Kiukweli tunatofautiana sana uelewa, sio lazima kila aliyeajiri Tanzania Daima awe ni mwanachama, mfuasi au mshabiki wa mmiliki!. Vivyo hivyo kwa Mtanzania, haina maana kila mtu pale ni mwanachama, mfuasi au mshabiki wa mmiliki!.
Sifa kuu ya mwandishi mahiri, ni kuandika ukweli tuu, "nothing but the truth" na kuandika kwa weledi kwa kuzingatia misingi ya uandishi, truthfullness, objectivity, impartiality, fairness and balancing, the right to privacy etc, vitu vyote hivi, Kibanda anavyo!.
Kwa maoni yangu, tuna waandishi wengi tuu ambao ni puppets wa wanasiasa!, hivyo wanapomuona fulani anafanyia gazeti la fulani, wanamdhania ni puppet wa mmiliki, siku akihama na kuhamia gazeti jingine, wanapata wasiwasi kuwa ule u puppet sasa utahamia kwa mmiliki mpya!.
Mimi ni mwandishi wa kujitegemea kwa kujitolea (silipwi na yeyote), nimenote siku nikiandika kuibonda CCM pongezi humiminika, siku nikianfika mazuri ya CCM, watu humu hunidhania nasi mimi ndio CCM!, siku nikiandika mabaya ya Chadema, cha moto huwa ninakipata!. Kamwe sitaacha kuandika ukweli ili tuu nisifiwe na walio wengi!. Kusimama kwenye ukweli daima, ndilo kosa pekee la Kibanda!.
Kiukweli waandishi wa habari, hatupaswi kabisa kuwa na upande, ila ni waandishi wachache sana ambao kiukweli kabisa hatuna upande!, the rest, most are puppets wa upande fulani!. That is wrong!.
Pasco.