Kevin Durant anabadili tu mademu

Baby Nimah

JF-Expert Member
Oct 31, 2018
701
747
DURANT-2.jpg
CALIFORNIA,
Marekani: NYOTA wa NBA, Kevin Durant, amezidi kwa warembo, kwani taarifa zinasema sasa anatoka na modo Sabrina Brazil.
Taarifa zinanyetisha kuwa mkali huyu wa timu ya Golden State Warriors amekuwa akitoka na mrembo Sabrina tangu alipotengana na mrembo mwingine, Cassandra Anderson.

KD, 30, pia amekuwa akihusishwa kimapenzi na mpenzi wa zamani wa Chris Brown, Amy Shehab pamoja na mwimbaji Keri Hilson. Durant alisitisha uhusiano wake na Cassandra, Oktoba, mwaka jana.
Lakini fowadi huyo pia aliachana na mchumba wake Monica Wright mwaka 2014 kwa madai ya kushangaza.
DURANT-1-1024x516.jpg

Alisema: “Nilikuwa na mchumba, lakini sikujua jinsi ya kumpenda, unajua ninachokisema? Tulitengana kwa staili hiyo.”
Lakini Monica, ambaye anacheza kikapu kwenye Ligi ya Wanawake Marekani (WNBA), alitoa sababu tofauti akidai walitengana kwa sababu ya imani yake kali kwa Mungu.

Mrembo huyo alisema: “Nilikosolewa sana kutokana na hilo, lakini nadhani Mungu alikuwa upande wangu. Kwa sababu nilishikilia kile ambacho najua ni kweli, hicho ndicho Mungu atanituza badala ya kile ambacho watu duniani w a naamini ni kizuri.”
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom