Kesi ya daktari wa Michael Jackson

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
Dr Conrad Murray

Jaji amemwamuru daktari binafsi wa Michael Jackson ashtakiwe kwa kuua bila kukusudia.

Jaji Michael Pastor alitoa uamuzi huo dhidi ya Dr Conard Murray katika kesi ya awali mjini Los Angeles.

Waendesha mashtaka walisema kwamba alimgawia dawa ya usingizi yenye sumu iliyochanganywa na dawa nyingine na kushindwa kumhudumia ipasavyo.

Dr Murray, mwenye umri wa miaka 57, amekana kuhusika na makosa hayo, na kusema hakumgawia Jackson chochote chenye sumu.

Jaji Pastor ametoa amri hiyo dhidi ya mtaalamu huyo wa moyo katika siku ya sita ya kesi hiyo.

Pia ameiomba bodi ya utabibu ya California kufuta leseni ya Dr Murray itakayomzuia kufanya kazi kwenye jimbo hilo.

Dr Murray anakabiliwa na kifungo cha miaka minne gerezani iwapo atapatikana na hatia.

BBC Swahili - Habari - Kesi ya daktari wa Michael Jackson
 
zungumzia mambo ya maana, bado unaabudu binadamu karne hii? tufuta habari yenye kuleta mabadiliko ya watu kimaendeleo
 
Back
Top Bottom