Kifo cha Filikunjombe, Lowassa alia

Kifo cha Filikunjombe, Lowassa alia

Shobi

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2015
Posts
3,401
Reaction score
4,371
Ni taarifa ya kushtusha sana ya msiba wa mwanasiasa chipukizi na jasiri, Deo Filikonjombe kutokana na ajali ya Helikopta jana jioni maeneo ya mbuga ya Selous mkoani Morogoro. Ni pigo lingine kubwa ambalo katika kipindi kifupi Taifa limepata, huku bado likiwa na kidonda cha kuondokewa na wana siasa wengine mahiri, Marehemu Celina Kombani, Dr Abdallah Kigoda na Dr Emanuel Makaidi aliyefariki jana.

Filikonjombe alikuwa Mbunge mahiri aliyesimama imara kutetea maslahi ya wananchi wa jimbo lake la Ludewa na watanzania kwa ujumla. Alikuwa mwiba kwa serikali ya Chama chake CCM kutetea maslahi ya nchi, mfano ni katika kashfa ya Escrow ambapo alikuwa Makamu Mwenyekiti wa kamati iliyochunguza kashfa hiyo.

Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira, familia, jamaa, marafiki na wananchi wa Ludewa, katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao

.BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE.


Edward N. Lowassa

 
1445016555793.jpg
 
filikunjombe kifo chake kimeniuma kulko alipokufa baba mzazi. ndo mwanasiasa pekee aliyekuwa ccm kimakosa.

pengie huyo aliyekufa alikuwa sio baba yako mzazi rwazi mulize mama yako akuambie baba yako hali
 
Last edited by a moderator:
Lowassa hawezi kumlilia Filikunjombe

mpinga shetani;
Tatizo mlilo nalo nyiye maccm ni kuwa kila kitu kwenu ni siasa za maji taka tuu. Kwa nini unaona kuwa Lowasa hawezi kumlilia Filikunjombe?? Si mtu? Hata mchawi mbona humlilia aliyemtwaa, iweje Lowasa asimlilie mtu ambaye wamekaa pamoja mjengoni, wamebadilishana maneno mawili matatu iwe kwa furaha au kwa uchungu lakini waliwahi kukaa pamoja na haswa ikikumbukwa kuwa hawa walikuwa wabunge wa chama kimoja kwa miaka mingi. Acha upuuzi kutania kila mahali. Weye kama hukuhuzunishwa na kifo cha Deo acha waliohuzunishwa waseme.:dizzy::dizzy:
 
Back
Top Bottom