Jamani naombeni mnifahamishe maana mie nasikia kuwa huko ughaibuni yaani USA na Ulaya watu wengi wanafanya kazi za kubeba box na zinapondwa sana bongo. Sasa huwa najiuliza ndio kazi gani hizo? anayefahamu please nifahamisheni mwenzenu.
kupanga mabox ya sabuni au soda shaw's au stop and shop, au new york hakuna shaw's?
bongo majungu mengi.
Kitu muhimu kuhusu hizi kazi za box, zifanywe huku ukialia mbele na kukumbuka nyumbani, maana ukizifanya kwa miaka mingi bila malengo, unafikia wakata akili inagota, umri unapanda mpaka unafika mahali box haibebeki tena na kujikuta huna jingine uliwezalo.
Mimi mwenyewe sio box tuu nimebeba bali mpaka zege huko ughaibuni. Kuna wenzetu wengi wamewin na sasa maisha ni mazuri, kila mwaka likizo ni Bongo na maendeleo kwa kwenda mbele. Pia kuna wenzetu wamerost, Bongo ni kituo cha polisi, hata ikitokea shida home, nauli ni issue.
'Kazi ni kazi bora mkono uende kinywani'
.
wabeba mabox wengi kwa standard za bongo ni sawa au zaidi ya watu wenye white collar jobs
Kazi zimegawanyika katika mafungu matatu
1. Skilled - ni kazi ambayo uwezi kufanya mpaka uwe mjuzi, au unatumia uwezo wako wa shule ie doctor, engineer......
2. Semi skilled - hii mara nyingi inatokana na mfanyakazi kufanya kazi mda mrefu katika sehemu na kujua kazi ambazo skilled wanafanya na kuaminika na kuwa anafanya hizo kazi, pia kuna kazi zinahitaji ujuzi lakini sio wahali ya juu.
3. Unskilled (maboxi) - kazi zote ambazo mtu anaweza kufundishwa leo kesho akaanza kufanya mwenyewe haziitaji shule. Cashier dukani benki popote pale, kazi za viwandani lakini sio maengineer, kazi za kwenye maghala, udereva, kuongea na simu.
Kuna kazi kama receptionist, kuongea na simu, cashier watu wanapenda kuziita semi skilled ili kujipandisha chati lakini ni unskilled job.
Kwa mfano tz kazi za mabox - dahaco, bandarini, breweries, receptionist, dereva.
Watu wanaweza kuanza na kazi za maboxi na wakatajiria. Muuza duka anaweza kuanza kuuza duka mpaka na yeye akawa na duka lake. Dereva wa pizza anaweza baadae akawa na duka lake.
Mimi wakati nasoma nilikua nafanya kazi part-time pizzahut na mwenye pizza hut yetu alianza kuwa dereva na sasa hivi ana franchise tano za pizzahut.
Na mimi hiyo kazi ya maboxi imenisomesha, kuna watu wamejenga wengi tu kwa hiyo inategemea na wewe unatumiaje hiyo hela yako.
Mfano madereva wa magari ya mafuta tanker wanapata £40,000 hii ni zaidi ya skilled job nyingi tu.
Jamani naombeni mnifahamishe maana mie nasikia kuwa huko ughaibuni yaani USA na Ulaya watu wengi wanafanya kazi za kubeba box na zinapondwa sana bongo. Sasa huwa najiuliza ndio kazi gani hizo? anayefahamu please nifahamisheni mwenzenu.