..asante kwa majibu yako murua.
..lakini kwenye bandiko lako la awali sikuona mahali ukielekeza kwamba mgombea awe na SERA, na aamini ktk ITIKADI fulani.
..well, sasa kama tukiongeza vigezo hivyo viwili then kidooogo, kwa mbaaali, naweza kukubalina na wewe kwamba hukuwalenga Dr.Sla/a na Tundu Lissu.
NB:
..kuhusu ITIKADI. Do u have a preference, or anything goes?
Nimezungumzia nafsi ya mtu anayegombea, nafsi ya mpiga kura kuangalia na kupima : Utu, Uzalendo, Uimara, Ufanisi, Uadilifu, Uwajibikaji na Umoja.
iwe
Kama hivi ndio vitendea kazi vya msingi mimi kama mpiga kura navithamini ili buheri yangu ya kipato na ustawi viwe na uhakika na ushamiri (kazi, elimu, ajira, pato, haki) basi anayetaka nimwamini na kumpa dhamana ya shahhada yangu ya kura ni lazima naye awe na uwezo wa kuyatenda na kuyaamini kwa dhati hayo 7 ambayo ndio masharti yangu, na naamini ni Watanzania wengi wanayathamini kuliko ahadi za kuletewa utajirio na neema!
Itikadi ni imani ya mtu na jumuia, Sera ni mfumo wa utekelezaji wa Itikadi na kuleta matunda yanayoonekana na kueleweka.
Tulikuwa na Itikadi ya Ujamaa wa Kiafrika, na kuwa na sera ya kujitegemea na tukajenga mazingira ya kukamilisha hilo.
Tumeutupa Ujamaa na Kujitegemea, hatuna sera au itikadi inayoeleweka kichama. ACT ndio jana wametangaza Itikadi na Sera za chama na zinavutia maan azinagusa Utu, Uzalendo, Uwajibikaji, Ufanisi kwa jinsi ninavyozitafsiri mimi na Watanzania wengi.
Uongozi mkuu wa CCM umeizika Itikadi ya Ujamaa na Kujitegemea, wanachama na wafuasi wengi bado wanaiamini Itikadi hiyo. Sera za kujitegemea zimevunjwa na sera za utajirisho na ushindani wa kibiashara ambazo zinanufaisha wachache na hasa wawekezaji wageni ndio Sera za CCM, na hazinufaishi wananchi na zinalitia Taifa hasara na kuongeza mzigo wa madeni.
Wapinzani wanachechemea kuwapa Watanzania itikadi na Sera za kuamsha hamasa za ujenzi wa Taifa lao. Sanasana Sera an Itikadi zinaelekea ni kuleta mfarakano, mivutano na uchu wa madaraka.
Badala ya Itikadi na Sera, vyama vimekimbilia kutengeneza Ilani za uchaguzi, ambazo ni ahadi za kusadikika na hazieleweki zitapimika vipi.
Ndio maana narudia tena kusema hatuwezi piga hatua bila kuwa na Utu, Uzalendo, Uimara, Uadilifu, Ufanisi, Uwajibikaji na Umoja.
Nguzo hizi zianze kwetu mmoja mmoja, zitambae kama jamii, vyama na Taifa na haya ndiyo yawe masharti ya kura za 2015.