Ralph Tyler
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 2,842
- 3,618
Wanapaita hospitali ya rufaa lakini vifo nje nje! Ukifika pale kwanza kasheshe ni jinsi ya kuingia ndani, mizinguo inaanza getini. Ukipenya geti ukafika ndani unakutana na foleni ya balaa, foleni kila mahali na haitembei! Na kila hatua kuna wanafunzi lukuki, ukidhani sasa ndio unatibiwa unakuta ni mwanafunzi anakupotezea muda weeeee halafu anakupasia kwa mwanafunzi mwingine unapapaswa unachokonolewa weeeee halafu unafaulishwa kwa mwanafunzi mwingine hivyohivyo hadi watosheke, hawajali maumivu yako. Wagonjwa wengi sana wamefia mikononi mwa wanafunzi. Ukitoboa hapo kwa wanafunzi (hapo utakuwa umeshasota foleni masaa!) kama ni wa kulazwa ni kilio upyaaaa! Tatizo linaanzia kwenye ile machela ya kukupeleka wodini, utaisubiri masaa! Ikipatikana anatafutwa wa kukupeleka, masaa! Akipatikana anakukokota kama mzigo hadi wodini, hapo utawekwa kwenye korido masaa! Kisha wanaingia kundi lingine la wanafunzi wanakuanza upyaaaa! Usife kwanini? Watu wakachunguze ile hospitali ni balaa! Mtu anaweza kulazwa asubuhi akaanza kutibiwa usiku au hata kesho yake! Kama mtu umekodi gari ikuwahishe hospitali ya rufaa unajiuliza mara mbili ulikuwa unaharakisha nini? Hii ni jipu kabisa inatakiwa itumbuliwe harakaaaa!
Muhimbili imesomesha madakatari hadi mabingwa wa mabingwa tangu tupate uhuru, mbona haina kasoro hizo?Madaktari wooooooooote unaowaona hapo, walianza hivyo hivyo kama wanafunzi. Bila madaktari wanafunzi wa leo hakuna madaktari bingwa wa kesho. Elewa hivyo. Daktari wa binadamu anajifunza kwa binadamu mgonjwa jinsi ya kutibu.
Vipimo hata vya palepale mgonjwa anavyozungushwa ni huzuni tupu. Nenda na kadi ya bima uandikiwe kipimo cha kawaida tu cha ultrasound. Utazungushwa kutwa nzima ili kupata tu booking, siyo kipimo! Urasimu wao hata gerezani kuna nafuu!Yote umesema kweli nilimpeleka mgonjwa wakatoa tarehe ya vipimo tukaenda siku ya vipimo majibu wakaturusha miezi mitatu ndio tukachukue sasa jiulize mtu atatumia dawa gani hapo kati? Yaani wanarahisisha sana kifo nije nje.
Labda ni huko macho pengine kuna nafuu, japo sina uhakika. Ulizia kwengine kote ni uozo mtupu.Labda tatizo ni wagonjwa wanaolazwa!
Mie mbona baba yangu mzazi anatabiwa hapo tatizo la pressure ya macho lakini anahudumiwa fasta sijamsikia akilalamika!
Muhimbili imesomesha madakatari hadi mabingwa wa mabingwa tangu tupate uhuru, mbona haina kasoro hizo?
Huo ni uzembe tu wa KCMC. Yaani unataka kutuambia kuwa ni sawa tu wagonjwa wafie mikononi mwa wanafunzi bila kutibiwa na wataalamu eti kisa nini? Kuna faida gani kuua mtu ili mwingine asome, huo ndio utaratibu?
KCMC imekuwa hospitali mbaya sana, ningeshauri hata ile "C" inayomaanisha "Christian" kwenye jina lake waiondoe waweke kitu kingine hata "Criminal" au "Cruel". Yesu Kristo asingekubali uzembe ule angewafurumusha hata kwa mangumi kama alivyofukuza wacheza kamari hekaluni. Hospitali imekuwa pango la kifo!
Kwahiyo hata huko mkiwa wanafunzi mlikuwa mnachezea wagonjwa kwa zamu bila kujali maumivu yao, na tena mkiwa bila mwalimu wa kuwasimamia na kuhakikisha usalama wa mgonjwa?Acha kudanganya watu. Nimesoma Muhimbili mimi...
Kwahiyo hata huko mkiwa wanafunzi mlikuwa mnachezea wagonjwa kwa zamu bila kujali maumivu yao, na tena mkiwa bila mwalimu wa kuwasimamia na kuhakikisha usalama wa mgonjwa?
Kwahiyo na nyie pia ni majipu?
Muhimbili mwanafunzi hatibu hata siku Mojaaaa anachukua tu patient history na kupropose ugonjwa na treatment...!! Japo wengine huperform procedure zinazokuwa proposed na Dr ambazo ni very minor..Ulitaka kudanganya kuwa Muhimbili ni tofauti. Shule yoyote ya madaktari ndio utaratibu wake. Mwanafunzi anachukuwa story ya mgonjwa, anaiwasilisha kwa mwalimu wake. Mwalimu wake anamfundisha na kumsahihisha. Mwishoe mgonjwa anakuwa kama ameonwa na mwalimu kwa sababu matibabu ya mwisho yatakayotolewa ni yale ya mwalimu, siyo ya mwanafunzi. Mwanafunzi wa udaktari wa binadamu anajifunzia kwa binadamu. Kama hautaki kupitia kwa mwanafunzi, nenda hospitali ndogo ama vituo vya afya.
Muhimbili mwanafunzi hatibu hata siku Mojaaaa anachukua tu patient history na kupropose ugonjwa na treatment...!! Japo wengine huperform procedure zinazokuwa proposed na Dr ambazo ni very minor..
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Samahani Chief mnaendeleaje hapo Muhimbili...!!Unajiona mjanjaaaaaaaaaa.... Kwani nimeandika nini mimi?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Samahani Chief mnaendeleaje hapo Muhimbili...!!
Rudia tena nilichosema kuhusu KCMC utaona ni tofauti.Ulitaka kudanganya kuwa Muhimbili ni tofauti. Shule yoyote ya madaktari ndio utaratibu wake. Mwanafunzi anachukuwa story ya mgonjwa, anaiwaslilisha kwa mwalimu wake. Mwalimu wake anamfundisha na kumsahihisha. Mwishoe mgonjwa anakuwa kama ameonwa na mwalimu kwa sababu matibabu ya mwisho yatakayotolewa ni yale ya mwalimu. Siyo ya mwanafunzi. Mwanafunzi wa udaktari wa binadamu anajifunzia kwa binadamu. Kama hautaki kupitia kwa mwanafunzi, nenda hospitali ndogo ama vituo vya afya.