Kibanda aliteswa na majasusi!

Mtu yeyote anaeshabikia uovu nae ni mwovu. na adhabu yake ni hapahapa duniani
 
Sarakasi ya mtoto wa mfalme!!! Haki ya nani kila kitu kina mwanzo na mwisho wake!! Hata libya Gaddafi alianza na alimaliza!! Je alimalizaje? Tuwe na busara na kuwafundisha wanafamilia namna ya ku-behave!!! Ni aibu sana!!
 
Kwa hakika hii imekaa vizuri, polisi wafanye kazi yao pasipokujali majina ya watu na position walizonazo katika jamii ili haki itendeke.
 
Poolleni sana watanzania wenzangu mnaodhani hii ni nchi yenu wakati ridhiwani anaamini kuwa sisi ni wapangaji kwenye shamba la baba yake lenye security guard wanaoitwa polisi...
 
Kati ya watu watakaoleta machafuko wakiachiwa ni pamoja na Ridhiwan,huyu jamaa analelewa sana sijui sheria zinasema nini! Ridhiwan amekera watu wengi sana kwa kauli yake hiyo ambayo naweza kusema ni ya kishenzi kwa sababu tu ya ulevi wa madaraka ya baba yake! Achunguzwe huyu!
 

Ni Eddo nn?
 
No suala hapa lazima liwe clear. Huyo RZ1 anao uhuru wa kusema kama ambavyo nyie pia mnasema.mbona hamkutaka wote waliojifanya wanajua ikulu ilivyomtesa ulimboka wakaisaidie polisi kiushahidi? Jambo sikubaliani na unyama aliofanyiwa kibanda lakin pia sitaki uhuru wa maoni udhibitiwe,watu waachwe waseme kama walivyosema ktk matukio mengi mengi yaliyopita.
 
thanks.
 

Kwa nini usimwache Ridhwan ajitetee mwenyewe au wewe ndiye huyo Ridhwani?
Vitendo vya wanafamilia ya Kikwete vinaashiria hitaji la kutafakari upya 'privileges' wanazopewa wanafamilia wa zitakazokuwa familia za marais wajao.
Kuna matumizi ya ovyo ya watu, vifaa na mali za walipa kodi wa nchi kuwagharimia watu wasiostahili kama Mke wa Kikwete na watoto wake kana kwamba nao walichagiliwa kwa kura !
Usalama wa Taifa umechakachuliwa na sasa kuonekana kama wafanyakazi wa familia hiyo, jambo geni kabisa katika utamaduni wa nchi hii.
Kuna minong'ono kibao juu ya kuzitumia nafasi zao za kuwepo ikulu kukosa kujitajirisha na kujikusanyia mali. Na sasa wakiwa wamelewa madaraka yao haramu wanatoa maagizo na matamko ya kuwaudhi na kuwakejeli watanzania!
Hivi Raisi wetu ni dhaifu kiasi cha kushindwa hata kuwakemea watu wa karibu yake namna ile?
 
Ina maana hili gazeti mpaka dakika hii halijafungiwa na Serikali kwa kuandika habari za uchochezi?

Sioni tofauti iliyolifungia Mwanahalisi na makala hii.
 

Una uhahkika na unayoyasema?
Na ile kampuni yake ya Caspian inayofanyafanya kazi kwenye migodi ya dhahabu kanda ya ziwa nayo iko Juba?

Kujitoa kwenye siasa za majukwaa haina maana kwamba ndo amejitoa siasa za Tanganyika, bado anahitaji sana kuendelea kudhibiti madaraka ya serikali ili kulinda mirija yake aliyowekeza Tanganyika.
 
Acha kuota wewe, wapi umemsikia mwenyekiti wa madaktari akileta usumbufu baada ya kufanywa vibaya kule mabwepande? Zaidi zaidi Kibanda atakuwa na adabu ili hilo jicho lililobaki liendelee kuwepo..!

Mpuuuuuuuuuuuuuuuuuz
 
Nimeishiwa maneno inatosha tu niseme nimesikitika na inasikitisha sana mambo haya kuendelea hapa nchini mwetu. Nimekuwa nikijiuliza hivi kweli wahalifu wamekuwa na nguvu kiasi hiki kuliko vyombo vya dola?
 
Hatukatai uhuru wa kusema ila ni uharaka wa RZ1 kutoa maoni yake hayo ukizingatia kwamba ule ushahidi uliotolewa na mwanaHalisi kuhusu ikulu kuhusika na mateso ya Ulimboka bado hayapata majibu. Mpaka leo vyombo vya dola havijatuambia Ramadhan Ighondu ni nani. Kwa muktadha huu nin rahisi mtu kuhisi RZ1 anataka kucover something.
 
its true kabisa mateso ya kibanda yamefanywa professionally

Sasa ktk hili haihitajiki uwe na elimu ya chuo kikuu au elimu/utaalamu wa kijasusi kugundua kwamba hii ni professional work

halafu eti kamanda wa kanda maalum ya dar es salaam afande mkuu, mheshimiwa sana KOVA anakuja na single ya kwamba huu ni uhalifu tu, tena anaunda na tume wakati majibu amesha-prempt

Je, wadau si wana haki ya kuhoji weledi (professionalism) ya kamanda wetu? Yeye kwa level yake ikitokea kama hili haraka haraka anatakiwa kutuambia kwa uwazi kabisa kwamba mateso haya yamefanywa professionally kwa malengo wanayoyajua wao wenyewe.

Ndio maana kwa kweli hatuna imani na jeshi letu la polisi
 
Hii ni Serikali dhalimu Mkuu Zogwale haina tofauti yoyote na ile Serikali ya Makaburu iliyokuwepo kule RSA.

 
Last edited by a moderator:
Ramadhan Ighondu ndiye mteseji wa Dr Ulimboka lakini hajahohiwa hadi leo. Nina wasiwasi kama Ridhiwani anaweza kukuguswa! Serikali corrupt hutesa na kuuwa watu hovyo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…