshamwagika, sasa tuangalie namna ya kuwatoa hawa watu kwenye matatizo.”
“Tunawatoa akina nani?”
“Tuliza moyo ndugu yangu, naamini unajua nazungumzia akina nani, lakini hasira ndiyo inakufanya unijibu hivyo!”
“Sikiliza Mshana, sina muda wa kuendelea kupoteza kwenye simu, nina mambo mengi sana muhimu ya kufanya. Kikubwa ambacho unatakiwa kufahamu, juu ya suala hili, kila mmoja ahangaike kivyake!”
“Sisi ni ndugu lakini?”
“Undugu wetu ndiyo usababishe mwanangu afe?”
“Hapana!””Mke wangu awekwe ndani?”
“Hayo yameshatokea, tunatakiwa kuangalia mbele kwa sasa.”
“Sina mbele nyingine na wewe, naona hata huo urafiki wetu wa kinafiki uishie hapa, kila mtu ahangaike kivyake!” Akasema Dk. Rwegoshora kwa kumaanisha.
“Lakini sikikiliza rafiki yangu, unajua...” akasema Profesa Mshana hata hivyo hakusikia dalili yoyote ya Dk. Rwegoshora kuwa hewani.
“Halooo...halooo...” alikuwa akiita, lakini baadaye akagundua kwamba Dk. Rwegoshora alikuwa amemkatia simu.
Hili ni tukio la pili la aina hiyo kufanywa na Dk. Rwegoshora, rafiki yake mkubwa ambaye walishibana. Hakuhitaji mtu yeyote wa kujitokeza kumwambia kwamba harufu ya urafiki wao kufikia tamati ilikuwa inanukia. Kila kitu kilikuwa wazi kabisa, kwamba hasira ya Dk. Rwegoshora zilikuwa kali na hakuona taabu yoyote kuvunja urafiki wao.
“Si neno, nitajua cha kufanya...ni mwanaume, mwenye elimu, siyo lazima kila kitu kitafanikiwa kupitia kwake. Nitatumia uzoefu wangu kuhakikisha hili tatizo linaisha. Najua nitaweza!” Akajipa moyo Profesa Mshana.
***
Simu ya mezani kwake iliita kwa muda mrefu sana, bila kuipokea. Kwa kawaida, OCID Wambura kila anapoingia ofisini kwake asubuhi, hujiandaa kwa ajili ya kikao na Waandishi wa Habari kwa lengo la kuwapa matukio yote yalitokea kwa saa 24 zilizopita.
Ilikuwa ni saa 3:35 za asubuhi, ikiwa ni dakika 25 tu, kabla ya kikao chake na waandishi, simu ile ilikuwa na usumbufu mkubwa sana kwake. Akaamua kuipokea baada ya kujishauri kwa muda.
“Ofisini kwa OCID hapa, naomba nikusaidie!”
“Ni mimi Zena afande!” Sekretari wake Zena akazungumza kwenye chombo kwa sauti laini sana.
“Zena mara hii umesahau ratiba yangu ya asubuhi?”
“Sijasahau afande ila kuna simu muhimu sana kutoka Makao Makuu!”
“Wapi?”
“Central!”
“Niunganishe tafadhali!”
“Ok!” Zena akasema kisha akapotea hewani.
Sekunde kadhaa zikapita hewani muziki ukisikika kutoka upande wa pili, kisha sauti nzito ya kukwaruza ikasikika.
“Haloo!”
“Haloo!”
Sauti aliyoisikia kwenye simu, bila kujitambulisha, OCID Wambura alishaitambua kwamba alikuwa akizungumza na Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Ben Kitalilo.
“Jambo?” Kamanda Kitalilo akasema.
“Jambo afande!”
“Hao watuhumiwa wa madawa ya kulevya kutoka Saudi Arabia, wahamishie huku makao makuu asubuhi hii!”
“Nimekusoma afande!”
“Lazima nione ripoti nzima ya mwenendo wa hilo sakata kutokea Saudi Arabia hadi hapo ofisini kwako!”
“Umesomeka afande.”
Simu zikakatwa. Bila kupoteza muda OCID akaamua kumpa kazi ya kuzungumza na waandishi wa habari msaidizi wake, yeye akaagiza watuhumiwa wote watolewe selo kisha wakaingizwa kwenye gari na safari ya kwenda makao makuu ya polisi ikaanza, yeye akifuatia nyuma kwa gari lake.
***
Saa 3:45 asubuhi, Dk. Rwegoshora alikuwa akiingia ofisini kwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Ben Kitalilo baada ya kuruhusiwa na sekretari wake. Alipokelewa na tabasamu la kutengeneza na Kamanda Kitalilo.
“Karibu bwana!”
“Ahsante!”
“Najua unafahamu ni kwanini nipo hapa. Shida yangu ni kuona unafanya jambo fulani kwa gharama yoyote, mke wangu atoke kwenye hii kesi ya madawa ya kulevya ya Farida Mbaraka!”
“Farida Mbaraka?”
“Ndiyo, yule binti aliyekamatwa Saudi Arabia na Genesis kwenda kumuokoa huko!”
“Aisee sitaweza!”
“Kwanini? Tusaidiane tafadhali, sitaki mke wangu aozee ndani!”
“Lingekuwa limefika kwangu kama mtu wa mwisho, ningejua cha kufanya, lakini limetokea kwa IGP mwenyewe, amesisitiza nihakikishe nasimamia hili suala kikamilifu. Nakushauri ucheze na sheria, tafuta wanasheria wasimame mahakamani, lakini lazima wawe wazuri kweli kweli, maana ni kesi ngumu sana!” Akasema Kamanda Kitalilo.
Maneno ya Kamanda Kitalilo yalimkatisha tamaa kabisa Dk. Rwegoshora, kwa vyovyote vile, hakuwa na msaada wowote kwake. Hakusema chochote zaidi ya kusimama na kutoka nje ya ofisi.
Akiwa anatoka nje, kwenye ngazi akawaona mke wake, mke wa rafiki yake Profesa Mshana, Genesis, Farida na vijana watatu wakiwa chini ya ulinzi wa polisi wakipanda ngazi nyuma yao mitutu ya bunduki ikiwasindikiza!
Akawatazama wote kwa zamu, lakini macho yake yalipofika kwa mkewe, yaligota hapo! Mkewe akaanza kulia kwa uchungu! Macho ya Dk. Rwegoshora yakabadilika rangi na kuwa mekundu kabisa!
ILIKUWA ni sawa na sinema ya kusisimua iliyofikia sehemu ambayo mtazamaji asingeweza kubanduka kwenye kiti kuiacha ikiendelea. Hivyo ndivyo ilivyokuwa katika ulimwengu mwingine kichwani mwa Dk. Rwegoshora.
Kwa hakika alitamani sana kile alichokiona kiwe ndoto lakini haikuwa hivyo, kila kitu kilikuwa ni kweli na halisi. Mke wake aliendelea kulia huku askari wakiwasukuma kuwapandisha ngazi haraka kwenda kituoni.
Dk. Rwegoshora hakuwa na la kufanya zaidi ya kushuka ngazi huku akigeuza shingo yake akimshuhudia mkewe akipelekwa msobemsobe. Moyo ulimuuma sana lakini hakuwa na la kufanya. Kitu pekee kilichokuwa mbele yake ilikuwa ni kwenda haraka sana ofisini kwa IGP.
Akaingia kwenye gari lake kisha akawasha na kuingiza gia namba moja, akaliondoa kwa kasi sana kama gari lililoibiwa! Alikuwa anakwenda kwa IGP. Mke wake alikuwa na thamani kuliko kitu kingine chochote katika maisha yake.
***
“Genesis ndiye yupi hapa?” IGP aliuliza kwa sauti nzito iliyoonesha ukali.
“Ni mimi Mkuu,” Genesis akasema kwa kujiamini.
“Yaani kijana mzuri namna hii unaweza kufanya vitu vya ajabu kama hivi?”
“Mkuu kila kitu kina sababu, unaweza kushangazwa na kitu nilichokifanya, lakini nimekifanya kwa sababu.”
“Kwani umefanya nini?”
“Aaaah! Afande mara hii umesahau kwamba nimeua?” Akajibu Genesis akitabasamu.
Jibu lile liliwashtua wote mle ofisini, IGP na wenzake wakaangaliana.
“Hivi umeua?”
”Ndiyo nimeua afande!”
“Umemuua nani?”
“Mtoto wake na yule pale...” akasema Genesis akisonta kidole alipokuwa amekaa mama Bianca.
“Huyu?” Insp. Sebastian akamuuliza akimgusa bega mama Bianca.
“Ndiyo!”
“Bi. Rwegoshora ni yupi?”
“Ni mimi!”
“Bi Mshana?”
“Nipo!”
“Festo?”
“Afande!”
“Patrick!”
”Mkuu!”
”Dullah!”
“Afande!”
“...bila shaka Farida ni wewe!” Aliuliza IGP akimtulizia macho Farida.
“Ndiyo afande!”
Baada ya hapo kilichofuata ilikuwa ni kila mmoja kuandika maelezo katika karatasi maalum. Kitu cha kushangaza Genesis alikuwa akiropoka hovyo na kusisitiza kwamba ni kweli alimuua Bianca na alifanya hivyo baada ya kugundua njama aliyofanya kwa kushirikiana na watu waliokuwa wamekamatwa ili kumpa kesi Farida.
“Genesis hebu njoo huku,” alimwita Insp. Sebastian akiondoka huku Genesis akimfuata nyuma.
Safari yao iliishia kwenye chumba maalumu cha mahojiano.
“Genesis kumbuka kwamba ukweli wako ndiyo ambao utakutoa katika haya matatizo.”
“Nafahamu Mkuu!”
“Sasa hebu naomba uwe mkweli, unajua nini kuhusu kesi hii?”
“Maelezo yangu ni yale yale sidhani kama kuna sehemu nitabadilisha. Siogopi kusema ukweli huu na nipo tayari kufa kwa kuusimamia. Ukweli ni kwamba nimemuua Bianca siku ile ile ya ndoa kwa kumchoma na kisu kifuani mwake.
“Kikubwa kilichosababisha nimuue ni baada ya kugundua mchezo mchafu uliofanyika. Mama yangu hafai kabisa na hata huyu mama yake Bianca. Ni hatari maana wanalazimisha yafanyike wanayoyataka kwa kutoa uhai wa mtu.
“Sikuwa tayari kuona Farida anakufa, mwanamke ninayempenda kuliko wote duniani. Nikaamua kwenda Saudi Arabia kumuokoa, nashukuru nilifanikiwa kumuondoa katika mikono ya kifo. Najua pesa inaweza kutumika kumrudisha Farida kwenye matatizo lakini mimi ninao ushahidi wa kutosha na nipo tayari kuwaonesha.”
“Ushahidi gani huo?” Insp. Sebastian akamuuliza akionekana kumsikiliza kwa makini sana.
“Ipo anwani ya barua pepe ambayo ina kila kitu, inaonesha mchezo mzima ulivyofanyika.”
“Ni ya nani?”
“Marehemu Bianca!”
“Unadhani hawawezi kufuta hayo maelezo?”
“Sidhani maana Bianca mwenyewe ameshafariki na ni yeye ambaye angeweza kufuta.”
“Uko tayari kunionesha sasa hivi?”
“Nipo tayari.”
Muda ule ule wakaongozana hadi kwenye chumba cha mtandao wa Internet, kisha Genesis akataja anwani ya barua pepe ya Bianca kisha akaingiza maneno ya siri, akamuonesha mawasiliano na maelezo yote ya jinsi mchezo mzima ulivyofanyika.
“Mungu wangu!” Akashtuka Insp. Sebastian.
“Usishtuke huo ndiyo ukweli wenyewe, naomba kwanza u-save huo ukurasa kwenye kompyuta yako halafu pia uchape ili ushahidi usipotee.”
“Usinifundishe kazi kijana, hebu twende huku.”
Wakaongozana tena hadi walipokuwa watuhumiwa wengine ambapo wote kwa pamoja waliingizwa selo.
***
Katika chumba hiki kidogo chenye meza ya kioo walikuwa wamekaa wapelelezi watatu kwenye kikao cha dharura wakijadili namna ya kupambana na kesi ya akina Genesis. Wote walikuwa na mafaili mikononi mwao tayari kwa kuanza kikao.
“Nadhani kila mmoja ameona hali ilivyo, bila shaka tuna mahali pa kuanzia,” alisema Insp. Sebastian ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa kikao.
“Ndiyo Inspekta, lakini lazima nikiri kwamba sijawahi kukutana na kesi ngumu kama hii.”
“Lakini kwa kuwa ni kazi yetu tunapaswa kuikabili. Nahitaji mawazo yenu... ni akina nani tunaweza kuwaengua kwenye hii kesi?”
“Kwa ripoti ya Saudi Arabia, Farida hana cha kujibu,” alisema Insp. Mchele.
“Ni kweli kabisa, ushahidi wote mimi ninao, nadhani Farida atabaki kuwa shahidi lakini ni lazima tumtoe.”
Wakakubaliana kwa pamoja na hicho ndicho kilichotokea. Muda mfupi baada ya kikao kuisha Farida aliachiwa huru, lakini katika hali ya kushangaza alikataa kuondoka.
“Kwa nini hutaki kuondoka? Unataka kuozea jela?” Askari alimuuliza Farida.
“SIWEZI KUONDOKA BILA GENESIS WANGU, NIPO TAYARI KUFA NAYE KAMA YEYE ALIVYOKUWA TAYARI KUFA KWA AJILI YANGU, SIONDOKI!” Alisema Farida akionekana kumaanisha kilichotoka kinywani mwake.
***
IGP alikuwa makini sana kumsikiliza Dk. Rwegoshora. Kwa namna alivyokuwa akimsikiliza alionekana wazi kuwa na nia ya kumsaidia lakini cha ajabu Dk. Rwegoshora alipomaliza kuzungumza aliongea maneno ya kukatisha tamaa kabisa.
“Lipo nje ya uwezo wangu, hili suala lipo mezani kwa waziri mwenyewe.”
“Kwa waziri?”
“Ndiyo ni yeye ndiye aliyeagiza nisimamie.”
“Acha nikamuone!”
Dk. Rwegoshora akaondoka moja kwa moja hadi ofisini kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Silvanus Misiga. Katibu muhtasi wake alipomuona hakuwa na haja ya kumchelewesha, akamruhusu aende ofisini kwa waziri. Alimkuta waziri akiwa ametulia ofisini kwake. Bila kupoteza muda akamueleza kilichompeleka.
“Tafadhali sana najua hili lipo ndani ya uwezo wako naomba unisaidie. Nampenda mke wangu kuliko kitu chochote na sipendi heshima yangu iharibike!”
“Kwa masikitiko makubwa rafiki yangu napenda kukwambia kwamba hili suala lipo nje ya uwezo wangu, rais amesema nilisimamie kikamilifu.”
Dk. Rwegoshora alishtuka sana, ilikuwa ni vigumu sana kuonana na Rais hasa katika suala linalogusa maslahi ya taifa kama lile, alimuona kabisa mke wake akiwa amevaa nguo za jela akitumikia kifungo chake!
Je, nini kitaendelea?