Muhimbili imesomesha madakatari hadi mabingwa wa mabingwa tangu tupate uhuru, mbona haina kasoro hizo?
Huo ni uzembe tu wa KCMC. Yaani unataka kutuambia kuwa ni sawa tu wagonjwa wafie mikononi mwa wanafunzi bila kutibiwa na wataalamu eti kisa nini? Kuna faida gani kuua mtu ili mwingine asome, huo ndio utaratibu?
KCMC imekuwa hospitali mbaya sana, ningeshauri hata ile "C" inayomaanisha "Christian" kwenye jina lake waiondoe waweke kitu kingine hata "Criminal" au "Cruel". Yesu Kristo asingekubali uzembe ule angewafurumusha hata kwa mangumi kama alivyofukuza wacheza kamari hekaluni. Hospitali imekuwa pango la kifo!