tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 27,181
- 27,781
Hekaya za 'Kifo' cha aliyekuwa gavana wa BoT aliyeikimbia nchi kwa sababu ya kushiriki ufisadi wa EPA, bado zinaendelea kuvuma masikioni mwa watanzania. Na inaonekana watunzi wa HEKAYA hizi wamejipanga vizuri hadi kufikia hatua ya kugharamia utunzi mzima wa hekaya.
Hitimisho la hekaya hizi limeanza kutungwa na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini, ambapo mmoja wa watunzi hao amegharamiwa safari ya kwenda Marekani kupiga picha ya kaburi feki lililoandaliwa na kisha kuandikwa jina la DAUDI BALLALI na picha hizo zimekusudiwa kutumika kunogesha hadithi kwenye gazeti analoliandikia.
Ndugu zangu, watanzania wa leo sio wajinga kama watu wengi wanavyodhani. Uongo unaotungwa kwamba eti Balali hakutaka mwili wake uonekane kwa watu, ni hekaya ambazo kila mtanzania mwenye akili timamu hawezi kuzikubali. Hata mtoto wangu wa miaka 3 anayesoma chekechea atakataa uongo huo. Tukio zima la 'kifo' cha balali ni hadithi ya kusadikika. Kovu la EPA alilosababisha Balali haliwezi kufutika mioyoni mwa watanzania.
:yield:
Hitimisho la hekaya hizi limeanza kutungwa na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini, ambapo mmoja wa watunzi hao amegharamiwa safari ya kwenda Marekani kupiga picha ya kaburi feki lililoandaliwa na kisha kuandikwa jina la DAUDI BALLALI na picha hizo zimekusudiwa kutumika kunogesha hadithi kwenye gazeti analoliandikia.
Ndugu zangu, watanzania wa leo sio wajinga kama watu wengi wanavyodhani. Uongo unaotungwa kwamba eti Balali hakutaka mwili wake uonekane kwa watu, ni hekaya ambazo kila mtanzania mwenye akili timamu hawezi kuzikubali. Hata mtoto wangu wa miaka 3 anayesoma chekechea atakataa uongo huo. Tukio zima la 'kifo' cha balali ni hadithi ya kusadikika. Kovu la EPA alilosababisha Balali haliwezi kufutika mioyoni mwa watanzania.
:yield: