ungonella wa ukweli
JF-Expert Member
- Mar 27, 2012
- 4,210
- 555
pembeni hapo shehe na poti yake otea kuna nini ndani
Picha kwa hisani ya Uamsho facebook
suna..........Mimi huwa najuliza kila siku sipati jibu.Hivi ndevu ndio uislam safi au?
mbona shehe anatoa ishara ya amani vidole viwili ananitisha
ni amani au ni alama ya ushindi..
suna..........
Mbinu za shekh Farid anazozitumia kutimiza malengo yake ya kisiasa ni mbinu za hali ya juu na ni za kigaidi,mi naamini serikali ilihusika katika utekaji wa Dr Ulimwomboka,lkn la huyu shekhe,ni kwamba alijificha makusudi ili atengeneze hali ya sintofahamu,na hatimae aendelee na mpango wake aliotoka nao Yemen.Watanzania tuwe makini.
Sheikh kumbe handsome! ile midevu ndiyo ilikua inakuharibia.
Na wale waliofanya vurugu na kushatarisha amani nchini huko Mbagala watafikishwa lini mahakamani?Kesi imetajwa leo katika mahakama ya Mwanakwerekwe na kisha ikahamishiwa katika mahakama ya Vuga.
Mawakili wametishia kujitoa katika kesi hyo kwa madai ya usumbufu wanaoupata wateja wao. Mawakili hao ni Salim Tawfik na Abdallah Juma wanaowawakilisha Sheikh Farid Hadi Ahmed na wenzake sita. Leo hii wamesusa kabisa kuingia mahakamani na wamesema wanakusudia kujitoa kutokana na uusmbufu wanaofanyiwa wateja wao wa kuhawangaisha.
Na sasa hivi mawakili hao wameshaondoka na watuhumiwa ndio wanafikishwa mahakamani wakiwa wamenyolewa ndevu zote wakiwa mahabusu. Kesi leo inatarajiwa kutolewa maamuzi ya masharti ya dhamana yaliyokuwa yanapingwa na mawakili wa utetezi ambao wameshaondoka mahakamani hapa.
Hatujui nini kitaendelea tena maana watu wamezuiliwa kuingia katika eneo la mahakamani. Nikipata updates nitawajulisha
Updates:
Mawakili wakisoma tamko la kutaka kujitoa kabla hawajaondoka mahakamani hapo.
Sheikh Farid akiwa kanyolewa ndevu akiwasili mahakama ya Vuga leo.
MORE UPDATES:
Sheikh Farid na wenzake wasomewa mashtaka mapya:
1) Kusababisha uvinjifu wa amani zanziba
2) Kusababisha uharibifu wa mali kisiwani zanzibar kutokana na vurugu
3) Kushawishi na kuchochea vurugu zilizosababisha kuhatarisha maisha ya watu na serikali kuingia hasaraK
Aidha mtuhumiwa mmoja anatuhumiwa kumtukana Kamishna wa Polisi Zanzibar Musa Ally Musa
washtakiwa wote wamenyimwa dhamana kwani ni Jaji pekee ndie anayeweza kutoa dhamana kwa makosa yao lakini wana haki ya kukata rufaa kudai dhamana katika mahakama ya juu.
Tunaomba dk shein aendelee hivohivo ,maana kuna watu wanataka kutumia dini ya mwenyezi mungu vibaya, kama wamezoea uarabuni basi sio tanzania. Vinginevyo wasajili vyama vya siasa tuelewe moja na si kutumia dini ya allah!
Amenyolewa ndefu bila ridhaa yake? Au kaamua kunyoa mwenyewe ili ionekane anagandamizwa na serikali?
duu mkuu kama waislamu wote tanzania tungekuwa hivo nchi ingewaka moto zaid, punguza jazba. Subra ni muhimu sana!Huna haja ya kujificha ...wewe utaamini kila aliyetkwa ambae mkristo...Kwa muislamu kwako wewe hana haki yeyote... Lakini sio nyakati hizi... Lolote baya atakalofanyiwa Seikh Farid ,ndio hilo hilo litawakuta Mapadri/Askofu/wachngaji.