Kero ya Rais kutumia barabara

Kero ya Rais kutumia barabara

Kuna watu hua wanazungumzia kwamba mhe rais anabana matumizi kwa kusafiri kutumia barabara, ni kweli pesa imebanywa (kwa assumption) lakini watu hawafikirii hasara ya pesa inayopatikana kwa raia kumsubiri raisi apite. Fikiria mfanyabiashara wa mabasi (kwa mfano Abood bus service) ikimtokea namna hiyo basi lake haliwezi kupiga idadi ya roots zile zile from Moro to Dar, na hatuna uhakika kama basi hilo lina mkopo wa CRDB au vipi. Usafiri wa ndege ni kweli wa gharama lakini ni wa haraka, akitoka Dodoma anaweza kwenda straight Ikulu na kuendelea na kazi but kwa gari already anakua kachoka.
 
Hili ni tatizo sababu kila mtu anataka kuwahi mambo yake ili isiwe kero basi uwekwe utaratibu wa kupishana kama wananchi wa kawaida kuepusha usumbufu kwa wadharauliwa dhidi mheshimiwa
 
Mleta mada muongo na mpuuzi mimi ni askari mtu hawezi simamishwa wakati msafala upo gairo jamaa muongo halafu mpuuzi.

Khaaaa wewe ni askari?? Mbona unakesha humu JF? Unaongoza magari saa ngapi?
 
Kwa Tz kusimamisha hata saa tatu si tatizo kwani trafic wetu wanaogopa kuhamishwahivyo hawatumii elimu yao kufanya kazi zao kwa weledi
 
Huu kwa kweli ni usumbufu kwa raia wema! Kuna sababu gani ya kutumia barabara na kusababisha raia waweke magari yao pembeni kupisha msafara wa Rais? Huu ni usumbufu uliopita kipimo! Hebu atumie ndege zake bwana! Sasa hivi tumesimamishwa hapa Chalinze eti tunapisha msafara ambao bado uko Gairo! Sasa fikria muda ambao raia watautumia mpaka apite hapa Chalinze! "HAPA MAIGIZO TU"

Kweli kabisa mkuu ni kero na hiyo ni kutafuta sifa za muda
 
Mleta mada muongo na mpuuzi mimi ni askari mtu hawezi simamishwa wakati msafala upo gairo jamaa muongo halafu mpuuzi.

Wacha ubishi wa kijiweni, twambie ni km ngapi wakati rais anatakiwa apite ndio magari yanawekwa pembeni
 
Mleta mada muongo na mpuuzi mimi ni askari mtu hawezi simamishwa wakati msafala upo gairo jamaa muongo halafu mpuuzi.
Mleta mada ana mchango wa pekee kiasi cha kutufanya tujue kuwa wewe ni askari tena polisi!
 
Nafikiri siyo salama kutumia Barbara muda mrefu kwa kiongozi mkuu wa nchi. Mimi naona barabara ina hatari nyingi kuliko ndege!
 
Mleta mada muongo na mpuuzi mimi ni askari mtu hawezi simamishwa wakati msafala upo gairo jamaa muongo halafu mpuuzi.

Kwa hiyo ukiwa askari ndo tukuamini?humu jf hatuchangii kwa vyeo wala nyadhifa.Toa data tembea.

Halafu kuna mtu humu jf aliwahi kuleta mada ikiuliza"hivi kuna askarikoko? Nilishangaa sasa km vile...
 
sasa atakuwa anaenda aje kwenye mikutano ya UN ambayo itafanyika outside East Africa?
Ataenda kwa gari. Hata mikutano ya UN, New york, itabidi aende kwa gari. Pia kwa sababu hiyo gharama zitapungua. Huyu kweli "anafaa".
 
Back
Top Bottom