Kesi ya kina Mramba: Serikali itashindwa!

Tutabanana hapa hapa nchini wasidhani kuna mtu atakimbia kanchi ketu kazuri.
Ikifika wakati ambao najua kwa kalenda ya Mungu upo na waja na upo sasa watakuwa na la kusema tu!
Tusubiri wakati wa unabii huu.
 
tena Mlamba amekwisha sema kuwa alikuwa na baraka toka kwa Mkapa . JK na Pinda wamekwisha kumsafisha . sijui hiyo inaendelea ya nini kama si kuchezea wananchi masikini wa tanzania . Hosea na mwanyika wamesafishwa na sabuni ya mkaa kwa hiyo tusitegemee jipya . hii ndiyo serikali ya JK aliyekuwa matumaini ya wanyonge miaka kama mitatu iliyopita. Tunaelekea kuzimu
 
Mimi tangia awali nilisema kesi hii hina maana yoyote kwa sababu

1. Ushahidi lazima utoke kwenye vikao vya baraza la mawaziri kitu ambacho kisheria hakiruhusi.

2. Si mahakama, au chombo chochote kile chenye madaraka ya kuhoji au kujua yaliyofanyika ndani ya Vikao vya Baraza la Mawaziri.
 
Mimi tangia awali nilisema kesi hii hina maana yoyote kwa sababu

1. Ushahidi lazima utoke kwenye vikao vya baraza la mawaziri kitu ambacho kisheria hakiruhusi.

2. Si mahakama, au chombo chochote kile chenye madaraka ya kuhoji au kujua yaliyofanyika ndani ya Vikao vya Baraza la Mawaziri.

Kama tayari serikali imeshindwa kesi kwa nini wanatupotezea muda? Kumbe bado sisi ni mabwege sana!
 
Mimi tangia awali nilisema kesi hii hina maana yoyote kwa sababu

1. Ushahidi lazima utoke kwenye vikao vya baraza la mawaziri kitu ambacho kisheria hakiruhusi.

2. Si mahakama, au chombo chochote kile chenye madaraka ya kuhoji au kujua yaliyofanyika ndani ya Vikao vya Baraza la Mawaziri.

Kwa ufafanuzi tuu ni kwamba Mramba Yona na Mgonja wamejiandaa vilivyo dhidi ya mashtaka waliyofunguliwa.Ushahidi walionao unahusisha hata makabrasha mengine ambayo kwa hali ya kawaida wananchi hawapaswi kuyaona.

Makabrasha hayo ni pamoja na copy ya original minutes za vikao vya baraza la Mawaziri ambavyo ni vitu nyeti vya Serikali.

Swali langu ni je haya mambo yakiwekwa wazi mahakamani serikali ya JK itakuwa kwenye nafasi ipi.Kwa sababu hawa mabwana wamejiandaa kumwaga mchele kwenye kuku wengi.Siku wakifanya hivyo mahakamani sijui kama kwenye jengo jeupe pale magogoni kama kutakalika.
 
..binafsi naona ni bora wangeshitakiwa kwa mashtaka ya rushwa.

..suala la kukaidi ushauri wa wataalamu na kuitia hasara serikali sidhani kama kuna anayeweza kusalimika huko serikalini. tena inaweza kuwa njia ya political witch-hunting.



..hebu chukulia mfano wa ndugu yetu John Magufuli. Nadhani ni kiongozi mzuri tu, lakini alikaidi ushauri wa wataalamu na kuvunja kituo cha mafuta kule Mwanza. Mahakama ilitoa hukumu kwamba Magufuli/serikali walivunja sheria na wanapaswa kulipa mabilioni ya fedha kama fidia.

..pamoja na kwamba naamini Magufuli is a nice chap, lakini alivunja sheria, alikaidi ushauri wa wataalamu, na ameitia serikali hasara. sasa kwanini na yeye hashtakiwi kama Mramba, Yona , na Mgonja?
 

...lakini alivunja sheria, alikaidi ushauri wa wataalamu, na ameitia serikali hasara. sasa kwanini na yeye hashtakiwi kama Mramba, Yona , na Mgonja?

Kama alivunja sheria, ina maana huo haukuwa ushauri, bali ilimlazimu afuate agizo la wataalam, agizo la sheria.

Lakini kama ulikuwa ni ushauri, ina maana hakulazimika kuufuata, hakuna sheria iliyomlazimu afuate ushauri.

Naomba source inayosema Magufuli alivunja sheria inayosema ni lazima ufuate ushauri.
 
Dilunga said:
Naomba source inayosema Magufuli alivunja sheria inayosema ni lazima ufuate ushauri.


Dilunga,

..labda uandishi wangu mbaya umekuchanganya kidogo. naomba nifafanue.

..hili suala lilikwenda mahakamani na huko akaamuliwa kwamba serikali imlipe fidia mmiliki wa kituo cha mafuta kilichobomolewa kwa amri wa Waziri John Pombe Magufuli.

..kwa wakati huu, tafsiri yangu ni kwamba, mmiliki wa kituo cha mafuta alifuata sheria kujenga kituo chake mahala hapo.

..kwa maana nyingine amri ya serikali iliyotolewa na Waziri Magufuli ilikuwa ni kinyume cha sheria. more directly serikali na Magufuli walivunja sheria.

..sina uwezo wa kukupatia source inayosema kwamba lazima Waziri afuate ushauri wa wataalamu wake. naamini haipo. pamoja na ukweli huo, nadhani tuko pamoja katika imani kwamba Waziri ana wajibu wa kufuata sheria za jamhuri wakati wote.

..Hukumu ya shauri la serikali vs mfanya biashara wa mafuta wa Mwanza inanilazimu kuamini kwamba Magufuli alivunja sheria na matokeo yake ameitia hasara serikali.

NB:

..ninachojaribu kuonyesha hapa ni jinsi mashtaka dhidi ya Mramba na Yona yanavyoweza kusababisha watu wazuri tu kama Magufuli[if you believe he is good man] kuandamwa.

..kwa maoni serikali ingetafuta mashtaka yenye nguvu zaidi kuliko haya ya kutia hasara na kukaidi ushauri wa wataalamu.
 
hakuna seriousness yeyote na hii serikali,yaani ni ufisadi kwenda mbele,unaweza kukuta wameshakaa na upande wa defence kuunda kesi ambayo wanajua tayari itaisha vipi...at the end of the day trillions za richmond,BOT,Meremeta,IPTL etc zote zimepotea lakini hakuna conviction hata moja then unajiuliza hizi trillions zimeenda wapi?...ila one thing for sure waliokula hizo pesa ni wale waliopewa kuzisimamia!
 
Kuna baadhi yetu tumepata kukalia viti vya ama Mramba, Yona au Mgonja. Utaratibu wa kutoa msamaha wa kodi ulikuwa ni aidha mlipa kodi kwenda kwa Waziri au Katibu Mkuu na kueleza kesi yake. Wakati mwingine mlipa kodi ali-approach Kamishna wa Kodi.

Hawa viongozi Serikalini, waliandika Waraka wa Kabineti, na waraka ulijadiliwa na Kabineti. Endapo ulikubaliwa, Katibu Mkuu akishirikiana na Mwanasheria Mkuu aliandika Tangazo katika Gazeti la Serikali, lililomsamehe huyo mlipa kodi. Kwa hiyo haieleweki Mgonja alikosa nini kama alikuwa anatekeleza agizo la Serikali.

Ieleweke pia kwamba Katiba ya Tanzania inatamka kwamba Kabineti ni mshauri tu wa Rais, na kwamba sio lazima Rais akubali ushauri wa Kabineti. Kwa hiyo hata Mramba na Yona walikuwa wanatekeleza agizo la Rais, kama waraka wao ulikubaliwa.

J.K. anafahamu utaratibu huu fika, kwa vile amepata kuwa Waziri wa Fedha. Naona ama J.K. amechanganyikiwa kukubali hawa washitakiwe kwa matumizi mabaya ya madaraka, au huu ni usanii tu kuwa "hood-wink" WaTz eti anapiga vita ufisadi.

Endapo Mramba na wenzake watatiwa hatiani, hakuna mwananchi aliyepata kuwa na madaraka makubwa Serikalini ataokoka. Lazima wakati mmoja, alifanya mambo ambayo baada ya Kabineti kuyakubali, hayakufanikiwa ilivyotegemewa. Kwa hiyo hata sisi na wengine wengi wastaafu tunaweza kushtakiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka. Upuuzi mtupu.

Na huku kusema eti Idara ya Kodi ilishauri msamaha usitolewe, ni upuuzi mtupu. Idara ya Kodi ni mshauri, na ushauri wake unaweza kukubaliwa au kukataliwa. Bora tu Kabineti ilikubali ikiwa chini ya uenyekiti wa Rais.
 
Last edited:
Kuna baadhi yetu tumepata kukalia viti vya ama Mramba, Yona au Mgonja. Utaratibu wa kutoa msamaha...

J.K. anafahamu utaratibu huu fika, kwa vile amepata kuwa Waziri wa Fedha. Naona ama J.K. amechanganyikiwa kukubali hawa washitakiwe...

Na kama kweli umewahi kuwa Waziri, basi ungetakiwa kujua kwamba Rais wa Tanzania hana mamlaka, haruhusiwi kisheria, kuingilia kazi za DPP; sio Kikwete aliyeamuru au kuruhusu watuhumiwa washitakiwe. Mzee wangu, wewe ulitakiwa uwe unajua hilo!

Na pia tukumbuke kina Mramba wameshitakiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi ( Penal Code, 2002, Kipengele 96 (1)). Taratibu na sheria ziko vitabuni, za nini kama zisipotumika kushitaki watu?


Any person who, being employed in the public service, does or directs to be done, in abuse of the authority of his office, any arbitrary act prejudicial to the rights of another is guilty of...

Na zaidi, fahamu kwamba hawajashitakiwa kwa kukataa ushauri pekee, bali kwa kutofuata sheria za manunuzi na sheria za uchimbaji madini:


STATEMENT OF OFFENCE

ABUSE OF OFFICE: Contrary to Section 96 (1) of the Penal Code [Cap.16 R.E. 2002].

MRAMBA S/O BASIL PESAMBILI and DANIEL S/O AGGREY NDHIRA YONA, between August 2002 and 14th June, 2004 within the City and Region of Dar es Salaam, being persons employed in the public service and serving in their respective capacities as Minister for Finance and Minister of Minerals and Energy respectively,
did jointly and together abuse the authority of their offices by arbitrarily procuring M/S ALEX STEWART (ASSAYERS) UK and its subsidiary Company M/S ALEX STEWART (ASSAYERS) GOVERNMENT BUSINESS CORPORATION to sign and execute gold production assaying agreement in Tanzania
in contravention of the Public Procurement Act [Cap.410 R.E.2002] and the Mining Act [Cap.123 R.E.,2002] respectively.

Tupo wote Mzee wangu?

Kwa hiyo usijaribu kumtetea tetea Yona na Mgonja na Mramba kwa ku imply wanaweza kujifanyia wanavyotaka, eti hakuna atakaepona. Wamevunja sheria! Usijaribu kuisafisha status quo na tawala zenu zilizovurunda nchi.

Shikamoo Mzee.
 
Mheshimiwa Dilunga,

Nashukuru kwa ku-react juu ya maoni yangu kuhusu kesi ya Mramba, Yona, na Mgonja.

Nilichofafanua ni utaratibu unaotumika kupata kibali ili waziri aingie ktk mkataba na taasisi yoyote tunayotaka ifanye kazi fulani. Kama Mramba, Yona na Mgonja waliandaa Cabinet Paper na ikakubaliwa, waliyotekeleza baadaye ni maamuzi ya Rais.

Naelewa kwamba DPP haagizwi na Rais au chombo chochote. Lakini DPP haamui mambo mazito kama kuwapeleka kortini watu mashuhuri kama ex-ministers na permanent secretaries,bila kushauriana na uongozi wa serikali. Kwa maoni yangu, ni lazima Rais alikubaliana na DPP juu ya kuendelea na kesi hii.

Jambo moja ningetaka kufafanua zaidi ni kwamba siwatetei hawa watuhumiwa. Kama kuna ushahidi kwamba walipokea rushwa kabla ya kuandaa Cabinet Paper, basi hilo ni kosa. Lakini ijulikane kwamba sheria ya manunuzi pamoja na sheria ya uchimbaji madini, zote zinaweza kuwekwa kando kwa maelezo yanayoainishwa katika Waraka wa Cabinet na Rais akikubali, basi utekelezaji unaanza.

Umemalizia kwa kusema tawala zetu zilivurunda. Sijui ni tawala zipi za nchi hii ambazo hazijavurunda. Tunawasubiri kizazi kipya mtuokoe.
 
Mheshimiwa Dilunga,

Nashukuru kwa ku-react juu ya maoni yangu kuhusu kesi ya Mramba, Yona, na Mgonja.

Nilichofafanua ni utaratibu unaotumika kupata kibali ili waziri aingie ktk mkataba na taasisi yoyote tunayotaka ifanye kazi fulani. Kama Mramba, Yona na Mgonja waliandaa Cabinet Paper na ikakubaliwa, waliyotekeleza baadaye ni maamuzi ya Rais.

Naelewa kwamba DPP haagizwi na Rais au chombo chochote. Lakini DPP haamui mambo mazito kama kuwapeleka kortini watu mashuhuri kama ex-ministers na permanent secretaries,bila kushauriana na uongozi wa serikali. Kwa maoni yangu, ni lazima Rais alikubaliana na DPP juu ya kuendelea na kesi hii.

Jambo moja ningetaka kufafanua zaidi ni kwamba siwatetei hawa watuhumiwa. Kama kuna ushahidi kwamba walipokea rushwa kabla ya kuandaa Cabinet Paper, basi hilo ni kosa. Lakini ijulikane kwamba sheria ya manunuzi pamoja na sheria ya uchimbaji, zote zinaweza kuwekwa kando kwa maelezo yanayoainishwa katika Waraka wa Cabinet na Rais akikubali, basi utekelezaji unaanza.

Umemalizia kwa kusema tawala zetu zilivurunda. Sijui ni tawala zipi za nchi hii ambazo hazijavurunda. Tunawasubiri kizazi kipya mtuokoe.


Jamani nyie mnasema nini ? Hakuna kesi hapa .Hii ni kama kesi ya Zombe , Mahalu na wengineo ,maadam NEC wamesema yale juzi kule Dodoma sitaku kupoteza muda wangu kuamini kuna kesi .Hakuna cha utawala bora wa DPP kuwa independent .Naamua kuangalia mambo haya kwa mtimzamo wa layman aliye kataa tamaa na ndivyo itakavyo kuwa .Ni siasa tupu nothing much .JK alitaka kuonekana yuko seruious ku cover EPA na Meremeta , na mengineyo yote .Serikali hii haina ukweli na siwezi kuiamini .
 
Wakuu,

Endapo kilichoambatanishwa ndiyo mashtaka dhidi yao basi tujue kazi ipo mbele yetu. Serikali itadaiwa mabilioni na tutakuwa tumechezea akili za watu na kupoteza heshima ya taifa!

Viva, GoT, Viva wanasheria wetu mnaofungua mashtaka ya namna hii.

Safari ni ndefu sana!

i65_FACTS31.07.09.jpg

Bado wanachapa mguu....
 
I think you r very right...Haiwezekani kesi ya high profile namna hiyo huyo Dilunga anataka kutuambia DPP hajaishirikisha serikali.... Tena lazima ijadiliwe ilikujua ina impact gani kwenye usalama wa nchi.... Guilty or not Guilty...I just doubt if they r guilty. Nakumbuka kabla ya kuwa engage Alex Stewart kulikuwa na mjadala mkali sana kwamba Co za madini wanatuibia... hawakuwa wa declare the real value of the gold they exported. Ndio likaja wazo laku tafuta kampuni ya ku audit madini kabla ya ku export... Then AS was engaged. Ripot zinaonyesha all these were discussed in the cabinet and the President...Hon Mkapa approved...ss case iko wapi.. By the way...do u know the power of the president in the Outgoing Constitution?
 
Back
Top Bottom