Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Wadau mimi naishi na mtoto wa dada yangu, kwasababu dada yangu hana uwezo nilichukua jukumu la kumsomesha huyu mtoto, kwasasa yupo form four, jana kafukuzwa shule baada ya kugundulika ni mjamzito wa miezi mitano. Kwasababu sifahamu vema sheria zinazosimamia hili swala naomba kufahamu yafuatayo:-
1. Je ni sahihi huyu mtoto kufukuzwa shule hasa ukichukulia nimelipa ada mpaka siku atakapomaliza masomo yake?
2. Kijana aliyempatia uja uzito anakili kufanya hivyo ila anajibu jeuri sana kwamba nisimfuatefuate. Je ni hatua gani za kisheria naweza kumchukulia huyu kijana hasa ukichukulia huyu bint yetu ana umri wa zaidi ya miaka kumi na nane yaani ana miaka18 na miezi7 hivyo alikutana naye kimwili akiwa ana umri zaidi ya miaka18.
1. Je ni sahihi huyu mtoto kufukuzwa shule hasa ukichukulia nimelipa ada mpaka siku atakapomaliza masomo yake?
2. Kijana aliyempatia uja uzito anakili kufanya hivyo ila anajibu jeuri sana kwamba nisimfuatefuate. Je ni hatua gani za kisheria naweza kumchukulia huyu kijana hasa ukichukulia huyu bint yetu ana umri wa zaidi ya miaka kumi na nane yaani ana miaka18 na miezi7 hivyo alikutana naye kimwili akiwa ana umri zaidi ya miaka18.