Pdidy
Platinum Member
- Nov 22, 2007
- 61,775
- 37,968
Mwalimu awapa mimba wanafunzi wakeAdvertisement

Wednesday, May 27, 2009 12:00 PM
MWALIMU wa Shule ya Msingi ya Qwam iliyopo Kata ya Kiru Wilayani Babati Mkoani Manyara ametuhumiwa kuwabaka na kuwapa mimba wanafunzi wake wawili wanaosoma darasa la saba katika shule hiyo.Imedaiwa kuwa wanafunzi hao waliopewa mimba na mwalimu huyo, mmoja ana umri wa miaka 15 na mwingine ana miaka 17 wote wakisoma darasa la saba na hali iliyowafanya wanafunzi hao kukatisha masomo kutokana na mimba hizo.
Kaimu Kamanda Mkoani Manyara, Daudi Siasi amethibitisha kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Mei 21, mwaka huu huko Arusha alikokuwa amekimbilia.
Alisema kuwa mwalimu huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi hao kwa kipindi kirefu na alikuwa akiwarubuni kwa kuwapa kazi za kufanya nyumbani kwake.
Alisema kuwa mwalimu huyo alikuwa anatumia mbinu ya kuwapa kazi nyumbani kwake na wanapofika huko ndipo alikuwa anatumia mwanya huo kutimiza adhma yake hiyo.
Alisema wanafunzi hao waligundudulika baada yakuwa mahudhurio yao shuleni yalikuwa hayaridhishi ndipo uongozi wa shule ulipowaita kwa nyakati tofauti wanafunzi kwa ajili ya kuwahoji.
Ndipo kila mmoja aligundulika kuwa ana mimba na alipoulizwa alimtaja mwalimu huyo kuwa alimpa mimba hiyo.
Alisema baada ya kuzagaa kwa taarifa hiyo mwalimu alitoroka tokea Mei 4 mwaka huu na kukimbilia kwao mjini Arusha na alikamatwa Mei 21 kwa kutumia mgambo wa kijiji.
Katika mahojiano makali na wanafunzi hao ilisemekana kuwa mwalimu huyo aliweza kumbaka mwanafunzi wa miaka 17 kati ya Septemba 17, mwaka jana na kumrudia tena Januari mwaka huu, hivyo mpaka sasa mwanafunzi huyo ana mimba yenye umri wa miezi minane.
Na aliweza kumbaka mwanafunzi mwenye umri wa miaka 15 kati ya Novemba 15, mwaka jana na kumrudia tena Machi 23, mwaka huu na hadi sasa mwanafunzi huyo ana mimba yenye umri wa miezi mitano.
Kamanda huyo alisema mwalimu huyo ataweza kufikishwa Mahakamani kujibu mashtaka hayo leo.

Wednesday, May 27, 2009 12:00 PM
MWALIMU wa Shule ya Msingi ya Qwam iliyopo Kata ya Kiru Wilayani Babati Mkoani Manyara ametuhumiwa kuwabaka na kuwapa mimba wanafunzi wake wawili wanaosoma darasa la saba katika shule hiyo.Imedaiwa kuwa wanafunzi hao waliopewa mimba na mwalimu huyo, mmoja ana umri wa miaka 15 na mwingine ana miaka 17 wote wakisoma darasa la saba na hali iliyowafanya wanafunzi hao kukatisha masomo kutokana na mimba hizo.
Kaimu Kamanda Mkoani Manyara, Daudi Siasi amethibitisha kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Mei 21, mwaka huu huko Arusha alikokuwa amekimbilia.
Alisema kuwa mwalimu huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi hao kwa kipindi kirefu na alikuwa akiwarubuni kwa kuwapa kazi za kufanya nyumbani kwake.
Alisema kuwa mwalimu huyo alikuwa anatumia mbinu ya kuwapa kazi nyumbani kwake na wanapofika huko ndipo alikuwa anatumia mwanya huo kutimiza adhma yake hiyo.
Alisema wanafunzi hao waligundudulika baada yakuwa mahudhurio yao shuleni yalikuwa hayaridhishi ndipo uongozi wa shule ulipowaita kwa nyakati tofauti wanafunzi kwa ajili ya kuwahoji.
Ndipo kila mmoja aligundulika kuwa ana mimba na alipoulizwa alimtaja mwalimu huyo kuwa alimpa mimba hiyo.
Alisema baada ya kuzagaa kwa taarifa hiyo mwalimu alitoroka tokea Mei 4 mwaka huu na kukimbilia kwao mjini Arusha na alikamatwa Mei 21 kwa kutumia mgambo wa kijiji.
Katika mahojiano makali na wanafunzi hao ilisemekana kuwa mwalimu huyo aliweza kumbaka mwanafunzi wa miaka 17 kati ya Septemba 17, mwaka jana na kumrudia tena Januari mwaka huu, hivyo mpaka sasa mwanafunzi huyo ana mimba yenye umri wa miezi minane.
Na aliweza kumbaka mwanafunzi mwenye umri wa miaka 15 kati ya Novemba 15, mwaka jana na kumrudia tena Machi 23, mwaka huu na hadi sasa mwanafunzi huyo ana mimba yenye umri wa miezi mitano.
Kamanda huyo alisema mwalimu huyo ataweza kufikishwa Mahakamani kujibu mashtaka hayo leo.