Kenya itaanza kujenga kinu cha nyuklia mnamo mwaka wa 2027.

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,502
9,282
Kenya itaanza kujenga kinu cha nyuklia mnamo mwaka wa 2027.

Kinu cha nyuklia cha Megawati 1,000 ni sehemu ya mpango wa nchi kuhamia kwa nishati safi na kuongeza uzalishaji wa kawi.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Nishati ya Nyuklia Justus Wabuyabo aliliambia gazeti la Business Daily la Kenya kwamba shirika hilo kwa sasa linafanya tathmini ya eneo na kukamilisha maandalizi ya kufungua zabuni za ujenzi wa kiwanda hicho.

Bw Wabuyabo alisema kuwa kiwanda hicho kitajengwa katika eneo la pwani ya Kenya kwa muda wa miaka sita hadi kumi, huku mtambo wa kwanza ukianza kufanya kazi mwaka wa 2034 .

Baadhi ya Wakenya wamekosoa mpango huo wakidai kuwa kiwanda cha nyuklia si cha lazima na Kenya haina uwezo wa kushughulikia taka za nyuklia.

"Tuna rasilimali za kutosha za umeme wa maji, jotoardhi, jua na upepo.Mbaya zaidi, sidhani kama tuna uwezo wa kuhakikisha usalama wa kinu cha nyuklia au kusafisha janga linapotokea," mtumiaji wa Twitter alisema.

Kwa sasa, Afrika Kusini ndiyo nchi pekee ya Afrika inayozalisha nishati ya nyuklia kibiashara.

Baadhi ya mataifa mengine ya Afrika yameanza mipango ya kupitisha nishati ya nyuklia, ikiwa ni pamoja na Rwanda na Misri, ambayo kwa sasa inajenga kinu cha nyuklia cha $30bn (£24bn).


BBC
 
Back
Top Bottom