Nowaka
Member
- Apr 5, 2019
- 20
- 13
Nasikitika sana jiji la Mbeya kubeba taswila ya kutoheshimu, viongozi wakuu wa kitaifa na mamlaka zao. Matokeo yake jiji limekuwa linachelea kupata maendeleo ya haraka, kwa sababu ya kukosa ushirikiano dhabiti kutoka mamlaka za kiserikali.
Ipo wazi kuwa, wana Mbeya wafike mahari, watambue ipo haja ya kukubali kushirikiana na viongozi wakuu pamoja na mamlaka zao, katika kujenga jiji la Mbeya. Hii biashara wanayofanya ya kujionesha ni watovu wa nidhamu kwa serikali haitowafikisha popote, zaidi zaidi itakuwa ni hasara kwa kuendelea kukosa miradi ya maendeleo na kusahaulika.
Rai yangu: bado nafasi ipo ya kushirikiana na serikali, ifike mahari tutambue kwa busara yupi ni mtu sahihi ambaye anaweza kutuvusha katika daraja kuelekea katika maendeleo ya kweli, ifike mahari tutambue tunapaswa kujenga mahusiano mema na viongozi katika mamlaka zao za serikali kwa ajili ya maendeleo yetu, tukosoe kwa staha na adabu pale ambapo tunaona mambo hayaendi sawa, kuanzia sasa tujenge taswila mpya hakika jiji la Mbeya litatoboa, kwani lina sifa zote za kutoboa ila wanasiasa wanalichelewesha jiji kutoboa.
Ipo wazi kuwa, wana Mbeya wafike mahari, watambue ipo haja ya kukubali kushirikiana na viongozi wakuu pamoja na mamlaka zao, katika kujenga jiji la Mbeya. Hii biashara wanayofanya ya kujionesha ni watovu wa nidhamu kwa serikali haitowafikisha popote, zaidi zaidi itakuwa ni hasara kwa kuendelea kukosa miradi ya maendeleo na kusahaulika.
Rai yangu: bado nafasi ipo ya kushirikiana na serikali, ifike mahari tutambue kwa busara yupi ni mtu sahihi ambaye anaweza kutuvusha katika daraja kuelekea katika maendeleo ya kweli, ifike mahari tutambue tunapaswa kujenga mahusiano mema na viongozi katika mamlaka zao za serikali kwa ajili ya maendeleo yetu, tukosoe kwa staha na adabu pale ambapo tunaona mambo hayaendi sawa, kuanzia sasa tujenge taswila mpya hakika jiji la Mbeya litatoboa, kwani lina sifa zote za kutoboa ila wanasiasa wanalichelewesha jiji kutoboa.