Acha kuota wewe, wapi umemsikia mwenyekiti wa madaktari akileta usumbufu baada ya kufanywa vibaya kule mabwepande? Zaidi zaidi Kibanda atakuwa na adabu ili hilo jicho lililobaki liendelee kuwepo..!Kweli nchi inajifanya kuwa iko mstari wa mbele kwa demokrasia kumbe ni kandamizi na udikteta tu!! Kwa nini tubake demokrasia? Waandishi wa habari wakiwemo editors ambao walitokea huko huko kwenye uandishi wa habari wanasaidia sana kuelimisha jamii, kuibua maovu ili mtu au nchi ijirekebishe, kutoa burudani, n.k. Sasa pale ambapo mtu anakosolewa tena kwa ushahidi badi hataki ila anachotaka ni kubaka demokrasia kwa ama kuua, kutesa au kutishia maisha ya mwandishi. Shujaa Kibanda, hata kama utabaki na jicho moja lakini bado utaandika na kuhariri habari!! You are a hero na historia itabaki kuwa historia. Pole sana mkuu Kibanda.
Rafiki yangu Pasco Mayala nadhani atasoma hili Uandishi wa Habari na Siasa ni hatari sana!
Mkuu hao ni wale wale wanaojua ni kitu gani walifanya kwa hiyo wanakuja hapa ili kupindisha ukweli!!!! Wakati tukijadili ile thread ya kutekwa na kuumizwa kwake nilisema hivi "Adui yako mlete karibu ili ummalize kwa urahisi". Bado nasimamia maneno haya!!! Huwezi kuniambia kuwe leo hii nimekuandika kwa skendo kubwa za kifisadi withh evidence halafu eti nikuache!! Wahusika wana connect the dot!!! Kibanda pia ni mtu wa karibu sana na mwanamtandao wa Chama cha Mauaji na mtu huyo ni tishio kwa Rais ajaye!!!!! tulihofu ataendelea kumjenga kisiasa mtu huyo ili ifikapo 2015 aweze kuwa safi kwa Uhuru Kenyata!!!! Sasa tufanyeje kama si kummaliza!!! Ninaamini walijua wameshamuua!!! Kwa hakika ataendelea kuandika na kuandika na kuandika kwa jicho hilo hilo moja!!! Ila tu nimejifunza kuwa Uandishi wa Habari na Siasa ni hatari sana!! Ila kwa bahati mbaya ndivyo waandishi na wahariri wengi walivyo kwa Tanzania hasa inapokaribia uchaguzi!! Tuwe makini sana!! Jifunzeni toka uchaguzi wa Kenya uliopita walijirekebisha sana tofauti na 2007 ambapo walishabikia sana na mwishowe madhara waliyaona!!
Na sasa taarifa zaidi zinasema lile jicho alipigwa risasi...na maeneo yale hakukusikia mlio wowote wa risasi, ina maana jamaa walikuwa na "Sailensa" jambazi wa kawaida sio rahisi kumilikihiyo kitu!
Ha ha ha nimecheka mno!! Yaani sina hakika kama unaweza kumteka baba yako!! Ni jana tu maskini kijana kichaa aliweze kumuua bibi yake na ndugu wengine wa ukoo na mama yake alipiga nondo na spring akajua ameua!!! Ila huyu kijana ni kichaa!!! Sasa kwa hiyo hao nao watakuwa kichaa? Tanzania ile amani na upendo vimeishia wapi? Kwa hiyo vimekuwa historia? Askofu Mokiwa naye kakoswa koswa juzi na issue iko polisi kwa upelelezi!! Ha ha ha!! Kama wa ulimboka aliletwa wa maigizo na wa Kibanda hawajakamatwa je hawa wa Mh. Mokiwa ambao hawakufanikiwa kumng'oa memo, kucha, kuvunja taya, mbavu, fuvu la kichwa kuharibu, etc je watakamatwa?? Siri kali!!
Wewe nae vipi ni risasi gani inayopiga jicho tu na bila kufumua kichwa chote? Au ndivyo silencer za kwenu zilivyo?
Halafu unakuta wanaoihusisha na Chadema issue hii ni wajinga fulani kama sijui Atongwele na pimbi wenzake ambao wanaonge pumba humu,mie nanyamaza wasije wakanisikia wakaning'oa kucha na meno yangu endeleeni tu nyie kama hamuwaogopiTISS na ccm yao
mi nimeshaogopa hadi kutoa coment hapa naona kama wataniua na mimi.
Basi kama ndivyo ilivyo basi siasa za kuuana au kulipiza kisasi hazina mashiko!! Kwa mantiki hii kazi imetumwa na walio madarakani!! Sasa wale wanaoituhumu CDM kwani iko madarakani?Kwa kawaida Majasusi ni kwa ajili ya watawala, mtawala akibadilika nao huhamia kwa mtawala mpya. Mtawala mpya akisema mteseni huyu , hata kama alikuwa mtawala Majasusi hawana maswali they have intuitive thinking.