Kauli za Rais Magufuli na mustakabali wa Taifa letu

Kauli za namna hii zinaakisi kile alichokisema Sugu kuwa serikali inaongozwa kwa mizuka.Serikali inayosimamia mfumo wa Elimu unaozalisha vilaza haina na haiwezi kuwa na sababu za kuwanyanyapaa vijana wetu waliosoma kupitia mfumo wa serikali unaozalisha vilaza.

Ukilaza ni matokeo ya mfumo wetu wa Elimu ulioshindwa kutoa Elimu bora,badala yake umejikita katika kuongeza maelfu ya vijana wasio na sifa za kielimu.


Angalia matokeo ya kidato cha nne 2015, kisha tumuulize Rais,vilaza hao ni zao la nani kama si serikali yake mwenyewe?



Screenshot_2016-06-03-19-37-23.png



Ikiwa wengi wa wanafunzi wanaomaliza secondary hufeli,nani anayepaswa kulaumiwa kwa matokeo hayo mabovu ya vijana wetu? Ukilaza ni matokeo ya Sera yetu ya Elimu iliyoshindwa kutatua changamoto za utoaji wa Elimu,hivyo anapotokea kiongozi Mwenye mamlaka ya kusimamia Sera,akaanza kutoa dhihaka kwa wananchi wake kwa kuwaita vilaza,kiongozi huyo anakuwa ni kielelezo cha viongozi kushindwa kutumia madaraka yao na dhamana zao kwa ajili ya Taifa letu.
 
SUALA SIO KUDHARAULIWA BALI NI KUWA TUNAHUDUMIWA NA WATU WENYE ELIMU DUNI HIVYO KUHATARISHA MAISHA YETU!!
si kweli ofisi nyingi tu zimesimamiwa na watu wa darasa la saba kwa muda mrefu na hakukua na zilienda vizuri tu
 
Jamaa ni mbaguzi wa waziwazi, mimi nasema huenda hana washauri wazuri au hashauriki
 
Kauli za namna hii zinaakisi kile alichokisema Sugu kuwa serikali inaongozwa kwa mizuka.Serikali inayosimamia mfumo wa Elimu unaozalisha vilaza haina na haiwezi kuwa na sababu za kuwanyanyapaa vijana wetu waliosoma kupitia mfumo wa serikali unaozalisha vilaza.

Ukilaza ni matokeo ya mfumo wetu wa Elimu ulioshindwa kutoa Elimu bora,badala yake umejikita katika kuongeza maelfu ya vijana wasio na sifa za kielimu.


Angalia matokeo ya kidato cha nne 2015, kisha tumuulize Rais,vilaza hao ni zao la nani kama si serikali yake mwenyewe?



View attachment 353396


Ikiwa wengi wa wanafunzi wanaomaliza secondary hufeli,nani anayepaswa kulaumiwa kwa matokeo hayo mabovu ya vijana wetu? Ukilaza ni matokeo ya Sera yetu ya Elimu iliyoshindwa kutatua changamoto za utoaji wa Elimu,hivyo anapotokea kiongozi Mwenye mamlaka ya kusimamia Sera,akaanza kutoa dhihaka kwa wananchi wake kwa kuwaita vilaza,kiongozi huyo anakuwa ni kielelezo cha viongozi kushindwa kutumia madaraka yao na dhamana zao kwa ajili ya Taifa letu.
Cheki sasa,kwahiyo "VILAZA" ni zaidi ya asilimia 88????....Inji hii!!!?
 
Alijuta kwa nini alikuwepo eneo la tukio, naona mkwere alikuwa mdogo kama piritoni
Aisee bila kuingiza mambo ya itikadi,mkwere jana alikuwa ktk wakati mgumu sana tena mbele ya wana jamii ambayo anaiongoza!ok ana madhaifu yake lkn siyo kivile
 
kilaza kilaza tu, tunawajua, mboye, msigwa, sugu, prof wa vilaza a.k.a haule, na wewe mtoa uzi, msichukie, nyie ni vilaza hakuna namna
 
Hapana Okw, Rais wetu anapenda tu utani, hapungukiwi busara. Kwa mfano, baada ya kutania kuwa wazee katika nchi hii ndio wamelifikisha taifa hili mahali pabaya, kwa kutambua kuwa ametania, siku mbili baadaye first lad akajitokeza mbele ya media na kusema kuwa, wazee ndio wameliletea maendeleo taifa hili! Jana, pale UDSM baada ya kusifia China kuwa ni rafiki wa kweli kwa Tanzania kwa kuwa inatoa misaada bila masharti tofauti na nchi nyingine ambazo hutoa misaada kwa masharti, naye dakika chache rais wetu akatangaza kutoa msaada wa bilioni 10 UDSM lakini kwa masharti!..tumzoee tu Okw!
Hata mimi noea naamini sas president anapenda kuchomekea jokes kwenye hotuba zake, haiwezekani ndo iwe vile burebure
 
Pia nilimsikia akisema kachaguliwa na mungu, sasa sijui nani kamchangua kati ya mungu na masikini.
 
Ina maana hata maafande wetu wa polis ni vilaza, wengi wao ni standard Seven na form four failure
 
kilaza kilaza tu, tunawajua, mboye, msigwa, sugu, prof wa vilaza a.k.a haule, na wewe mtoa uzi, msichukie, nyie ni vilaza hakuna namna
We tetea hoja iliyo mezani siyo unaanza kutaja watu waliokuzidi kila kitu mjinga wewe.unafikiri sababu we ni KILAZA kila mtu ni KILAZA??Dont fool your yourself mate.
 
Kwa kauli hiyo....asilimia 95 ya watanzania ni vilaza....sasa atuombe radhi.....haiwezekani wazee wa nchi hii wamsomeshe halafu shukrani anawaita watanzania vilaza
 
da! tunashukuru mh magu kutuita vilaza hakika hii inchi haitokua ya uchumi wa kati wa viwanda kutokana na mfumo wa elimu ni mbovu tunatakiwa tuige wenzetu walio endelea mifumo yao kama ujerumani ambapo kwa level ya elimu ya juu mwanafunz hutunukiwa chet kwakila level mfano mwaka wa kwana chet cha awali, wapili o'diploma, wanne a,diploma the last one degree so mtu atasoma atakapoishia anapatastahik yake utakuta mtu anasoma mwaka wa mwisho disco da! kwel bado 2po ktk colonial education, Na hata level ya secondary tusiangalie mtiani mmoja kwan unamkuta mtu anauwezo ila kutokana na sababu mbalimbali zaweza pelekea huyu mtu kufanya vibaya nakupoteza ndoto hatimae kupoteza nguv ya taifa huu mfumo pia upo kenya hii ni research nilizofanya kutoka extenal force na leo hii ndo hao wanaitwa vilaza lkn kichwan zipo angalia leo ukimpeleka chet, diploma anafanya vizur sabab mfumo ni rafik yang ni hayo
 
da! tunashukuru mh magu kutuita vilaza hakika hii inchi haitokua ya uchumi wa kati wala viwanda kutokana na mfumo wa elimu ni mbovu tunatakiwa tuige wenzetu walio endelea, mifumo yao kama ujerumani ambapo kwa level ya elimu ya juu mwanafunz hutunukiwa chet kwakila level mfano mwaka wa kwanza chet cha awali, wapili o'diploma, watatu A'diploma the last one degree so mtu atasoma atakapoishia anapatastahik yake utakuta mtu anasoma mwaka wa mwisho disco da! kwel bado 2po ktk colonial education, Na hata level ya secondary tusiangalie mtiani mmoja kwan unamkuta mtu anauwezo ila kutokana na sababu mbalimbali zaweza pelekea huyu mtu kufanya vibaya nakupoteza ndoto hatimae kupoteza nguv ya taifa huu mfumo pia upo kenya hii ni research nilizofanya kutoka extenal force na leo hii ndo hao wanaitwa vilaza lkn kichwan zipo ukitaka kujua angalia leo ukimpeleka chet, diploma anafanya vizur sabab mfumo ni rafik, yang ni hayo
 
Nimeonelea leo niseme kwa lengo la kuelewesha umma nini hasa kimesababisha Magufuli aonekane ni rais anayetoa kauli kali na muda mwingine za kuudhi hasa kwa hii ya kuita wanafunzi kuwa baadhi ni vilaza.

Kabla ya yote napenda kusema kuwa mimi nilikuwa ccm nikahama na Lowassa na tarudi CCM kama Lowassa atarudi CCM na sikumpigia kura Magufuli pamoja na kwamba tunatokea wote Geita na hapa sihitaji maelezo mengi ila angalieni thread zangu kabla ya uchaguzi.

Magufuli ameathirika na ngoma za kienyeji hususani ngoma ya beni ambapo ili ujenge jina basi lazima uwe na kauli za ajabu ajabu ikiwezekana hata kauli za kuudhi tu wanaokuzunguka.

Rais Magufuli ukiachilia mbali ngoma za jadi kama hii beni pia amecheza ngoma zingine za aina ya bugobogobo nk.

Baba yangu alishawahi kuwa mchezaji katika ngoma hizi na tabia hii ilitukosti sana watoto japo alikuwa anatupenda na tulimzoea.

Nakumbuka nikiwa shule ya Msingi Kafita tulitumwa mchago nilipomwambia nimefuata mchago alinijibu....kachukue pesa mezani ulipokuwa umeziacha wakati unaenda shuleni. Sikwenda ndani nilibaki nimesimama tu hadi akanitoa nikarudi shule.

Magufuli nakumbuka alishatoa kauli kama hii akiwaambia wanakigamboni wapige mbizi japo mimi nilifahamu ni matani.

Katika ngoma hizo ukiwa na tabia ya kutoa kauli za kukera basi malenga atakupenda na kukuita jina lako mara kwa mara ili uonekane na iwe rahisi kupata hata mademu.

Kwenye hizo ngoma ukiwa mpenda matani (kauli za ajabu ajabu walikuwa wanaitwa: Mahoyoki (wingi) au ihoyoki (mmoja).

Hivyo Magufuli kuacha hizi kauli hadi atakaposahau asili ya maisha yake mimi haniumizi akili ila wanafunzi hawajatendewa haki na aache ubabe japo namuunga mkono kwa dhamira ya dhati ya kuirudisha nchi katika uwajibakaji na kupambana na rushwa.
 
Back
Top Bottom