Kesi namba 458 (Jamhuri v JamiiForums) Shahidi wa Jamhuri ashindwa kufika Mahakamani! Kesi yapigwa kalenda

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,808
11,973
Kesi namba 458 (Jamhuri v Maxence Melo na mwenzake Micke William) inayohusu kuendesha mtandao bila kutumia Kikoa cha do.TZ na Kuzuia Upelelezi wa Polisi imeendelea leo Agosti 1, 2019 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu.

Upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili Daisy Makakala huku upande wa Utetezi ukiwakilishwa na Wakili Peter Kibatala mbele ya Hakimu Huruma Shaidi.

Wakili wa Jamhuri, Daisy Makakala ameiambia Mahakama kuwa shauri hilo lilikuwa mbele ya Mahakama kwa ajili ya kusikilizwa lakini kutokana na kukosekana kwa shahidi wao wa mwisho, Tully Esther Mwambapa ambaye yupo nje ya mkoa, anaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kusikilizwa kwa shauri hilo.

Upande wa Utetezi ulikubali kuahirisha shauri hilo lakini pia Wakili Kibatala amesema upande wa utetezi hawawezi kupinga sheria za nchi hivyo aliiomba Mahakama imtake Wakili wa Jamhuri kuleta shahidi wao huyo wa mwisho ili shauri hilo lisikilizwe na kuisha.

Shauri hili limeahirishwa tena hadi Agosti 26, 2019 huku upande wa Jamhuri ukisisitiza kuwa utajitahidi shahidi wao afike siku hiyo

Katika shauri hilo lililofunguliwa Desemba 2016 na kuanza kusikilizwa Februari 2017, tayari mashahidi zaidi ya Watatu kutoka upande wa Jamhuri wameshasikilizwa na shahidi wa mwisho kusikilizwa ilikuwa mnamo Novemba 07, 2018.

Baada ya hapo shauri limekuwa likiahirishwa huku sababu kadhaa zikitolewa na kubwa ikiwa ni kukosekana kwa shahidi.

------
Kujua mashauri yote ya JamiiForums yanavyoendelea tembelea: Muendelezo wa Kinachojiri Kisutu: Kesi za Jamhuri dhidi ya JamiiForums
 
Awamu ya kishamba Sana Hii......Alieliingiza Lile dude pale magogoni Afe kifo kibaya Sana
Awamu ya kupeana mikesi isiyo na kichwa wala Miguu

Wasukuma mtanisamehe......Sio Siri mtabaki Washamba na Viburi Milele
 
Hivi nani ana trust judicial system ya hii shithole country?

Tena kwa kesi zenye kuihusisha regime ndani?

The whole system ni inherently uozo mtupu!

Vunja vunja kila kitu weka katiba mpya,tume huru na commissions huru za kila kitu then uone kuna ms3ng3 anaweza mess with the citizens!
 
Hivi nani ana trust judicial system ya hii shithole country?

Tena kwa kesi zenye kuihusisha regime ndani?

The whole system ni inherently uozo mtupu!

Vunja vunja kila kitu weka katiba mpya,tume huru na commissions huru za kila kitu then uone kuna ms3ng3 anaweza mess with the citizens!
Sawa Sawa kbsa mzee baba

Ova
 
Dah, sometime mkubwa akijamba huona aibu na kujishtukia shtukia tu.
Kwa hili serikali imejamba na inajishtua yenyewe hamna point hapo ni danadana tu.
 
Kesi namba 458 (Jamhuri v Maxence Melo na mwenzake Micke William) inayohusu kuendesha mtandao bila kutumia Kikoa cha do.TZ na Kuzuia Upelelezi wa Polisi imeendelea leo Agosti 1, 2019 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu.

Upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili Daisy Makakala huku upande wa Utetezi ukiwakilishwa na Wakili Peter Kibatala mbele ya Hakimu Huruma Shaidi.

Wakili wa Jamhuri, Daisy Makakala ameiambia Mahakama kuwa shauri hilo lilikuwa mbele ya Mahakama kwa ajili ya kusikilizwa lakini kutokana na kukosekana kwa shahidi wao wa mwisho, Tully Esther Mwambapa ambaye yupo nje ya mkoa, anaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kusikilizwa kwa shauri hilo.

Upande wa Utetezi ulikubali kuahirisha shauri hilo lakini pia Wakili Kibatala amesema upande wa utetezi hawawezi kupinga sheria za nchi hivyo aliiomba Mahakama imtake Wakili wa Jamhuri kuleta shahidi wao huyo wa mwisho ili shauri hilo lisikilizwe na kuisha.

Shauri hili limeahirishwa tena hadi Agosti 26, 2019 huku upande wa Jamhuri ukisisitiza kuwa utajitahidi shahidi wao afike siku hiyo

Katika shauri hilo lililofunguliwa Desemba 2016 na kuanza kusikilizwa Februari 2017, tayari mashahidi zaidi ya Watatu kutoka upande wa Jamhuri wameshasikilizwa na shahidi wa mwisho kusikilizwa ilikuwa mnamo Novemba 07, 2018.

Baada ya hapo shauri limekuwa likiahirishwa huku sababu kadhaa zikitolewa na kubwa ikiwa ni kukosekana kwa shahidi.

------
Kujua mashauri yote ya JamiiForums yanavyoendelea tembelea:
Mungu ibariki JF
 
Back
Top Bottom