Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 13,343
- 20,797
Waziri wa mambo ya nje wa Kenya Bibi Amina Mohamed anayetembelea nchini amempongeza JK kwa hotuba yake aliyoitoa bungeni wiki hii na hasa tamko lake la Tanzania kutojitoa katika EAC.
Bibi Amina amekuja nchini pamoja na mambo mengine kujadili uhusiano baina ya nchi zetu na pia mtafaruku uliojitokeza katika uhusiano wa nchi zilizomo katika EAC.
Wana JF:
Je hatua ya Amina kuja nchini ni sehemu ya juhudi za kidiplomasia zinazochukuliwa na Kenya ili kurejesha mtengamano wa EAC?
Bibi Amina amekuja nchini pamoja na mambo mengine kujadili uhusiano baina ya nchi zetu na pia mtafaruku uliojitokeza katika uhusiano wa nchi zilizomo katika EAC.
Wana JF:
Je hatua ya Amina kuja nchini ni sehemu ya juhudi za kidiplomasia zinazochukuliwa na Kenya ili kurejesha mtengamano wa EAC?
Kwa upande wake, Kenya moja ya nchi waanzilishi wa Jumuia ya Afrika Mashariki na ambayo ilishutumiwa kushiriki kuibagua Tanzania, imemtuma waziri wake wa mambo ya nje, Amina Mohammed kwenda Tanzania na kuwa na mazungumzo na waziri mwenzie wa mambo ya nje Bernard Membe kuhusu mfarakano huo na nia ya kuimarisha zaidi uhusiano wa nchi mbili hizo.
Katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Jumapili, waziri Amina Mohammed, amesema Kenya inaunga mkono hotuba ya Rais Jakaya Kikwete, kuhusu uamuzi wake wa kutojitoa katika Jumuia ya Afrika Mashariki, huku akisisitiza kuwa bila Tanzania hakuna Afrika Mashariki na bila Afrika Mashariki hakuna Tanzania.
"Kama unavyojua Kenya na Tanzania tumekuwa tukiijenga jumuiya ya Afrika Mashariki kwa muda mrefu sana, tuko na mafanikio mengi sana, kuna mambo mengi tumeyafanya, kuna njia ndefu imebakia kuna mambo mengi yasiyoweza kupimwa kati ya nchi hizi. Na tuna tumaini kwamba tutaendelea kuijenga Afrika Mashriki kwa nguvu zote na tutawasiliana na watu wetu kwa sababu tunataka watu wetu waishi vema na wawe majirani wazuri na waendelee . Kwa Tunataka uchumi wetu uende vizuri. Kwa hiyo tutaendelea kushirikiana, sisi ni wale wa kwanza tuliokuwa pale kwa hiyo tunataka tufanye kile tunachoweza kuendeleza Afrika Mashariki..... Lakini tumefurahia sana sana hotuba ya Rais aliyotoa pale bungeni na tunawashukuru pia Watanzania kumuunga mkono."
Uhusiano wa Kenya na Tanzania ni wa kindugu
Pia waziri Amina amesisitiza kuwa hakuna namna ambavyo Tanzania na Kenya zitatenganishwa, kwa namna ambavyo zimejenga maingiliano makubwa ya kijamii na kiuchumi, huku akiomba Tanzania kusaidia kusukuma ombi la Kenya la kutaka kesi ianyomkabili Rais wake, Uhuru Kenyatta iahirishwe kwa mwaka mmoja zaidi ili kumpa fursa ya kutekeleza majukumu yake ya kitaifa.
Kwa upande wake waziri wa mambo ya nje wa Tanzania, Benard Membe amesema serikali yake imefurahi kuona Kenya imekuwa nchi ya kwanza kuipongeza Tanzania kwa kuinusuru jumuia ya Afrika Mashariki kama ilivyokuwa mwanzoni na kujenga jumuiya ya watu na si ya viongozi, na kuahidi kushirikiana na Kenya katika masuala mbalimbali likiwemo la kutaka kesi inayomkabili Rais Uhuru Kenyatta katika mahakama ya ICC iahirishwe kwa mwaka mmoja zaidi.
Waziri Membe amesema waziri mwenzake Amina kutoka Kenya amesema hotuba ya Rais Kikwete imewazindua kwani hawakujua kuwa baadhi ya yale waliyokuwa wakiyafanya yalikuwa ni kukiuka taratibu za Jumuia ya Afrika Mashariki na kuahidi kuwa Kenya itashirikiana kikamilifu na nchi waanzilishi halisi wa Jumuia ya Afrika Mashariki.
Katika kuonyesha nia thabiti ya kutotoka katika Jumuia ya Afrika Mashariki, Rais Kikwete katika hotuba yake aliyoitoa bungeni, alisema "Tanzania ni mwanachama mvumilivu, mtiifu na mwaminifu na tunatimiza wajibu wetu kwa jumuia na kuhusika kikamilifu katika ujenzi wake."alisema.
Chini ni Link ya Habari hiyo
BBC Swahili - Habari - Kenya yaiunga mkono Tz A.Mashariki