Kama jumamosi na jumapili hawafanyi kazi basi waweke mitambo yao kama startime ukilipia automatical kinafungua. Yaani nilifura kwa hasira kushindwa kumwona sumaye. Nimerudi startime bila kutaka.
Ni mara ya ngapi umepata shida wakati unalipia?? Hebu soma hii kisha kama una swali niulize.
Piga *150*50*5# KABLA YA KUFANYA MALIPO. Unaweza kutumia Airtel, Tigo, Vodacom au Zantel.
-
Kabla hujafanya malipo, piga namba *150*50*5#, chagua kifurushi unachotaka na chagua kama unataka kubadili kifurushi sasa hivi. Baada ya hapo, sasa unaweza kufanya malipo kama kawaida kupitia mitandao ya simu au kwa wakala wa AzamTV, Selcom, MaxMalipo au Buttonpay.
-
Kama ulishafanya malipo zaidi ya siku mbili zilizopita na ungependa kubadili kifurushi, angalia salio kwanza, kisha lipia upya kifurushi unachotaka. Kisha piga namba *150*50*5# na chagua kama unataka kubadili kifurushi sasa hivi au baada ya kifurushi cha sasa kuisha.
-
Kuangalia salio piga *150*50*5# na chagua kuangalia salio
Kusajili huduma mpya, piga *150*50*5#, na chagua sajili huduma mpya.
-
Mfano wa 1 jinsi ya kutumia code:
Kama una kirufushi cha 12,000 kilichoisha muda wake na unataka kupata cha 20,000. Piga *150*50*5# Kabla ya kufanya malipo. Chagua kubadili kifurushi sasa hivi na chagua Azam Plus ya 20,000. Utatumiwa ujumbe ombi limefanikiwa. Baada ya hapo, fanya malipo. Malipo yakiingia kwenye akaunti yako, kifurushi kitabadilishwa baada ya dakika 5. Hakikisha umewasha kingamuzi chako.
Ukifanya kinyume na hivi, yaani ukalipia kwanza, kifurushi chako cha zamani kitafunguliwa hata ukilipa 20,000.