Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,981
Kesi namba 458 ya mwaka 2016 (Jamhuri dhidi ya aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media na Mwanahisa wake) imesikilizwa leo, 20 Agosti 2020 majira ya saa tano asubuhi mbele ya Hakimu Huruma Shaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar
Mara ya mwisho, kesi hii ilisikilizwa Julai 30, 2020
Leo washitakiwa wamejitetea katika kuelekea hitimisho la kesi hii.
Mawakili wa Utetezi Walikuwa ni Peter Kibatala na Jeremiah Mtobesya huku Upande wa Jamhuri akiwa ni Wakili Faraji Nguka
Kibatala ndiye aliyeanza kumuuliza Maswali Maxence Melo mara baada ya kujitambulisha na kula kiapo...
Kibatala: Mwambie Hakimu kama unakumbuka mashitaka
Maxence: Ndio nayakumbuka Mashtaka
Kibatala: Shitaka la kwanza linasema wewe na Mwenzako mlioperate JamiiForums ambayo haijasajiliwa hapa Nchini, Mwambie hakimu kuhusiana na hili
Maxence: Sisi tulikuwa tumesajilia Nchini na tulikuwa tunaitumia
Kibatala: Ni kweli mlikuwa wakurugenzi wawili?
Maxence: Si kweli kwamba tulikuwa wakurugenzi wawili
Kibatala: Wewe ulikuwa na uhusiano gani wa Jamii Media Company Limited?
Maxence: Nilikuwa kama Secretary na Director
Kibatala: Wenzetu walileta ushahidi wa BRELA (P1) barua hiyo inaonesha kwamba ulikuwa Secretary na Director
Maxence: Ni kweli, nilikuwa Secretary na Director wakati tunasajili kampuni.
Kibatala: Je, ni kweli mlisajili?
Maxence: Ni kweli tulisajili tarehe 20 Juni 2008
Kibatala: Wao wanasema hadi kipindi cha mashitaka (2016) ulikuwa Mkurugenzi (Director).
Maxence: Tulifanya mabadiliko, niliandika barua BRELA ya kufanya Mabadiliko ya kujiondoa kuwa Secretary na mabadiliko kwenye ukurugenzi. Siwezi jua nini kipo BRELA kwani nilinyimwa faili niweze kuangalia kama bado wananitambua kama Mkurugenzi au la! Walisema shauri lipo mahakamani hawezi kunipa faili.
Kibatala: Hii Jamii Media kwamba ilioperate bila kusajiliwa na kikoa cha do.tz, kwanza hii Do.tz ni nini?
Maxence: Hakuna kitu kama hicho inatakiwa kuwa (dot tz). Yaani jamiiforums.co.tz au jamiiforums.or.tz. au jamiiforums.ac.tz
Kibatala: Kuna shahidi alikuja kubadilisha kuhusiana hiyo do.tz?
Maxence: Shahidi wa kwanza wa Jamhuri pia alisema walicholeta kwenye hati ya mashitaka sio sahihi. Shahidi huyo alisema tumeshasajili na alisema tulikuwa na domain mbili. Alitoa vielelezo kuthibitisha majina yalikuwa yamesajiliwa. Alikuwa anaongoza in-chief na yeye ndo alikuwa Msajili wa vikoa.
Kibatala: Vipi kuhusu kutumia kikoa?
Maxence: Tulisajili domain mbili alikuja nazo shahidi. D1 iliyoingizwa kama kielelezo na kinaonesha tulisajili domain mbili, www.jamiiforums.co.tz na www.jf.co.tz
Kibatala: Wanasema hamtumii ni kweli?
Maxence: Tunatumia domain zote mbili na zimesajiliwa. Ikiwezekana mtu yeyote azitembelee aone kama zinafunguka
Kibatala: Unaposema tutembelea unamaanisha nini?
Maxence: Ukitembelea Domain hizo zinafanya kazi. Mtu yoyote anaweza kutumia simu au kifaa chochote cha kidijitali chenye mfumo wa intaneti kuangalia kama zinafanya kazi.
Kibatala: PW1 wakati anaulizwa maswali na wakili Tundu Lissu baadae mimi, alisemaje?
Maxence: PW1 alikiri mwaka 2009 alishirikiana na mimi kuhamasisha watanzania kusajili kikoa cha .tz. Shahidi huyo alisema haikuwa lazima kutumia bali ilikuwa ni kuhamasisha uzalendo
Kibatala: Wewe na mwenzako hamkutoa ushirikiano kwa Polisi. Unasemaje kuhusiana na kuzuia upelelezi?
Maxence: Mimi sijazuia upelelezi
Kibatala: Wenzetu walitoa vielelezo vya barua kwamba barua hii ndo msingi wa wao kwa Polisi kutoa Ushirikiano. Mwambie Hakimu kuhusu hii barua ya Januari 26, 2016 imekuwa addressed kwa nani na ilitoka wapi?
Maxence: Ilitoka Wizara ya Mambo ya Ndani, Cyber Crimes Unit. Ilielekezwa kwa Mwanasheria wa Jamii Forums Media.
Kibatala: Mwambie mheshimiwa Hakimu kama wewe ni Mwanasheria
Maxence: Mimi sio Mwanasheria
Kibatala: Kuna Shahidi alisema wewe ni Mwanasheria?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Jamii Forums Media ni kitu gani?
Maxence: Sijui
Kibatala: Taasisi zilizozungumziwa na mashahidi wote ni zipi?
Maxence: Mashahidi walikuwa wanazungumzia Jamii Media Company Limited na wengine Jamii Forum
Kibatala: Hii barua imesainiwa na nani?
Maxence: Imesainiwa na Joshua Mwangasa – ASP
Kibatala: Joshua Mwangasa alishawahi kutoa ushahidi?
Maxence: Hajawahi kuja mahakamani kutoa ushahidi wa barua hii ingawa yeye ndo kasaini
Kibatala: Wapi ilielekezwa kwako, muoneshe Hakimu kama kuna sehemu inaonyesha barua hii ilielekezwa kwako
Maxence: Sioni sehemu yoyote kuwa barua iliekezwa kwangu
Kibatala: Kuna shahidi alisema ilipokelewa na wewe binafsi kuhusu mashitaka haya?
Maxence: Hakuna aliyefanya hivyo
(Kibatala narudisha kwa hakimu ushahidi P3)
Kibatala: Wenzetu walikuja na kielelezo P4, msomee Hakimu
Maxence: Ni barua ya Januari 26, 2016 kutoka kwa Victory Attorneys ilisainiwa na Benedict Alex
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Hakimu kama Benedict Alex aliwahi kuitwa kutoa Ushahidi mahakamani
Maxence: Hajawahi
Kibatala: Kuna shahidi aliyesema juu ya huyu shahidi kushindwa kuja mahakamani baada ya kuitwa kutoa Ushahidi?
Maxence: Hakuna aliyekuja kusema hivyo
Kibatala: Ni shahidi yupi alileta uthibitisho kuwa wewe ndiye ulimtuma Benedict ajibu hizi barua?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Na ni shahidi yupi alisema wewe umepata nakala yake?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Kielelezo P6 walileta ushahidi ni barua gani kutoka wapi?
Maxence: Ni barua ya Februari 4, 2016
Kibatala: Aliyeandikiwa hiyo barua ni nani?
Maxence: Aliandikwa Mwanasheria wa Jamii Forums Media. Mimi si mwanasheria wa Jamii Forums Media.
Kibatala: Wapi Hakimu ataona ulipokea kielelelezo au Mwanasheria wa Jamii Forums Media ameshitakiwa?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Imesainiwa na Kagae. Je, alishaitwa kutoa Ushahidi?
Maxence: Sijawahi kumuona
Kibatala: Kielelezo walileta pia in dispatch ya hiyo barua inaonesha barua imeelekezwa kwa nani?
Maxence: Alipokea Advocate Benedict
Kibatala: Aliwahi kuitwa mahakamani kusema amepokea hiyo barua?
Maxence: Sijawahi kumuona
Kibatala: Kuna sahihi (signature) inaonekana kuwa ni ya Benedict kuonesha kama ndiye alipokea barua. Kuna ushahidi uliwahi kuletwa kama uthibitisho kuwa ni sahihi yake?
Maxence: Haijawahi kuletwa
Kibatala: Wewe ndo unashitakiwa. Kwenye hivi vielelezo kuna sehemu wamekuonesha kwenye hizi barua?
Maxence: Hakuna sehemu yoyote
Kibatala: Kielelezo namba P7, Mwambie Hakimu unaona nini
Maxence: Hii ni barua imetoka Victory Attorneys na ni ya Februari 12, 2016. Inaelekezwa kwa Kamishna wa Cyber Crimes Unit na imesainiwa na Benedict Alex.
Kibatala: Kuna shahidi alithibitisha kuwa mliwahi kupata nakala?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Nina maswali matatu, manne matano
1. Mwambie Hakimu kama shahidi wa mwisho toka CRDB alikutaja popote kwenye ushahidi wake
Maxence: Hakunitaja
2. Kuna shahidi alisema una manufaa hadi uzuie uchunguzi?
Maxence: Hakuna
3. Ulikuwa unanufaika na nini hadi uzuie uchunguzi?
Maxence: Sikuwa na interest yoyote, sikuwa na sababu ya kuzuia upelelezi
Kibatala anasema amemaliza
======
Wakili wa Jamhuri anafanya cross-examination:
Wakili Nguka: Unaijua kampuni ya Jamii Forum?
Maxence: Hapana
Nguka: Jamii Media Company Limited?
Maxence: Naifahamu
Jamhuri: Ilisajiliwa lini?
Maxence: Sikumbuki tarehe kamili lakini ilikuwa Juni mwaka 2008
Jamhuri: Nani anasomeka kuwa Mkurugenzi?
Maxence: Nilikuwemo mimi na wenzangu wawili. Tulikuwa wakurugenzi watatu (anataja wengine wawili)
Nguka: Ni lini uligota kuwa Mkurugenzi?
Maxence: Nilipeleka nyaraka BRELA 2012 kujiondoa kuwa Secretary
Nguka: Ulipata nyaraka zozote kukubaliwa?
Maxence: Ndio nyaraka hizo zipo
Nguka: Ulitoa nyaraka mahakamani?
Maxence: Hapana
Nguka: Ni nani anaweza kusajili makampuni?
Maxence: Msajili wa Makampuni
Nguka: Kielelezo P4 naomba unisomee fomu namba 14 A. Nisome Directors hao
Maxence: Inaonesha mimi ni Secretary na Director wa Jamii Media Company Limited mwaka 2008
Nguka: Kusajili na kutumia ni kitu kimoja au viwili?
Maxence: Ni vitu viwili tofauti
Nguka: Shahidi wa kwanza alisema wamesajili na hawatumii
Maxence: Charge sheet ilisema hatukusajili
Nguka: Unakumbuka barua ya tarehe 26 Januari 2016? Je, Barua uliiona?
Maxence: Ndio niliiona hapa mahakamani, kabla ya mahakamani sikuiona popote
Nguka: Kuna barua ilijibiwa?
Maxence: Sijui kwa sababu kuna barua walikuwa wanajibizana. Nliziona mahakamani
Nguka: Umeona nakala za barua?
Maxence: Ndio, nakala ya Jamii Media. Lakini Sijawahi kuipata barua hiyo, niliionea hapa mahakamani
Wakili Nguka: Naishia hapo
Wakili Kibatala anasema hana maswali ya re-examination kwa Maxence. Anaruhusiwa kupisha mshtakiwa wa pili
===
Sasa anaulizwa Maswali Mshitakiwa namba mbili.
(Anaapa)
Kibatala: Katika hati inasomeka Micke William, je ndo jina lako?
Mike: Hapana, mimi naitwa Mike William Mushi. Imeandikwa kwenye cheti cha kuzaliwa hati ya kusafiria, leseni ya Udereva nk (Ametoa kielelezo cha leseni ya udereva kama ushahidi)
Kibatala: Unamkumbuka shahidi Beatrice alisema nini?
Mike: Alisema mimi sihusiki na kesi hii
Kibatala: Beatrice alikuwa anafanya kazi gani?
Mike: Mpelelezi
Kibatala: Ni shahidi gani alikutaja sehemu yoyote au mahali popote?
Mike: Hakuna
Kibatala: Uliwahi kuhusiana na ku-operate au kutumia hiyo website ya JamiiForums.com?
Mike: Sijawahi kusajili wala kutumia domain ya JamiiForums.com
Kibatala: Wewe umewahi kuwa Director wa Jamii Media Company Limited?
Mike: Sijawahi
Wakili Kibatala amemaliza…
Wakili wa Jamhuri anamuuliza Maswali Mike Mushi:
Nguka: Shahidi tusaidie, kabla ya shauri kusikiliza tulisema tunakuja kufanya PH?
Mike: Sina kumbukumbu nzuri
Nguka: Siku ya kwanza ulisomewa hati ya mashitaka Mahakama ilikutamka vizuri?
Mike: Sina kumbukumbu sahihi
Nguka: Mwanzoni hukuona umuhimu wa kuelezea majina yako hapa Mahakamani?
Mike: Kama ambavyo sijui kwanini mimi nipo hapa
Wakili Nguka amemaliza…
(Kibatala anaingia kufanya re-examination)
Kibatala: Wewe umeanza kujitetea lini tangu kesi hii ianze?
Mike: Sasa hivi, ndo siku ya kwanza kuongea hapa Mahakamani
Wakili Kibatala anasema hana maswali zaidi
Hakimu: Mtahitaji kuleta Submissions?
Wote: Ndio
Hakimu: Basi tarehe 21 Septemba 2020 ndo siku ya mwisho kufanya submissions na mention kwa ajili ya hukumu itakuwa siku hiyo hiyo.
Dhamana inaendelea hadi tarehe 21 Septemba 2020.
Kesi namba 458 inayomkabili Mkurugenzi wa Jamii Media, Maxence Melo kutajwa leo
Mara ya mwisho, kesi hii ilisikilizwa Julai 30, 2020
Leo washitakiwa wamejitetea katika kuelekea hitimisho la kesi hii.
Mawakili wa Utetezi Walikuwa ni Peter Kibatala na Jeremiah Mtobesya huku Upande wa Jamhuri akiwa ni Wakili Faraji Nguka
Kibatala ndiye aliyeanza kumuuliza Maswali Maxence Melo mara baada ya kujitambulisha na kula kiapo...
Kibatala: Mwambie Hakimu kama unakumbuka mashitaka
Maxence: Ndio nayakumbuka Mashtaka
Kibatala: Shitaka la kwanza linasema wewe na Mwenzako mlioperate JamiiForums ambayo haijasajiliwa hapa Nchini, Mwambie hakimu kuhusiana na hili
Maxence: Sisi tulikuwa tumesajilia Nchini na tulikuwa tunaitumia
Kibatala: Ni kweli mlikuwa wakurugenzi wawili?
Maxence: Si kweli kwamba tulikuwa wakurugenzi wawili
Kibatala: Wewe ulikuwa na uhusiano gani wa Jamii Media Company Limited?
Maxence: Nilikuwa kama Secretary na Director
Kibatala: Wenzetu walileta ushahidi wa BRELA (P1) barua hiyo inaonesha kwamba ulikuwa Secretary na Director
Maxence: Ni kweli, nilikuwa Secretary na Director wakati tunasajili kampuni.
Kibatala: Je, ni kweli mlisajili?
Maxence: Ni kweli tulisajili tarehe 20 Juni 2008
Kibatala: Wao wanasema hadi kipindi cha mashitaka (2016) ulikuwa Mkurugenzi (Director).
Maxence: Tulifanya mabadiliko, niliandika barua BRELA ya kufanya Mabadiliko ya kujiondoa kuwa Secretary na mabadiliko kwenye ukurugenzi. Siwezi jua nini kipo BRELA kwani nilinyimwa faili niweze kuangalia kama bado wananitambua kama Mkurugenzi au la! Walisema shauri lipo mahakamani hawezi kunipa faili.
Kibatala: Hii Jamii Media kwamba ilioperate bila kusajiliwa na kikoa cha do.tz, kwanza hii Do.tz ni nini?
Maxence: Hakuna kitu kama hicho inatakiwa kuwa (dot tz). Yaani jamiiforums.co.tz au jamiiforums.or.tz. au jamiiforums.ac.tz
Kibatala: Kuna shahidi alikuja kubadilisha kuhusiana hiyo do.tz?
Maxence: Shahidi wa kwanza wa Jamhuri pia alisema walicholeta kwenye hati ya mashitaka sio sahihi. Shahidi huyo alisema tumeshasajili na alisema tulikuwa na domain mbili. Alitoa vielelezo kuthibitisha majina yalikuwa yamesajiliwa. Alikuwa anaongoza in-chief na yeye ndo alikuwa Msajili wa vikoa.
Kibatala: Vipi kuhusu kutumia kikoa?
Maxence: Tulisajili domain mbili alikuja nazo shahidi. D1 iliyoingizwa kama kielelezo na kinaonesha tulisajili domain mbili, www.jamiiforums.co.tz na www.jf.co.tz
Kibatala: Wanasema hamtumii ni kweli?
Maxence: Tunatumia domain zote mbili na zimesajiliwa. Ikiwezekana mtu yeyote azitembelee aone kama zinafunguka
Kibatala: Unaposema tutembelea unamaanisha nini?
Maxence: Ukitembelea Domain hizo zinafanya kazi. Mtu yoyote anaweza kutumia simu au kifaa chochote cha kidijitali chenye mfumo wa intaneti kuangalia kama zinafanya kazi.
Kibatala: PW1 wakati anaulizwa maswali na wakili Tundu Lissu baadae mimi, alisemaje?
Maxence: PW1 alikiri mwaka 2009 alishirikiana na mimi kuhamasisha watanzania kusajili kikoa cha .tz. Shahidi huyo alisema haikuwa lazima kutumia bali ilikuwa ni kuhamasisha uzalendo
Kibatala: Wewe na mwenzako hamkutoa ushirikiano kwa Polisi. Unasemaje kuhusiana na kuzuia upelelezi?
Maxence: Mimi sijazuia upelelezi
Kibatala: Wenzetu walitoa vielelezo vya barua kwamba barua hii ndo msingi wa wao kwa Polisi kutoa Ushirikiano. Mwambie Hakimu kuhusu hii barua ya Januari 26, 2016 imekuwa addressed kwa nani na ilitoka wapi?
Maxence: Ilitoka Wizara ya Mambo ya Ndani, Cyber Crimes Unit. Ilielekezwa kwa Mwanasheria wa Jamii Forums Media.
Kibatala: Mwambie mheshimiwa Hakimu kama wewe ni Mwanasheria
Maxence: Mimi sio Mwanasheria
Kibatala: Kuna Shahidi alisema wewe ni Mwanasheria?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Jamii Forums Media ni kitu gani?
Maxence: Sijui
Kibatala: Taasisi zilizozungumziwa na mashahidi wote ni zipi?
Maxence: Mashahidi walikuwa wanazungumzia Jamii Media Company Limited na wengine Jamii Forum
Kibatala: Hii barua imesainiwa na nani?
Maxence: Imesainiwa na Joshua Mwangasa – ASP
Kibatala: Joshua Mwangasa alishawahi kutoa ushahidi?
Maxence: Hajawahi kuja mahakamani kutoa ushahidi wa barua hii ingawa yeye ndo kasaini
Kibatala: Wapi ilielekezwa kwako, muoneshe Hakimu kama kuna sehemu inaonyesha barua hii ilielekezwa kwako
Maxence: Sioni sehemu yoyote kuwa barua iliekezwa kwangu
Kibatala: Kuna shahidi alisema ilipokelewa na wewe binafsi kuhusu mashitaka haya?
Maxence: Hakuna aliyefanya hivyo
(Kibatala narudisha kwa hakimu ushahidi P3)
Kibatala: Wenzetu walikuja na kielelezo P4, msomee Hakimu
Maxence: Ni barua ya Januari 26, 2016 kutoka kwa Victory Attorneys ilisainiwa na Benedict Alex
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Hakimu kama Benedict Alex aliwahi kuitwa kutoa Ushahidi mahakamani
Maxence: Hajawahi
Kibatala: Kuna shahidi aliyesema juu ya huyu shahidi kushindwa kuja mahakamani baada ya kuitwa kutoa Ushahidi?
Maxence: Hakuna aliyekuja kusema hivyo
Kibatala: Ni shahidi yupi alileta uthibitisho kuwa wewe ndiye ulimtuma Benedict ajibu hizi barua?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Na ni shahidi yupi alisema wewe umepata nakala yake?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Kielelezo P6 walileta ushahidi ni barua gani kutoka wapi?
Maxence: Ni barua ya Februari 4, 2016
Kibatala: Aliyeandikiwa hiyo barua ni nani?
Maxence: Aliandikwa Mwanasheria wa Jamii Forums Media. Mimi si mwanasheria wa Jamii Forums Media.
Kibatala: Wapi Hakimu ataona ulipokea kielelelezo au Mwanasheria wa Jamii Forums Media ameshitakiwa?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Imesainiwa na Kagae. Je, alishaitwa kutoa Ushahidi?
Maxence: Sijawahi kumuona
Kibatala: Kielelezo walileta pia in dispatch ya hiyo barua inaonesha barua imeelekezwa kwa nani?
Maxence: Alipokea Advocate Benedict
Kibatala: Aliwahi kuitwa mahakamani kusema amepokea hiyo barua?
Maxence: Sijawahi kumuona
Kibatala: Kuna sahihi (signature) inaonekana kuwa ni ya Benedict kuonesha kama ndiye alipokea barua. Kuna ushahidi uliwahi kuletwa kama uthibitisho kuwa ni sahihi yake?
Maxence: Haijawahi kuletwa
Kibatala: Wewe ndo unashitakiwa. Kwenye hivi vielelezo kuna sehemu wamekuonesha kwenye hizi barua?
Maxence: Hakuna sehemu yoyote
Kibatala: Kielelezo namba P7, Mwambie Hakimu unaona nini
Maxence: Hii ni barua imetoka Victory Attorneys na ni ya Februari 12, 2016. Inaelekezwa kwa Kamishna wa Cyber Crimes Unit na imesainiwa na Benedict Alex.
Kibatala: Kuna shahidi alithibitisha kuwa mliwahi kupata nakala?
Maxence: Hakuna
Kibatala: Nina maswali matatu, manne matano
1. Mwambie Hakimu kama shahidi wa mwisho toka CRDB alikutaja popote kwenye ushahidi wake
Maxence: Hakunitaja
2. Kuna shahidi alisema una manufaa hadi uzuie uchunguzi?
Maxence: Hakuna
3. Ulikuwa unanufaika na nini hadi uzuie uchunguzi?
Maxence: Sikuwa na interest yoyote, sikuwa na sababu ya kuzuia upelelezi
Kibatala anasema amemaliza
======
Wakili wa Jamhuri anafanya cross-examination:
Wakili Nguka: Unaijua kampuni ya Jamii Forum?
Maxence: Hapana
Nguka: Jamii Media Company Limited?
Maxence: Naifahamu
Jamhuri: Ilisajiliwa lini?
Maxence: Sikumbuki tarehe kamili lakini ilikuwa Juni mwaka 2008
Jamhuri: Nani anasomeka kuwa Mkurugenzi?
Maxence: Nilikuwemo mimi na wenzangu wawili. Tulikuwa wakurugenzi watatu (anataja wengine wawili)
Nguka: Ni lini uligota kuwa Mkurugenzi?
Maxence: Nilipeleka nyaraka BRELA 2012 kujiondoa kuwa Secretary
Nguka: Ulipata nyaraka zozote kukubaliwa?
Maxence: Ndio nyaraka hizo zipo
Nguka: Ulitoa nyaraka mahakamani?
Maxence: Hapana
Nguka: Ni nani anaweza kusajili makampuni?
Maxence: Msajili wa Makampuni
Nguka: Kielelezo P4 naomba unisomee fomu namba 14 A. Nisome Directors hao
Maxence: Inaonesha mimi ni Secretary na Director wa Jamii Media Company Limited mwaka 2008
Nguka: Kusajili na kutumia ni kitu kimoja au viwili?
Maxence: Ni vitu viwili tofauti
Nguka: Shahidi wa kwanza alisema wamesajili na hawatumii
Maxence: Charge sheet ilisema hatukusajili
Nguka: Unakumbuka barua ya tarehe 26 Januari 2016? Je, Barua uliiona?
Maxence: Ndio niliiona hapa mahakamani, kabla ya mahakamani sikuiona popote
Nguka: Kuna barua ilijibiwa?
Maxence: Sijui kwa sababu kuna barua walikuwa wanajibizana. Nliziona mahakamani
Nguka: Umeona nakala za barua?
Maxence: Ndio, nakala ya Jamii Media. Lakini Sijawahi kuipata barua hiyo, niliionea hapa mahakamani
Wakili Nguka: Naishia hapo
Wakili Kibatala anasema hana maswali ya re-examination kwa Maxence. Anaruhusiwa kupisha mshtakiwa wa pili
===
Sasa anaulizwa Maswali Mshitakiwa namba mbili.
(Anaapa)
Kibatala: Katika hati inasomeka Micke William, je ndo jina lako?
Mike: Hapana, mimi naitwa Mike William Mushi. Imeandikwa kwenye cheti cha kuzaliwa hati ya kusafiria, leseni ya Udereva nk (Ametoa kielelezo cha leseni ya udereva kama ushahidi)
Kibatala: Unamkumbuka shahidi Beatrice alisema nini?
Mike: Alisema mimi sihusiki na kesi hii
Kibatala: Beatrice alikuwa anafanya kazi gani?
Mike: Mpelelezi
Kibatala: Ni shahidi gani alikutaja sehemu yoyote au mahali popote?
Mike: Hakuna
Kibatala: Uliwahi kuhusiana na ku-operate au kutumia hiyo website ya JamiiForums.com?
Mike: Sijawahi kusajili wala kutumia domain ya JamiiForums.com
Kibatala: Wewe umewahi kuwa Director wa Jamii Media Company Limited?
Mike: Sijawahi
Wakili Kibatala amemaliza…
Wakili wa Jamhuri anamuuliza Maswali Mike Mushi:
Nguka: Shahidi tusaidie, kabla ya shauri kusikiliza tulisema tunakuja kufanya PH?
Mike: Sina kumbukumbu nzuri
Nguka: Siku ya kwanza ulisomewa hati ya mashitaka Mahakama ilikutamka vizuri?
Mike: Sina kumbukumbu sahihi
Nguka: Mwanzoni hukuona umuhimu wa kuelezea majina yako hapa Mahakamani?
Mike: Kama ambavyo sijui kwanini mimi nipo hapa
Wakili Nguka amemaliza…
(Kibatala anaingia kufanya re-examination)
Kibatala: Wewe umeanza kujitetea lini tangu kesi hii ianze?
Mike: Sasa hivi, ndo siku ya kwanza kuongea hapa Mahakamani
Wakili Kibatala anasema hana maswali zaidi
Hakimu: Mtahitaji kuleta Submissions?
Wote: Ndio
Hakimu: Basi tarehe 21 Septemba 2020 ndo siku ya mwisho kufanya submissions na mention kwa ajili ya hukumu itakuwa siku hiyo hiyo.
Dhamana inaendelea hadi tarehe 21 Septemba 2020.
Kesi namba 458 inayomkabili Mkurugenzi wa Jamii Media, Maxence Melo kutajwa leo