Kauli ya Mchungaji kuelekea Uchaguzi 2015

Kauli ya Mchungaji kuelekea Uchaguzi 2015

Naona huyu mchungaji haitakii mema CCM. Watanzania tukijiuliza hayo na kuchgaua viongozi kwa vigezo hivyo mbona CCM haitapata hata diwani mmoja, achilia mbali wabunge na Rais
 
Shida itakuwa kujaribu kufunga na kuomba ili kiongozi mwadilifu na mzalendo na muwajibikaji atoke ccm!!!
 

My Sister Tiba,, hapa sasa ndipo lazima uukubali ukweli mchungu, kuwa huyu ndie rais wako ajaye!. Ni kweli hao ngombea ndio utajiri wake pekee alioanza nao maisha ila kwa vile huyu ni mtu wa Mungu, hivyo ana upako fulani kama wa Midas, everything he touches turn to gold!. Alipokuwa mgurugenzi wa AICC neema ikamwangukia, akaanza kumiliki land Arusha, Mungu akamuangazia akapewa wizara ya Ardhi, enzi hizo viwanja vikitolewa bure tena prime areas!, akajenga zile nyumba akakodisha mabalozi faida akaitumia kama mtaji wa Alfa!. Mungu akamuangazia zaidi akapewa wizara ya Mifugo, Ranchi ya zaita zikauzwa kwa bei ya bure na yeye uwezo alikuwa nao hivyo akanunua!. Mungu akambariki zaidi na kumfanya akawa Waziri Mkuu wetu lakini katika maandalizi ya kumfanya awe rais wetu, Mungu akampitisha kwenye majaribu ya Richmond, ili iwe kama kawaida baada ya mateso na kifo, huja ufufuko na uzima wa milele, sasa hii ndio safari ya kukitwaa kile kiti alitayarishiwa na Mungu mwenyewe, au hukumsikia TB Joshua?!.

Kilichoanzisha Alfa ni mtaji kutokana na vitega uchumi vyake, hata hizo Nyumba London ni faida tuu kutoka vitega uchumi vyake!.

Kwa vile ni mtu wa Mungu na mwenye upako wa neema, hao marafiki zake wanaomchangia wamejikuta wanabarikiwa sana hivyo kuchanga zaidi na zaidi kama sadaka tuu makanisani, hawasubiri kuja kulipwa baadae ila kila ukitoa tuu unajikuta unazidishiwa mara sabaini fii sabaa!.

Hiyo the bottom you are very right, EL is not clean!, yae he is not, hata JK was not clean, but he was!, hata CCM is not clean, but it is!, hata YULE aliyekuja kuukomboa ulimwengu huu, aliisha sema hakuja kwa ajili ya wakamilifu!, alikuja kwa ajili ya hao hao ambao sio clean!. Na akasema "Wainuliwe wote wenye mizigo waje kwa YEYE wapumzishwe!", ndio maana hata lile zigo la Richmond, amelibeba tuu sio lake, na sasa anasubiri kuinuliwa ili apumzishwe kule juu!.

Kama JK amweza kuwa presidential material na ametutawala miaka hii kumi, EL ni 100 times better, ataiinua hii nchi kutoka huku kwenye vumbi na majajala na kutupeleka kwenye ile nchi ya ahadi, mabomba mchi nzima yatatoa maziwa na asali!.

Hata alipokuja YEYE, mwanzo alikataliwa hivi hivi mnavyotaka kumkataa huyu mtu!, hivyo sasa YEYE aliyemwandikisha atajidhihirisha utukufu wake kwenu, kwa "lile jiwe walilolikataa waashi, litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni!",

Amesema "Huu ni mwamba na juu ya mwamba huu, nitalifa taifa langu!".

Just wait and see!.

Pasco

Mkuu Pasco, kwanza naomba nikukosoe kwa hiyo lugha unayo tumia as if wewe nawe sasa umekuwa book 7, kauli ya utake usitake huyo ndiye rais wangu ajaye. Kauli hii kwangu mimi is just sweeping statement ambayo haina ukweli hata chembe. Lowassa bado ana mtihani wa kupitishwa na chama chake lakini pia kama tunaamini kwenye demokrasia na tunatarajia kuwa na uchaguzi ambao utakuwa huru na wa haki, huyu mtu wako bado atashindana na mgombea wa vyama vya upinzani. Hapo napo anayonafasi ya kuchaguliwa au la sasa hii kauli ya lazima atakuwa rais wangu ajaye siitarajii kutoka kwa mtu kama wewe.

Kutoka huo mtiririko wa jinsi alivyopata utajiri wake, umeonyesha dhahiri EL ni mtu wa namna gani, anajijali yeye na watu waliomzunguka haijali dhamana ya kusimamia mali za watanzania aliyopewa. Hatufai huyu.

Pia umesema JK wakati anachaguliwa na yeye hakuwa msafi hivyo kwa kuwa JK alichaguliwa akiwa mchafu bado tuendelee kufanya kosa hilo hilo la kuwapeleka watu wasio wasafi Ikulu. Inawezekana JK hakuwa msafi kwani pesa ziliizomuingiza ikulu ziliibiwa kutoka benki kuu (EPA), na matokeo ya kuwa na rais aliyeingia madarakani kwa kuiba pesa za umma wote tumeyaona. Wezi wanakalishwa mezani na kuombwa warudishe pesa walizoiba wakati raia wengine kwa wizi wa kuku wanapigwa mvua na kuozea jela. Naogopa kusema mengi kwani bado ninazipenda kucha zangu, lakini Lowassa kwa msimamo wangu binafsi (kumbuka kura yangu ni moja tu) hatufai hata kiduchu.

Tiba
 
Mkuu tumekusikia, na katika sifa hizo zote, kwa bahati nzuri yupo mtangaza nia mmoja tuu aliyezifika na kuzipitiliza, sio tuu kwa kukubali kukosolewa pekee, bali kukubali kuzibeba dhambi za wengine na kukaa nazo pembeni ili kuliepushia taifa na shari, huku ni kujitoa mwenyewe nafsi yako kwa ajili ya taifa lako!.

Kwenye hilo la uadilifu, mtu mwenye karama ya utajiri, anayetoa sehemu za utajiri wake na kuwagawia masikini, kuwagawia wengine, ni mtu mwenye baraka anayestahili kukabidhiwa nchi ili sasa awagawiye wote!.

Mtu wa aina hii ndiye rais wetu October 25!.

Pasco
Inaonekana kama unajua kuandika lakini ni kama vile akili huna. Miwani unayovaa ikusaidie kuona vitu halisi na ubongo wako upe uwezo wa kutafsiri hali halisi. Uwezo aliowapa mungu wa kuandika msiutumie kuangamiza nchi yetu. Ni rais wa aina gani huyo ambaye baadhi ya sifa yake ni kugawa vitu vyake? Tunataka atakayewagawie wavuvi nyavu siyo huyu wenu anayechukua samaki wetu sote na kutuhadaa kwa kutugawia kwa mkono wa kushoto.
 
Kwa ile afya yake,October 25 atakuwa anatembelea Machella
Kwa vile uimara wa afya ya mtu, uzima au ugonjwa uko determined the the powers above us!, aliyeliandika jina lake na atakayemsimamia hadi kupitishwa CCM, ndiye atakayeiimarisha afya yake kwa sababu Lowassa ameisha tamka wazi, atayaweza yote katika YEYE!.

Pasco
 
Wakuu, nimefuatilia majibizano kati ya Pasco na wadau wengine. Kwa waliwahi kumsoma Achebe ktk A Man of the People na Ibsen ktk An Enemy of the People watamwelewa Pasco. He is trying to be both ironical and satirical. Anasema kinyume cha kile anachomaanisha kwa namna ya kejeli. Hivyo asilaaniwe kwani hamaanishi anachokisema.
 
Hapa Mchungaji Ameshindwa Tu Kunyosha Maelezo Anamaanisha Watanzania Tusiichague Ccm Kawa Mazoe Sifa Zote Alizozitaja Hauwezi Ukazikuta Kwa Mgombea Wa Ccm Hiyo Mambo Iko Ukawa
 
Kwa vile uimara wa afya ya mtu, uzima au ugonjwa uko determined the the powers above us!, aliyeliandika jina lake na atakayemsimamia hadi kupitishwa CCM, ndiye atakayeiimarisha afya yake kwa sababu Lowassa ameisha tamka wazi, atayaweza yote katika YEYE!.

Pasco
Chadema inadhamira ya kweli ya kukutoa wewe utumwani. Chadema iko determined kuigeuza nchi hii kuwa ya maziwa na asali. Na kwakuwa tumetubu kwa Mungu kwa kosa kubwa la kumweka Kikwete kama wana Israel walipomlazimisha Mungu awape Sauli kuwa mfalme, wana wa Israel walipata misukosuko wakapigwa mapigo hadi walipotubu na kumpata mfalme Daudi ndivyo na sisi watanzania tumetubu kwa Mungu kwa kukipa chama cha majizi, waongo,wauaji na makatili. Mungu ameridhia kutupa 'Daudi' wetu. UKAWA. Ndio maana tunasema UKAWA TUMAINI LETU
 
Hapa naona kuna Chanya na Hasi. Ninachoamini Mimi ni kwamba mwisho wa yote Chanya itasimama na kuishinda Hasi.
 
Uchaguzi 2015

Itikadi kuu ya kitaifa iwe ni kujenga upya Tanzania, kama Taifa huru yenye kuzingatia vipaumbele vifuatavyo: Utu, Uzalendo, Ufanisi, Uwajibikaji, Uadilifu Uimara na Umoja wa Kitaifa

Wenye Nia Urais, Ubunge, Udiwani wapimwe si kwa kauli zao tuu, bali kwa matendo yao kama wanaweza kujenga: Utu, Uzalendo, Ufanisi, Uadilifu, Uwajibikaji, Uimara na Umoja

Tusipime wagombea kwa utamu na ntiririko wa ufahamu wa kuongea au maneno tunayotaka kusikia, tusikubali kuwapa dhamana na majukumu makubwa kutonkana na umahiri wa kampeni zao, kujaa kwa umati wa wafuasi au vilio vyao vya kulilia dhamana ya kumkomboa Mtanzania.

Tukague Ufanisi wa utendaji wa wagombea katika miaka yao ya uwakilishi na kulitumikia Taifa na kuzioanisha na kauli walizozitoa miaka hiyo ya nyuma. Je tuwape dhamana na kwaamini wataweza sasa? Kama walishindwa kujenga mfumo fanisi wa maendeleo na uwajibikaji katika ngazi za wilaya, je kwenye duru za Kitaifa watatuaminishaje wana uwezo kufanikiwa?

Tuhoji uimara wao na utendaji wao mpaka sasa katika miaka mitano iliyopita, wamewafanyia nini cha maendeleo wananchi wachache waliowapa dhamana ya uwakilishi na uongozi? Je, kama katika wilaya na majimbo, wamepata matatizo ya ushawishi kustawisha jamii iliyo imara na yenye maendeleo endelevu na si ya maneno,tuaminije wanaweza kuongoza Taifa zima?

Tuhoji umadhubuti na uimara wa wagombea kusimamia haki, kujenga demokrasia ya kweli, kukubali upinzani, kukemea na kuwajibisha uhujumu. Je, matendo yao yameonyesha msimamo unaoeleweka kujenga jamii yenye demokrasia ya kweli yenye ushirikishi?

Tuhoji, je wamekuwa wawazi bila woga kupiga vita uhujumu ambao una sura mbali mbali kama uvivu, uzembe, matumizi mabaya ya dhamana na fedha, uhujumu, rushwa na uonevu?

Uimara wa Tanzania na maendeleo yake ya kijamii, kiuchumi na kisiasa si wingi wa rasilimali na ahadi za kuneemeka bila kuzingatia: Utu, Uzalendo, Ufanisi, Uadilifu, Uwajibikaji na Umoja katika kujenga Uimara wa Taifa na Utaifa!

Taifa letu, haliwezi kupiga hatua mbele kushinda vita dhidi ya Ujinga, Umasikini, Maradhi na Uhujumu bila kuzingatia malengo haya ya msingi.

Hatutaweza futa ujinga na maradhi tusipothamini Utu, Uzalendo, Uadilifu, Uwajibikaji, Ufanisi na Umoja.

Ni kujidanganya eti utajiri wa rasilimali na mapato ya uzalishaji yatutasaidia kutatua matatizo ya Taifa huku nguzo kuu na tunu za Utaifa wetu zinapuuziwa na kutokupewa kipaumbele kama dira iliyo kuu ya kujenga jamii shirikishi.

Vita kuushinda Uhujumu havina faida kwa Umoja hatuna Uzalendo, Utu, Ufanisi, Uwajibikaji na Uimara kupambana na ufisadi, rushwa, ujangili, utegemezi na utovu wa nidhamu!

Haitawezekana kufuta Umasikini pasipo kuwa na kipumbele cha Uzalendo, Utu, Ufanisi, Uwajibikaji, Uadilifu au Umoja pamoja na rasilimali zote tulizonazo na kujitangaza kwa majisifu.

Tuliposema ili tuendelee tunahitaji Watu, Ardhi Siasa Safi na Uongozi Bora, ni wakati huu ambapo tunahitaji kuchagua siasa safi na uongozi bora ulio wazi nawenye dhamira ya kulitumikia Taifa kwa dhati kuzingatia vigezo hivi vya : Utu, Uzalendo, Ufanisi, Uadilifu, Uimara, Uwajibikaji na Umoja.

Watanzania tuachane na mazoea ya kuamini maneno ya Wanasiasa ambao hawajengi Umoja au Ushirikishi kutokana na Amani tuliyonayo.

Tanzania na Watanzania ni lazima tujisahihishe mwaka huu wa uchaguzi kwa kutoa dhamana kwa watu wenye hekima, busara, ujasiri na uimara wa kutafakari, kufanya kazi na kufanya maamuzi yenye matokeo chanya: bora na endelevu. Tuwape dhamana watu ambao ni wepesi kujisahihisha na kufanyia kazi mapungufu yao.

Watanzania tukatae kupewa viongozi wasiojiheshimu, waongo, wazandiki, wanafiki na wenye tamaa na uchu wa madaraka na mamlaka. Hawatufai Ng'o!

Tanzania itajengwa na kuongozwa na viongozi waadilifu, wasikivu, wavumilivu, wachapa kazi wenye kukubali kukosolewa na kufanyia kazi kwa moyo maoni tofauti na mawazo yao.

Nami natangaza rasmi: Nia yangu ni kuleta na kupata Uongozi utakaoongoza kuzingatia: Uzalendo, Utu, Uadilifu, Ufanisi, Uwajibikaji, UImara na Umoja kwa Taifa letu na Watanzania wote kwa ujumla bila kujali tofauti zozote zile!

Rev.hivyo ulivyo viongea hapo bila unafiki haviwezi patikana ndani ya ccm vunapatikana nje ya ccm.
 

My Sister Tiba,, hapa sasa ndipo lazima uukubali ukweli mchungu, kuwa huyu ndie rais wako ajaye!. Ni kweli hao ngombea ndio utajiri wake pekee alioanza nao maisha ila kwa vile huyu ni mtu wa Mungu, hivyo ana upako fulani kama wa Midas, everything he touches turn to gold!. Alipokuwa mgurugenzi wa AICC neema ikamwangukia, akaanza kumiliki land Arusha, Mungu akamuangazia akapewa wizara ya Ardhi, enzi hizo viwanja vikitolewa bure tena prime areas!, akajenga zile nyumba akakodisha mabalozi faida akaitumia kama mtaji wa Alfa!. Mungu akamuangazia zaidi akapewa wizara ya Mifugo, Ranchi ya zaita zikauzwa kwa bei ya bure na yeye uwezo alikuwa nao hivyo akanunua!. Mungu akambariki zaidi na kumfanya akawa Waziri Mkuu wetu lakini katika maandalizi ya kumfanya awe rais wetu, Mungu akampitisha kwenye majaribu ya Richmond, ili iwe kama kawaida baada ya mateso na kifo, huja ufufuko na uzima wa milele, sasa hii ndio safari ya kukitwaa kile kiti alitayarishiwa na Mungu mwenyewe, au hukumsikia TB Joshua?!.

Kilichoanzisha Alfa ni mtaji kutokana na vitega uchumi vyake, hata hizo Nyumba London ni faida tuu kutoka vitega uchumi vyake!.

Kwa vile ni mtu wa Mungu na mwenye upako wa neema, hao marafiki zake wanaomchangia wamejikuta wanabarikiwa sana hivyo kuchanga zaidi na zaidi kama sadaka tuu makanisani, hawasubiri kuja kulipwa baadae ila kila ukitoa tuu unajikuta unazidishiwa mara sabaini fii sabaa!.

Hiyo the bottom you are very right, EL is not clean!, yae he is not, hata JK was not clean, but he was!, hata CCM is not clean, but it is!, hata YULE aliyekuja kuukomboa ulimwengu huu, aliisha sema hakuja kwa ajili ya wakamilifu!, alikuja kwa ajili ya hao hao ambao sio clean!. Na akasema "Wainuliwe wote wenye mizigo waje kwa YEYE wapumzishwe!", ndio maana hata lile zigo la Richmond, amelibeba tuu sio lake, na sasa anasubiri kuinuliwa ili apumzishwe kule juu!.

Kama JK amweza kuwa presidential material na ametutawala miaka hii kumi, EL ni 100 times better, ataiinua hii nchi kutoka huku kwenye vumbi na majajala na kutupeleka kwenye ile nchi ya ahadi, mabomba mchi nzima yatatoa maziwa na asali!.

Hata alipokuja YEYE, mwanzo alikataliwa hivi hivi mnavyotaka kumkataa huyu mtu!, hivyo sasa YEYE aliyemwandikisha atajidhihirisha utukufu wake kwenu, kwa "lile jiwe walilolikataa waashi, litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni!",

Amesema "Huu ni mwamba na juu ya mwamba huu, nitalifa taifa langu!".

Just wait and see!.

Pasco

#Pasco ,
Nadhani uliandika hivyo ukitumaini unamsaidia, na hicho ni kidogo ulicho andika juu yake. Yamkini unafahamu mengi zadi juu yake. Unaweza kuendelea kutumwagia sifa zake nyingine zinazo elezea aliyo yafanya akiwa kiongozi katika Serikali na Nje ya Serikali?

Wakati nasubiri mifano mingine mingi kutoka kwako ama wachangiaji wengine, nitakuja kutoa general evaluation baadaye.
 
Mkuu Pasco, kwanza naomba nikukosoe kwa hiyo lugha unayo tumia as if wewe nawe sasa umekuwa book 7, kauli ya utake usitake huyo ndiye rais wangu ajaye. Kauli hii kwangu mimi is just sweeping statement ambayo haina ukweli hata chembe. Lowassa bado ana mtihani wa kupitishwa na chama chake lakini pia kama tunaamini kwenye demokrasia na tunatarajia kuwa na uchaguzi ambao utakuwa huru na wa haki, huyu mtu wako bado atashindana na mgombea wa vyama vya upinzani. Hapo napo anayonafasi ya kuchaguliwa au la sasa hii kauli ya lazima atakuwa rais wangu ajaye siitarajii kutoka kwa mtu kama wewe.

Kutoka huo mtiririko wa jinsi alivyopata utajiri wake, umeonyesha dhahiri EL ni mtu wa namna gani, anajijali yeye na watu waliomzunguka haijali dhamana ya kusimamia mali za watanzania aliyopewa. Hatufai huyu.

Pia umesema JK wakati anachaguliwa na yeye hakuwa msafi hivyo kwa kuwa JK alichaguliwa akiwa mchafu bado tuendelee kufanya kosa hilo hilo la kuwapeleka watu wasio wasafi Ikulu. Inawezekana JK hakuwa msafi kwani pesa ziliizomuingiza ikulu ziliibiwa kutoka benki kuu (EPA), na matokeo ya kuwa na rais aliyeingia madarakani kwa kuiba pesa za umma wote tumeyaona. Wezi wanakalishwa mezani na kuombwa warudishe pesa walizoiba wakati raia wengine kwa wizi wa kuku wanapigwa mvua na kuozea jela. Naogopa kusema mengi kwani bado ninazipenda kucha zangu, lakini Lowassa kwa msimamo wangu binafsi (kumbuka kura yangu ni moja tu) hatufai hata kiduchu.

Tiba

Watu wanaangamia kwa kukosa maarifa usishangae mtu mwenye upeo mpana akifanya dhihaka na mioyo ya watanzania huku wakiendelea kukaza shingo kuwa el ndie rais ajae hakika hizo shingo zitavunjika.
 
Mkuu Pasco, kwanza naomba nikukosoe kwa hiyo lugha unayo tumia as if wewe nawe sasa umekuwa book 7, kauli ya utake usitake huyo ndiye rais wangu ajaye. Kauli hii kwangu mimi is just sweeping statement ambayo haina ukweli hata chembe. Lowassa bado ana mtihani wa kupitishwa na chama chake lakini pia kama tunaamini kwenye demokrasia na tunatarajia kuwa na uchaguzi ambao utakuwa huru na wa haki, huyu mtu wako bado atashindana na mgombea wa vyama vya upinzani. Hapo napo anayonafasi ya kuchaguliwa au la sasa hii kauli ya lazima atakuwa rais wangu ajaye siitarajii kutoka kwa mtu kama wewe.

Kutoka huo mtiririko wa jinsi alivyopata utajiri wake, umeonyesha dhahiri EL ni mtu wa namna gani, anajijali yeye na watu waliomzunguka haijali dhamana ya kusimamia mali za watanzania aliyopewa. Hatufai huyu.

Pia umesema JK wakati anachaguliwa na yeye hakuwa msafi hivyo kwa kuwa JK alichaguliwa akiwa mchafu bado tuendelee kufanya kosa hilo hilo la kuwapeleka watu wasio wasafi Ikulu. Inawezekana JK hakuwa msafi kwani pesa ziliizomuingiza ikulu ziliibiwa kutoka benki kuu (EPA), na matokeo ya kuwa na rais aliyeingia madarakani kwa kuiba pesa za umma wote tumeyaona. Wezi wanakalishwa mezani na kuombwa warudishe pesa walizoiba wakati raia wengine kwa wizi wa kuku wanapigwa mvua na kuozea jela. Naogopa kusema mengi kwani bado ninazipenda kucha zangu, lakini Lowassa kwa msimamo wangu binafsi (kumbuka kura yangu ni moja tu) hatufai hata kiduchu.

Tiba
Dada yangu Tiba, nakupa pole tena, kwa sababu tuna watu wa aina tatu, aina ya kwanza ni wishful thinkers, hawa wana wish Tanzania ipate rais mzuri, mwenye uwezo, mwenye mission na vision ya Tanzania tunayoitaka na asiye na mawaa yoyote kama anavyowish muanzisha mada hii Rev. Kishoka, ambaye ana wish tumpate rais mwenye sifa hizi!, hili linawezekana kwa sababu Tanzania tunao watu wenye sifa hizo, but only if wishes were horses !...keep wishing, ku wish ni kitu kimoja na reality ni kitu kingine!.

Kundi la pili ni wale waliokata tamaa!, hawa sitawazungumzia, bali ndio idadi kubwa na waliowengi ambao kwanza hawajiandikishi, wakijiandikisha hawajitokezi kupiga kura!, hawa ndio hukaa mstari wa mbele kwenye maandamano na kujaza umati wa watu kwenye mikutano ya kampeni!, they are simply good for nothing!.

Kundi la tatu ni la ma-realist, hili ndilo kundi la wakweli!, mimi ndio nimo kwenye kundi hili!, sisi ma realist ni wale tunaokubali ukweli halisi jinsi ulivyo hata uwe ni ukweli mchungu vipi, huo ndio ukweli wenyewe!. Chama cha CCM ndicho chama tawala, ndicho chama kinara cha rushwa, ndicho chama mlezi wa ufisadi, kwa kifupi, CCM kimeoza, kinanuka hadi kimevunda!, ila hiki ndicho chama tawala, na hali ya upinzani nchini kwetu ilivyo nyoronyoro, bado hakuna chama cha kukishinda CCM, hivyo mgombea wa CCM ndie rais wetu 2015!, huu pia ndio ukweli mchungu!, ila ruksa ku wish otherwise!.

1995 timu inayoitwa Boys II Men, iliundwa na waligombea pamoja, waliondoka pamoja na kupanda tende moja kenda kuchukua fomu Dodoma, na wote wawili walikatwa ndipo from them wakaamua wasigombee tena wote wawili , wakaunda kitu kinachoitwa mtandao ambapo walikubaliana 2005 atangulie mmoja, 2015 afuatie mwingine!.

Ni kweli 2005 mmoja akaingia, na mwingine akafanywa ndie kiranja mkuu!. Kulipotokea kashfa ya Richmond ikimhusu mmoja, ambapo angeondoka mchi ingetikisika na CCM isingeweza tena kurudi madarakani, kiranja mkuu akakubali kujitwika msalaba, akazibeba dhambi za mwenzeke ili kwa kuteswa kwake mwenzake akapona na CCM ikapona!.

Sasa ndio 2015 na hii ni zamu ya aliyebakia!. Huyo aliyebakia kweli si msafi, ni fisadi, afya ni mgogoro, ila CCM pia sio chama kisafi, ni chama cha rushwa ni chama cha kifisadi ila ndicho chama kilichopo!. Kufuatia zigo alilojitolea kulibeba sii zigo lake, ukimya wake katika zigo hilo ndio karata yake ya turufu ya kupitishwa na vikao vya juu vya Chama chake, ama apitishwe aendelee kukaa kimya, au akatwe ambapo itakuwa ni kama kumwaga ugali, then na yeye atamwaga mboga!.

Kuliko haya yatokee, CCM italazimika kumpitisha Lowassa in return to his silence, na mgombea akiishapitishwa CCM huyo ndio rais wetu!, Tanzania bado hatuna upinnzani, ili ikitokea asipitishwe, na akaamua kujitoa CCM na kujiunga UKAWA, hii ndio njia pekee ambapo upinzani utaingia madarakani ili yatimie maneno ya Mwalimu kuwa upinzani wa kweli, utatoka CCM!, hivyo as a realist, nakuandaa tuu kisaikolojia ujiandea kuukubali ukweli halisi kuwa 2015 Lowassa ndie rais wako!, you either take it, or leave it!.

Pasco

 
Wakuu, nimefuatilia majibizano kati ya Pasco na wadau wengine. Kwa waliwahi kumsoma Achebe ktk A Man of the People na Ibsen ktk An Enemy of the People watamwelewa Pasco. He is trying to be both ironical and satirical. Anasema kinyume cha kile anachomaanisha kwa namna ya kejeli. Hivyo asilaaniwe kwani hamaanishi anachokisema.

Wewe tupo pamoja
 
MUNGU AMEKATAZA DHAMBI,sisi Watanzania tunaifuata dhambi na kufanya umalaya wa kisiasa mchana kweupe.Mwaka huu tutajua ni yapi makanisa na misikiti ya kweli na yenye kutambuliwa na MUNGU.Tutawajua wachungaji na masheik ambao ndani mwao hamna MUNGU ila mna shetani anayejifanya MUNGU,Tusidhani kuwa ss watanzania eti ni wema sana,tutakuwa tunajidanganya.Ndugu zangu Kwenda kwetu kanisani na misikitini ni vzr kukaleta maana ambayo ni nzuri kwa taifa letu.Siamini kama MTU mweusi aishie Tanzania eti Leo hii anasimama na kushangilia Wezi hakikaTAIFA hili linaanza kutia AIBU sasa.ADHABU YA KUWANADI MAFISADI,WEZI,WAHUJUMU UCHUMI na WAUAJI HADHARANI ETI kwa Kutumia jina la MUNGU NDUGU ZANGU Hatutaepuka ghadhabu ya MUNGU Mwenyezi tuko mbioni kuangamia na muda si mrefu mtajionea .WATU WOTE WENYE TUHUMA dhidi ya UMMA hatustahili hata kuwazungumzia maana aibu inaturudia ss na wao WANATUSHANGAA na kutudharau na wanasema kumbe Tanzania ni TAIFA LA mazuzu.TUSIJITOE AKILI MAKUSUDI kama wafanyavyo baadhi ya wagombea kupima akili zetu. HAKUNA UMASKINI UPITAO UMASKINI WOTE DUNIANI KAMA UMASKINI WA AKILI MAANA UNATEMBEA UKIWA MFU.
 
Back
Top Bottom