MWAISEMBA CR
Member
- Apr 21, 2014
- 86
- 78
KAULI ZA KIPUUZI ZA VIONGOZI WA KISIASA DHIDI YA VYOMBO ZA DINI ZINAPASWA ZIPINGWE VIKALI
Na: Shujaa Charles Richard Mwaisemba (CRM)
Kwa muda mrefu sasa imeanza kuzoeleka na kuonekana ni desturi kwa viongozi wa kisiasa hasa hawa Ma-DC na RC(Wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa) kutoa kauli za kipuuzi na matamko yenye ukakasi na yasiyofuata misingi ya kisheria kwa kutumia mamlaka zao vibaya kuamrisha matamko yao yafautwe na kutekelezwa kama walivyoyasema
Lakini cha kushangaza kutokana na ujinga wa watanzania walio wengi kwa kutokujua haki za kisheria, bado kumeendelea kuwepo na watu wanatetemeka na kushabikia kauli hizo za kipuuzi za Viongozi hao wa kisiasa.Mfano Majuzi hapa amesimama mkuu wa wilaya ya Ilala,Mhe Sophia Mjema
“Kuna watu wanapiga mapambio Jumatatu mpaka jumatatu, Ukiingia huko ndani watu 5, wewe j3 mpaka j3 unaita watu, huna watu ,funga!” Anaendelea kusema “Tunajua sisi katika kuomba ni mara hizi 3, yaani ijumaa (Waislam), Jumamosi(Wasabato) na Jumapili(Wakristo wengine).HIZI SIKU NYINGINE HAKUNA MARUFUKU, Ninyi kazi mnafanya saa ngapi, Jumatatu hadi Jumatatu, “
DC huyu SOPHIA MJEMA aliendelea kukazia kuwa siku za kusali na kufungulia spika anazozitambua lazima ziwe hizo siku 2 yaani jumamosi na Jumapili kwa wakristo, Hivyo akamalizia kumpatia afisa utamaduni kuyafanyia kazi
Viongozi wa namna hii wasiojua sheria inapaswa wote wafukuzwe mara moja, Ni sheria ipi inayosema siku ya mtu kumuabudu Mungu wake ni ijumaa, jumamosi na Jumapili tu?Wewe mpagani, usiyejua hata sheria za nchi, Utafundisha watu wamuabudu Mungu ni muda gani na siku gani za kusali? Nani kakwambia Mungu anaabududiwa ijumaa, jumamosi au Jumapili? Au ni kwa sheria zako za kipagani?
Unatufundisha wakristo tusali eti jumamosi na jumapili? Kama hujui sheria za katiba yetu inayotupa uhuru wa kuabudu basi usizungumze sheria za ukristo usizozijua.Sheria ya wakristo ya kumwabudu Mungu ni siku zote na hata akichagua siku Fulani ni ya kuadhimisha tu {WARUMI 14:5-6 “Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. 14.6 Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu.”}
Kwa mfano Waislam wanaoswali swala tano, Je ni kwamba ni watu ambao hawafanyi kazi? Kila mtu anasisitizwa kufanya kazi kwa wakati wake ili apate kula,Maana kutokufanya kazi hata kwenye maneno ya Mungu ni dhambi.Na kila mtu ana muda wake wa kazi wengine asubuhi wengine usiku, hata hao unaodai wa wachungaji wanaofanya ibada jumatatu hadi jumatatu kazi zao ni hizo hizo za kuwasaidia watu wenye mateso na kuonewa wanaitwa watumishi wa Mungu kama wewe ulivyo mtumishi wa serikali.
Kupiga marufuku watu kusali katikati ya wiki pale wapatapo muda ni kuingilia uhuru wa kuabudu tuliopewa na katiba yetu ya jamuhuri wa muungano “Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya Muungano, KAZI YA KUTANGAZA DINI, KUFANYA IBADA NA KUENEZA DINI ITAKUWA NI HURU NA JAMBO LA HIARI YA MTU BINAFSI; na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za Mamlaka ya nchi”. Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo: sheria ya 1984 Number 15, ib. 6
Kwahiyo Mtumishi wa serikali unapoanza kuingilia uhuru wa watu kuabudu na kuwapangia muda na siku za kusali unasababisha hatari kubwa na hata unaweza kutowesha amani ya nchi pale kauli za namna hii za kichochezi zinapozungumzwa bila kufuata misingi ya kisheria.
Mpaka hapa ninapozungumza nina ushahidi wa makanisa mengi kupigwa marufuku si tu kuabudu kwenye mikesha, Vyombo kuzuiwa kupigwa na kutumika wakati wa ibada na mbaya zaidi vyombo vya dola yaani polisi wameshaanza kuingilia ibada za watu siku kati kati ya wiki hata jumapili kuzuia wasifanye ibada kwa madai kuwa ni kelele kwa wananchi wanaowazunguka.Jambo hili likinyamaziwa hivi ni hatari kwa nchi na linaweza kuzusha machafuko makubwa kwa kuingilia uhuru wa vyombo vya dini
Ikiwa serikali itaanza kunyamazia kauli za kipuuzi za viongozi kama hawa itafanya watu kuanza kuhoji, Mbona Misikiti kila siku usiku kunakuwepo na azana ambazo zinawatoa watu usingizini hata wasiohusika, Mbona yapo mabaa yanapiga kelele usiku kuchwa na zaidi watu wataanza kuhoji kwanini mnaingilia uhuru wa mtu kuabudu na kuzuia watu kufanya ibada zao isipokuwa siku mnazowapangia wao?Nani kakwambia nchi hii ni ya wakristo na waislam? Wapagani je wasali lini?
Ikiwa Serikali inaona matatizo yanayotokana na hicho kinachoitwa kelele za makanisa, misikiti au mabaa basi serikali itenge maeneo maalum ya majengo hayo ambayo yapo mbali na maeneo ya makazi ya watu, sio kuwapa uhuru kujenga katikati ya makazi ya watu alafu unaanza kuwazuia na kuwapangia siku za kufanya ibada na siku za kukutana na kuwazuia kutumia vyombo vya mziki vinavyoelekezwa Kulingana na imani zao.Serikali inaweza kushauri wapunguze sauti za vyombo vyao ila si kutuma mapolisi kuingilia mikesha na kuzuia watu kufanya ibada.Ikiwa wanataka hizo kauli zao zifanyiwe kazi basi wapeleleke mswada bungeni kupitisha kuondoa sheria ya sasa ya uhuru wa kuabudu kuliko kutumia mamlaka zenu kupiga marufuku kwa mambo yaliyo nje ya katiba za nchi yetu.
Na: Shujaa Charles Richard Mwaisemba (CRM)
Kwa muda mrefu sasa imeanza kuzoeleka na kuonekana ni desturi kwa viongozi wa kisiasa hasa hawa Ma-DC na RC(Wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa) kutoa kauli za kipuuzi na matamko yenye ukakasi na yasiyofuata misingi ya kisheria kwa kutumia mamlaka zao vibaya kuamrisha matamko yao yafautwe na kutekelezwa kama walivyoyasema
Lakini cha kushangaza kutokana na ujinga wa watanzania walio wengi kwa kutokujua haki za kisheria, bado kumeendelea kuwepo na watu wanatetemeka na kushabikia kauli hizo za kipuuzi za Viongozi hao wa kisiasa.Mfano Majuzi hapa amesimama mkuu wa wilaya ya Ilala,Mhe Sophia Mjema
“Kuna watu wanapiga mapambio Jumatatu mpaka jumatatu, Ukiingia huko ndani watu 5, wewe j3 mpaka j3 unaita watu, huna watu ,funga!” Anaendelea kusema “Tunajua sisi katika kuomba ni mara hizi 3, yaani ijumaa (Waislam), Jumamosi(Wasabato) na Jumapili(Wakristo wengine).HIZI SIKU NYINGINE HAKUNA MARUFUKU, Ninyi kazi mnafanya saa ngapi, Jumatatu hadi Jumatatu, “
DC huyu SOPHIA MJEMA aliendelea kukazia kuwa siku za kusali na kufungulia spika anazozitambua lazima ziwe hizo siku 2 yaani jumamosi na Jumapili kwa wakristo, Hivyo akamalizia kumpatia afisa utamaduni kuyafanyia kazi
Viongozi wa namna hii wasiojua sheria inapaswa wote wafukuzwe mara moja, Ni sheria ipi inayosema siku ya mtu kumuabudu Mungu wake ni ijumaa, jumamosi na Jumapili tu?Wewe mpagani, usiyejua hata sheria za nchi, Utafundisha watu wamuabudu Mungu ni muda gani na siku gani za kusali? Nani kakwambia Mungu anaabududiwa ijumaa, jumamosi au Jumapili? Au ni kwa sheria zako za kipagani?
Unatufundisha wakristo tusali eti jumamosi na jumapili? Kama hujui sheria za katiba yetu inayotupa uhuru wa kuabudu basi usizungumze sheria za ukristo usizozijua.Sheria ya wakristo ya kumwabudu Mungu ni siku zote na hata akichagua siku Fulani ni ya kuadhimisha tu {WARUMI 14:5-6 “Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. 14.6 Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu.”}
Kwa mfano Waislam wanaoswali swala tano, Je ni kwamba ni watu ambao hawafanyi kazi? Kila mtu anasisitizwa kufanya kazi kwa wakati wake ili apate kula,Maana kutokufanya kazi hata kwenye maneno ya Mungu ni dhambi.Na kila mtu ana muda wake wa kazi wengine asubuhi wengine usiku, hata hao unaodai wa wachungaji wanaofanya ibada jumatatu hadi jumatatu kazi zao ni hizo hizo za kuwasaidia watu wenye mateso na kuonewa wanaitwa watumishi wa Mungu kama wewe ulivyo mtumishi wa serikali.
Kupiga marufuku watu kusali katikati ya wiki pale wapatapo muda ni kuingilia uhuru wa kuabudu tuliopewa na katiba yetu ya jamuhuri wa muungano “Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya Muungano, KAZI YA KUTANGAZA DINI, KUFANYA IBADA NA KUENEZA DINI ITAKUWA NI HURU NA JAMBO LA HIARI YA MTU BINAFSI; na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za Mamlaka ya nchi”. Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo: sheria ya 1984 Number 15, ib. 6
Kwahiyo Mtumishi wa serikali unapoanza kuingilia uhuru wa watu kuabudu na kuwapangia muda na siku za kusali unasababisha hatari kubwa na hata unaweza kutowesha amani ya nchi pale kauli za namna hii za kichochezi zinapozungumzwa bila kufuata misingi ya kisheria.
Mpaka hapa ninapozungumza nina ushahidi wa makanisa mengi kupigwa marufuku si tu kuabudu kwenye mikesha, Vyombo kuzuiwa kupigwa na kutumika wakati wa ibada na mbaya zaidi vyombo vya dola yaani polisi wameshaanza kuingilia ibada za watu siku kati kati ya wiki hata jumapili kuzuia wasifanye ibada kwa madai kuwa ni kelele kwa wananchi wanaowazunguka.Jambo hili likinyamaziwa hivi ni hatari kwa nchi na linaweza kuzusha machafuko makubwa kwa kuingilia uhuru wa vyombo vya dini
Ikiwa serikali itaanza kunyamazia kauli za kipuuzi za viongozi kama hawa itafanya watu kuanza kuhoji, Mbona Misikiti kila siku usiku kunakuwepo na azana ambazo zinawatoa watu usingizini hata wasiohusika, Mbona yapo mabaa yanapiga kelele usiku kuchwa na zaidi watu wataanza kuhoji kwanini mnaingilia uhuru wa mtu kuabudu na kuzuia watu kufanya ibada zao isipokuwa siku mnazowapangia wao?Nani kakwambia nchi hii ni ya wakristo na waislam? Wapagani je wasali lini?
Ikiwa Serikali inaona matatizo yanayotokana na hicho kinachoitwa kelele za makanisa, misikiti au mabaa basi serikali itenge maeneo maalum ya majengo hayo ambayo yapo mbali na maeneo ya makazi ya watu, sio kuwapa uhuru kujenga katikati ya makazi ya watu alafu unaanza kuwazuia na kuwapangia siku za kufanya ibada na siku za kukutana na kuwazuia kutumia vyombo vya mziki vinavyoelekezwa Kulingana na imani zao.Serikali inaweza kushauri wapunguze sauti za vyombo vyao ila si kutuma mapolisi kuingilia mikesha na kuzuia watu kufanya ibada.Ikiwa wanataka hizo kauli zao zifanyiwe kazi basi wapeleleke mswada bungeni kupitisha kuondoa sheria ya sasa ya uhuru wa kuabudu kuliko kutumia mamlaka zenu kupiga marufuku kwa mambo yaliyo nje ya katiba za nchi yetu.