Kesi ya Lundenga Sept. 23

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Kesi ya Lundenga Sept. 23

na Vumilia Kondo
Tanzania Daima~Sauti ya watu

KESI ya madai inayomkabili Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino Agency International, waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, Hashimu Lundenga, itaanza kusikilizwa rasmi Septemba 23 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu chini ya Hakimu Jagalile Mwaseba.

Kesi hiyo iliyofunguliwa Agosti 5 mwaka huu na mke wa Lundenga ,Twigi Hashimu Lundenga, mlalamikaji anataka kugawana mali walizochuma pamoja na mumewe huyo baada ya kumtelekeza na familia.

Hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo jana, Ritha Tarimo, alimtaka mwanasheria wa mlalamikaji (Twigi), kuwa anatakiwa kuwasilisha pingamizi la majibu yaliyoletwa na wakili wa Lundenga, Audax Kahendaguza, hadi ifikapo Septemba 19.

Licha ya kuwa Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania, Lundenga, pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu ya Yanga.

Licha ya dini ya Kiislamu kumruhusu Lundenga kuwa na mke zaidi ya mmoja, kinacholalamikiwa mahakamani hapo ni madai ya Lundenga kuitelekeza familia ya mke wake wa kwanza, baada ya kuoa mwanamke mwingine, aliyewahi kuwa mmoja wa Miss Tanga mwaka 1997.

Inadaiwa kuwa, baada ya Lundenga kumwoa mwanamke huyo wa Kitanga, alihamia katika nyumba mpya iliyoko Sinza, ambayo aliijenga akiwa na mke wa kwanza, huku akiitelekeza familia ya mke wa kwanza, hivyo mwanamke huyo anataka wagawane mali.
 
Kesi ya Lundenga Sept. 23

na Vumilia Kondo
Tanzania Daima~Sauti ya watu

KESI ya madai inayomkabili Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino Agency International, waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, Hashimu Lundenga, itaanza kusikilizwa rasmi Septemba 23 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu chini ya Hakimu Jagalile Mwaseba.

Kesi hiyo iliyofunguliwa Agosti 5 mwaka huu na mke wa Lundenga ,Twigi Hashimu Lundenga, mlalamikaji anataka kugawana mali walizochuma pamoja na mumewe huyo baada ya kumtelekeza na familia.

Hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo jana, Ritha Tarimo, alimtaka mwanasheria wa mlalamikaji (Twigi), kuwa anatakiwa kuwasilisha pingamizi la majibu yaliyoletwa na wakili wa Lundenga, Audax Kahendaguza, hadi ifikapo Septemba 19.

Licha ya kuwa Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania, Lundenga, pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu ya Yanga.

Licha ya dini ya Kiislamu kumruhusu Lundenga kuwa na mke zaidi ya mmoja, kinacholalamikiwa mahakamani hapo ni madai ya Lundenga kuitelekeza familia ya mke wake wa kwanza, baada ya kuoa mwanamke mwingine, aliyewahi kuwa mmoja wa Miss Tanga mwaka 1997.

Inadaiwa kuwa, baada ya Lundenga kumwoa mwanamke huyo wa Kitanga, alihamia katika nyumba mpya iliyoko Sinza, ambayo aliijenga akiwa na mke wa kwanza, huku akiitelekeza familia ya mke wa kwanza, hivyo mwanamke huyo anataka wagawane mali.

Jamani wanawake wa Tanga si mchezo Lundenga sikulaumu ila kumbuka watoto!1
 
Back
Top Bottom