Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 464
- 687
Leo nataka niwashukuru kipekee walimu wangu walionipa heshima ya kuitwa daktari, chuo kikuu cha udaktari KCMC na CUHAS Bugando, hivi vyuo ni vyuo bora kabisa vya udaktari, nikiwa alumni wa vyuo hivi nasimama kama ushuhuda wa kazi nzuri wanayoifanya kwa maslahi ya nchi yetu.
Sitaweza kuacha kuwakumbuka na kutangaza ubora za mafunzo mliyonifunza walimu wangu. KCMC na CUHAS ni alama kubwa katika historia ya uwekezaji katika elimu ya Tiba uliofanywa na na kanisa la Katoliki na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania. Mm binafsi nawapongeza sana Askofu Pissa, rais wa baraza la maaskofu Tanzania na Askofu Malasusa kwa kazi nzuri zenye matokeo yanayoonekana.
Kanisa ni tumaini la watanzania, maaskofu wetu tunawategemea kuwa tumaini mahali pasipo na tumaini. Tusaidieni kuiangazia nuru nchi yetu.
Ahsanteni sana baba maaskofu wangu. Mungu awabariki sana
Sitaweza kuacha kuwakumbuka na kutangaza ubora za mafunzo mliyonifunza walimu wangu. KCMC na CUHAS ni alama kubwa katika historia ya uwekezaji katika elimu ya Tiba uliofanywa na na kanisa la Katoliki na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania. Mm binafsi nawapongeza sana Askofu Pissa, rais wa baraza la maaskofu Tanzania na Askofu Malasusa kwa kazi nzuri zenye matokeo yanayoonekana.
Kanisa ni tumaini la watanzania, maaskofu wetu tunawategemea kuwa tumaini mahali pasipo na tumaini. Tusaidieni kuiangazia nuru nchi yetu.
Ahsanteni sana baba maaskofu wangu. Mungu awabariki sana