Elections 2010 Khatib ataka mrithi wa JK atoke Z'bar


Sasa wewe ni muongo. Kama wazanzibari hawakutaka Karume awe rais wao kwa nini hawakumpigia kura mpinzani wake? Kwa nini basi hao CCM walioona kuwa wamewekewa mgombea na bara hawakususia uchaguzi au kumpigia mpinzani wa Karume mdogo? Au mnataka kutuambia ni machogo waliokuja zanzibar kumpigia kura Karume wakati wazanzibari wote mlimpigie kura Maalim?i Acheni unafik na kutafuta visingizio. Nyinyi ndio mnaopiga kura kwa hiyo mnampata rais mayempigia kura.

Amandla........
 
Nimekusoma mkubwa Fundi Utumbo!ila unachopaswa kukumbuka Karume alichaguliwa na watanzania bara waliofanywa watumishi wa majeshi yetu ya ulinzi na usalama,au unataka reference? sogea karibu na feri ulizia kwa watu wanaojihusisha na safari za Zanzibar utajua kwamba ushindi kwa hawa jamaa ni lazima.
 

Uzushi mwingine! Yaani Karume alishinda kutokana na kura za wanajeshi na polisi wa bara ambao hata hawaruhusiwi kupiga kura katika uchaguzi wa zanziba kutokana na sheria zenu za ukaaji! Katika nchi ya watu takriban milioni moja hao askari machogo wako kiasi gani kiasi cha kuweza kuwachagulia rais? Nyinyi wenyewe mmegeukana wakati wa kupiga kura. Mkiwa pamoja mnajifanya hamumtaki Karume lakini ndani ya nafsi zenu mnaona heri yeyote kuliko mpemba! Ni ubaguzi wenu ndiyo uliompa ushindi Karume na si kuweko kwa machogo. Na ni ubaguzi huo huo utakaompa ushindi yeyote yule atakae simamishwa na CCM.

Amandla......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…