GAGL
JF-Expert Member
- Aug 5, 2010
- 390
- 395
Katika kuifikia Tanzania isiyokuwa na ukimwi kama kampeni iliyozinduliwa na Mhe. Rais miaka michache iliyopita "Tanzania bila ukimwi inawezekana" ninapendekeza kiapo cha ndoa kiwe namna hii:- "Mimi X nakubali kumuoa/kuolewa na Y awe mke/mume wangu katika maisha yangu yote, katika shida na raha na naahidi kumpenda, kumlinda katika hali yoyote ile na naahidi mbele ya Mungu, kanisa/msikiti/serikali, waamini waliopo hapa, ndugu, jamaa na marafiki kutomsaliti mwenzangu kimwili kwa kushiriki zinaa na mtu mwingine, ee Mwenyezi Mungu nisaidie"
Hii ni mbinu mpya ya kisaikolojia ambayo inaweza kusaidia sana katika kupambana na janga hili la ukimwi, kwani njia pekee inayoeneza ukimwi kiurahisi ni ngono ikisaidiwa sana na ukosefu wa uaminifu katika mahusiano. Kama kutakuwa na uaminifu utakuwa imara katika ndoa basi hata katika mahusiano ya kawaida kutakuwa na uaminifu.
Nawasilisha.
Hii ni mbinu mpya ya kisaikolojia ambayo inaweza kusaidia sana katika kupambana na janga hili la ukimwi, kwani njia pekee inayoeneza ukimwi kiurahisi ni ngono ikisaidiwa sana na ukosefu wa uaminifu katika mahusiano. Kama kutakuwa na uaminifu utakuwa imara katika ndoa basi hata katika mahusiano ya kawaida kutakuwa na uaminifu.
Nawasilisha.