Kifo cha aibu

Kifo cha aibu

DIDAS TUMAINI

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2014
Posts
242
Reaction score
680
Serikali DHALIMU ya mwendazake ilimshtaki ndugu yangu mmoja kwa kesi ya uhujumu uchumi. Akakamatwa, biashara zake zikafungwa, na fedha zilizokua kwenye akaunti zake zikachukuliwa. Akakaa rumande zaidi ya mwaka mmoja bila dhamana.

Akaacha mtoto wa miezi mitatu nyumbani. Mtoto akadhulumiwa haki yake ya malezi ya baba. Yeye anadai hakufanya jinai isipokua aliadhibiwa kwa sababu za kisiasa. Askari upelelezi wa kesi yake siku moja alimuapia kuwa UTAFIA JELA.

Tulipoenda kumtembelea magereza akatuambia kwamba ameambiwa na mpelelezi wa kesi yake kwamba atafia jela. Tukatafuta namba ya simu ya huyo mpelelezi kumuuliza kama ni kweli alitamka maneno hayo. Akaishia kutukana matusi mazito.

Mtoto akaendelea kukua hadi kufikisha mwaka mmoja bila kumfahamu baba yake mzazi. Mama yake akaenda kanisani akalia kwa uchungu na kumkabidhi Mungu kesi hiyo. Wafanyabiashara wenzake wakamtaka akiri ili afanye "plea burgaining" alipe na aachiwe lakini akasema hawezi kukiri kosa ambalo hajalifanya. Akasota jela zaidi ya mwaka mmoja.

Mapema mwaka huu yule mpelelezi akakutwa amefia nyumba ya kulala wageni, akiwa uchi na madawa ya kuongeza nguvu za kiume pembeni. Inadaiwa alikua na mwanamke lakini mwaanamke huyo hakufahamika. Habari yake "ikafichwafichwa" ili kuepusha aibu kwa Jamhuri.

Miezi michache baadae (Mama akiwa tayari madarakani) ndugu huyo akafutiwa kesi yake na kuachiwa huru bila masharti yoyote. Akaunti zake zikafunguliwa na baadhi ya fedha zikarudishwa (si zote). Akaanza maisha upya. Jumapili moja tukafanya ibada ya shukrani kwa ajili ya wema ambao Mungu amemtendea, baadae tukawa na tafrija kidogo nyumbani kwake Mbweni.

Kwenye ile tafrija akasema "nimesahau kumualika rafiki yangu mmoja, askari upelelezi aliyeniapia kuwa nitafia gerezani. Ningefurahi angekua hapa kushuhudia ukuu wa Mungu kwamba sijafia gerezani" Lakini tukamwambia alishakufa. Alifia nyumba ya kulala wageni. Kifo cha aibu.

Malisa GJ


IMG-20211028-WA0002.jpg
 
Kwahiyo alikufa kwa ajili ya dua yenu? Na mm Kuna mtu kanidhulumu nifundishe maombi ya kumuuwa kama ni kweli
 
Kwahiyo alikufa kwa ajili ya dua yenu? Na mm Kuna mtu kanidhulumu nifundishe maombi ya kumuuwa kama ni kweli
Hatuwezi kukufundisha kwasababu hata wewe lazima umedhulumu tu wengine. Subiri tu ufe kwa aibu kwa kuzungushwa zungushwa na machela kama Jiwe.
 
Lilikufa kwa aibu na sasa linachezea vitasa vya hatarii huko kuzimu!
Alikufa ila si kwa aibu! Unajua kifo cha aibu wewe? Tuanzie hapo, suala la kuchezea vitasa lipo na halikwepeki kama alifanya maovu. Suala ni kuwa hakufa kwa aibu.

Rejea kifo cha Sani Abacha wa Nigeria halafu uje!!
 
Lilidhani litaishi milele matokeo yake Lilikufa kwa aibu likizungushwa zungushwa na machela likiwa unconscious. I hate him
Yaani bado anakutesa japo kafa?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] jamaa alimtumbua mzee wako au ndugu yako? Au wewe ni mhitimu wa chuo kikuu usiye na ajira? Kutembezwa kwenye machela si aibu ni heshima na hadhi ya kiongozi mkuu wa nchi.

Sani Abacha ndiye alikufa kwa aibu! Ila in short jamaa alikuwa anaboa upande fulani, mimi mzee wangu mpaka leo hajapata mafao yake, Jiwe aliyaminya! So sad!
 
Serikali DHALIMU ya mwendazake ilimshtaki ndugu yangu mmoja kwa kesi ya uhujumu uchumi. Akakamatwa, biashara zake zikafungwa, na fedha zilizokua kwenye akaunti zake zikachukuliwa. Akakaa rumande zaidi ya mwaka mmoja bila dhamana.

Akaacha mtoto wa miezi mitatu nyumbani. Mtoto akadhulumiwa haki yake ya malezi ya baba. Yeye anadai hakufanya jinai isipokua aliadhibiwa kwa sababu za kisiasa. Askari upelelezi wa kesi yake siku moja alimuapia kuwa UTAFIA JELA.

Tulipoenda kumtembelea magereza akatuambia kwamba ameambiwa na mpelelezi wa kesi yake kwamba atafia jela. Tukatafuta namba ya simu ya huyo mpelelezi kumuuliza kama ni kweli alitamka maneno hayo. Akaishia kutukana matusi mazito.

Mtoto akaendelea kukua hadi kufikisha mwaka mmoja bila kumfahamu baba yake mzazi. Mama yake akaenda kanisani akalia kwa uchungu na kumkabidhi Mungu kesi hiyo. Wafanyabiashara wenzake wakamtaka akiri ili afanye "plea burgaining" alipe na aachiwe lakini akasema hawezi kukiri kosa ambalo hajalifanya. Akasota jela zaidi ya mwaka mmoja.

Mapema mwaka huu yule mpelelezi akakutwa amefia nyumba ya kulala wageni, akiwa uchi na madawa ya kuongeza nguvu za kiume pembeni. Inadaiwa alikua na mwanamke lakini mwaanamke huyo hakufahamika. Habari yake "ikafichwafichwa" ili kuepusha aibu kwa Jamhuri.

Miezi michache baadae (Mama akiwa tayari madarakani) ndugu huyo akafutiwa kesi yake na kuachiwa huru bila masharti yoyote. Akaunti zake zikafunguliwa na baadhi ya fedha zikarudishwa (si zote). Akaanza maisha upya. Jumapili moja tukafanya ibada ya shukrani kwa ajili ya wema ambao Mungu amemtendea, baadae tukawa na tafrija kidogo nyumbani kwake Mbweni.

Kwenye ile tafrija akasema "nimesahau kumualika rafiki yangu mmoja, askari upelelezi aliyeniapia kuwa nitafia gerezani. Ningefurahi angekua hapa kushuhudia ukuu wa Mungu kwamba sijafia gerezani" Lakini tukamwambia alishakufa. Alifia nyumba ya kulala wageni. Kifo cha aibu.

Malisa GJView attachment 1991865
unafurahia kifo cha askari au
 
Yaani bado anakutesa japo kafa?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] jamaa alimtumbua mzee wako au ndugu yako? Au wewe ni mhitimu wa chuo kikuu usiye na ajira? Kutembezwa kwenye machela si aibu ni heshima na hadhi ya kiongozi mkuu wa nchi.

Sani Abacha ndiye alikufa kwa aibu! Ila in short jamaa alikuwa anaboa upande fulani, mimi mzee wangu mpaka leo hajapata mafao yake, Jiwe aliyaminya! So sad!
Tanzania is safe now after his death
 
Back
Top Bottom