A
Anonymous
Guest
Fichua uovu: Uyole, jimbo jipya la Tulia.
Nimefanya malipo ya kuunganishiwa huduma ya maji safi tangu mwezi wa nne, lakini hadi leo sijapatiwa huduma hiyo. Kila ninapofuatilia, naambiwa vifaa bado havijapatikana, niwasubiri hadi vitakapokuja.
Kinachoniumiza ni kwamba ninatumia gharama kubwa kununua maji kila siku, ilhali mtaani ninaona mabomba yakivuja ovyo bila kurekebishwa wala kuchukuliwa hatua. Inazua maswali: je, kweli vifaa havipo, au kuna mchezo unaendelea?
Naomba suala hili lipatiwe ufumbuzi na sauti ya wananchi isikilizwe, kwani hali hii imekuwa ni mzigo mkubwa kwa maisha yetu ya kila siku.