Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Kesi ya Dk. Mahanga kupinga `ukihiyo yaahirishwa
Imeandikwa na Flora Mwakasala; Tarehe: 14th January 2011 @ 23:20
MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala, imeahirisha kesi ya madai ya kulipwa Sh bilioni moja iliyofunguliwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kazi na Ajira, Dk. Makongoro Mahanga, mpaka Februari 24 mwaka huu itakapotajwa tena.
Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Esther Mwakalinga aliahirisha kesi hiyo jana baada ya Mahanga kudai kuwa hatakuwepo mahakamani hapo kwa kuwa amesafiri kwenda Dodoma.
Mahanga ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea alifungua kesi akidai kulipwa zaidi ya Sh bilioni moja na mwanaharakati Kainerugaba Msemakweli kutokana na kumtaja kwenye orodha ya mafisadi wa elimu.
Kwa mujibu wa Jalada la kesi hiyo, Februari 7 mwaka jana Msemakweli alidaiwa kuwa aliitisha mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuzindua kitabu alichokiandika ambacho
Mahanga anadai kuchafuliwa jina lake kwa kuandika habari za uongo dhidi ya taaluma yake.
Katika mkutano huo Msemakweli alidaiwa kutumia kikao hicho alichoitisha kwa ajili ya uzinduzi wa kitabu chake cha jina la Mafisadi wa Elimu Toleo la Kwanza kumchafua jina Mahanga.
Katika ukurasa wa mbele wa kitabu hicho anadaiwa kuweka picha ya Mahanga na katika ukurasa wa 12, 13, 14 kulikuwa na picha nyingine huku kukiwa na taarifa na maelezo ya uongo ikiwa ni pamoja na kueleza jinsi Mahanga alivyoghushi vyeti vya elimu ya juu.
Aidha katika ukurasa wa 14 katika aya ya pili na tatu kulikuwa na baadhi ya maneno yanayosomeka kama, Ufisadi wa Mahanga...Pia kwenye Fedha za Umma.
Mbali na kudaiwa kughushi vyeti vya elimu pia Mahanga anadaiwa kuchukua fedha za umma kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na kuzitumia kwa ufisadi.
Imeandikwa na Flora Mwakasala; Tarehe: 14th January 2011 @ 23:20
MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala, imeahirisha kesi ya madai ya kulipwa Sh bilioni moja iliyofunguliwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kazi na Ajira, Dk. Makongoro Mahanga, mpaka Februari 24 mwaka huu itakapotajwa tena.
Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Esther Mwakalinga aliahirisha kesi hiyo jana baada ya Mahanga kudai kuwa hatakuwepo mahakamani hapo kwa kuwa amesafiri kwenda Dodoma.
Mahanga ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea alifungua kesi akidai kulipwa zaidi ya Sh bilioni moja na mwanaharakati Kainerugaba Msemakweli kutokana na kumtaja kwenye orodha ya mafisadi wa elimu.
Kwa mujibu wa Jalada la kesi hiyo, Februari 7 mwaka jana Msemakweli alidaiwa kuwa aliitisha mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuzindua kitabu alichokiandika ambacho
Mahanga anadai kuchafuliwa jina lake kwa kuandika habari za uongo dhidi ya taaluma yake.
Katika mkutano huo Msemakweli alidaiwa kutumia kikao hicho alichoitisha kwa ajili ya uzinduzi wa kitabu chake cha jina la Mafisadi wa Elimu Toleo la Kwanza kumchafua jina Mahanga.
Katika ukurasa wa mbele wa kitabu hicho anadaiwa kuweka picha ya Mahanga na katika ukurasa wa 12, 13, 14 kulikuwa na picha nyingine huku kukiwa na taarifa na maelezo ya uongo ikiwa ni pamoja na kueleza jinsi Mahanga alivyoghushi vyeti vya elimu ya juu.
Aidha katika ukurasa wa 14 katika aya ya pili na tatu kulikuwa na baadhi ya maneno yanayosomeka kama, Ufisadi wa Mahanga...Pia kwenye Fedha za Umma.
Mbali na kudaiwa kughushi vyeti vya elimu pia Mahanga anadaiwa kuchukua fedha za umma kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na kuzitumia kwa ufisadi.