Bashir Yakub
Member
- May 27, 2013
- 84
- 1,562
KAULI YA NAPE KUWA,HAKUNA WIZI WA VIFURUSHI NA MWENYE USHAHIDI APELEKE, NI YA HOVYO MNO.
Na Bashir Yakub, WAKILI
+255 714 047 241.
Wizi upo na ushahidi ni vigumu kuupata. Na hii ni kwasababu ushahidi wa matumizi ya vifurushi wanao wenyewe wanaotuuzia vifurushi. Wao ndo wana Mita za ufuatiaji sisi hatuna.
Mathalan, ni mtumiaji yupi mwenye kifaa cha kufuatilia matumizi ya GB 1 aliyoinunua. Ajue kwamba wakat nikiperuz mita ya matumizi ilikuwa ikitembea kwa spidi fulan hivyo mpaka sasa nimetumia kiasi fulani. Nape mwenyewe hana uwezo huo.
Vifaa hivyo na mita za kufuatilia natumizi wanazo wenyewe wanaotuuzia mabando. Halafu bado Nape anaomba ushahidi wa matumizi kutoka kwa mwananchi wa Manzese, tuachage utani jamani.
Sisi watumiaji ni vipofu. Tunajua tunachonunua lakini hatujui tulichonunua kinatumika vipi na kwa mwendo upi. Kwenye matumizi tumezibwa macho na ni maksudi. Tunasubiri tu kuambiwa BANDO LAKO LIMEKWISHA.
Unawezaje kumtaka kipofu aliyepigwa akupe ushahidi wa kuona aliyempiga. Halafu umlazimishe kuwa kama hakuona basi hujapigwa. Huyu haoni unamtakaje akupe ushahidi wa kuona tukio likitendeka.
Kwanza Nape amejuaje kuwa hakuna wizi. Ni kampuni au taasisi ipi imepata access ya kufanya uchunguzi wa kina kwenye mitambo ya makampuni ya simu na kugundua kuwa hakuna wizi.
Suala la wizi wa vifurushi ni la teknolojia ya hali ya juu mno. Ni suala ambalo kuligundua unahitaji muda na teknolojia iliyo juu ya ile ya makampuni ya simu. Sio suala la kumtaka mwananchi wa Kivule akuletee ushahidi.
Yapo makampuni makubwa ya kimataifa yanafanya kazi hizi. Unahitaji kuyapa kazi na muda ili yakuletee taarifa ya uchunguzi wa kiteknolojia.
Rafiki yangu mmoja kutoka makampuni haya haya ya simu ananiambia hakuna kampuni zinazoogopwa na Makampuni ya simu kama hizi kampuni ambazo kazi yake ni kufuatilia matumizi ya vifurushi na mda wa maongezi.
Ananiambia kuna moja ilitoka ufaransa ikaja kuomba kibali kufanya kazi Tanzania haikuthubutu kupata. Makampuni ya simu kwa kushirikiana na akina fulani yalihakikisha haianzishi operesheni zake nchini na haikuweza.
Suala la wizi wa vifutushi sio dogo. Ni kubwa mno na kilio cha mda mrefu cha Watanzania. Tunahitaji uchunguzi wa kina kutoka makampuni maalum yanayofanya kazi hizi na wadau. Ghana walifanya na wizi uliogindulika ulikuwa wa kutisha.
Sisi sio wajinga tulalamike kila siku tunaibiwa wakati sio kweli, tuheshimiane bana.
Yaani Nape anafanya uchunguzi wa jambo kubwa kama hili kwa kuwauliza makampuni ya simu na Tcra, serious??. Yaani unamuuliza mtuhumiwa halafu unategemea akupe majibu ya kujitia hatiani.
Na wao wanakujibu kwamba hakuna wizi wowote bali ni watu tu wenyewe wanaacha simu zinajiupdate vifurushi vinaliwa halafu wanalalamika wameibiwa. Na wewe unakuja mbio kutwambia hivyo hivyo kama walivyokwambia.
Kwa mfano ulitegemea wakwambie nini labda. Kwamba ni kweli tunawaibia watu vifurushi ama. Tuache mzaha na maisha ya watu.
Ni ahadi yetu ya dhati kwenu kuwa suala la vifurushi katu halitaisha kirahisi bila mwizi kukamatwa, iwe leo ama kesho, liwe jua ama mvua, machweo ama mawio, usiku ama mchana.
Na Bashir Yakub, WAKILI
+255 714 047 241.
Wizi upo na ushahidi ni vigumu kuupata. Na hii ni kwasababu ushahidi wa matumizi ya vifurushi wanao wenyewe wanaotuuzia vifurushi. Wao ndo wana Mita za ufuatiaji sisi hatuna.
Mathalan, ni mtumiaji yupi mwenye kifaa cha kufuatilia matumizi ya GB 1 aliyoinunua. Ajue kwamba wakat nikiperuz mita ya matumizi ilikuwa ikitembea kwa spidi fulan hivyo mpaka sasa nimetumia kiasi fulani. Nape mwenyewe hana uwezo huo.
Vifaa hivyo na mita za kufuatilia natumizi wanazo wenyewe wanaotuuzia mabando. Halafu bado Nape anaomba ushahidi wa matumizi kutoka kwa mwananchi wa Manzese, tuachage utani jamani.
Sisi watumiaji ni vipofu. Tunajua tunachonunua lakini hatujui tulichonunua kinatumika vipi na kwa mwendo upi. Kwenye matumizi tumezibwa macho na ni maksudi. Tunasubiri tu kuambiwa BANDO LAKO LIMEKWISHA.
Unawezaje kumtaka kipofu aliyepigwa akupe ushahidi wa kuona aliyempiga. Halafu umlazimishe kuwa kama hakuona basi hujapigwa. Huyu haoni unamtakaje akupe ushahidi wa kuona tukio likitendeka.
Kwanza Nape amejuaje kuwa hakuna wizi. Ni kampuni au taasisi ipi imepata access ya kufanya uchunguzi wa kina kwenye mitambo ya makampuni ya simu na kugundua kuwa hakuna wizi.
Suala la wizi wa vifurushi ni la teknolojia ya hali ya juu mno. Ni suala ambalo kuligundua unahitaji muda na teknolojia iliyo juu ya ile ya makampuni ya simu. Sio suala la kumtaka mwananchi wa Kivule akuletee ushahidi.
Yapo makampuni makubwa ya kimataifa yanafanya kazi hizi. Unahitaji kuyapa kazi na muda ili yakuletee taarifa ya uchunguzi wa kiteknolojia.
Rafiki yangu mmoja kutoka makampuni haya haya ya simu ananiambia hakuna kampuni zinazoogopwa na Makampuni ya simu kama hizi kampuni ambazo kazi yake ni kufuatilia matumizi ya vifurushi na mda wa maongezi.
Ananiambia kuna moja ilitoka ufaransa ikaja kuomba kibali kufanya kazi Tanzania haikuthubutu kupata. Makampuni ya simu kwa kushirikiana na akina fulani yalihakikisha haianzishi operesheni zake nchini na haikuweza.
Suala la wizi wa vifutushi sio dogo. Ni kubwa mno na kilio cha mda mrefu cha Watanzania. Tunahitaji uchunguzi wa kina kutoka makampuni maalum yanayofanya kazi hizi na wadau. Ghana walifanya na wizi uliogindulika ulikuwa wa kutisha.
Sisi sio wajinga tulalamike kila siku tunaibiwa wakati sio kweli, tuheshimiane bana.
Yaani Nape anafanya uchunguzi wa jambo kubwa kama hili kwa kuwauliza makampuni ya simu na Tcra, serious??. Yaani unamuuliza mtuhumiwa halafu unategemea akupe majibu ya kujitia hatiani.
Na wao wanakujibu kwamba hakuna wizi wowote bali ni watu tu wenyewe wanaacha simu zinajiupdate vifurushi vinaliwa halafu wanalalamika wameibiwa. Na wewe unakuja mbio kutwambia hivyo hivyo kama walivyokwambia.
Kwa mfano ulitegemea wakwambie nini labda. Kwamba ni kweli tunawaibia watu vifurushi ama. Tuache mzaha na maisha ya watu.
Ni ahadi yetu ya dhati kwenu kuwa suala la vifurushi katu halitaisha kirahisi bila mwizi kukamatwa, iwe leo ama kesho, liwe jua ama mvua, machweo ama mawio, usiku ama mchana.