Kauli ya Kusema DP World watamiliki Maeneo yote ya Bandari za Bahari, Maziwa na Nchi kavu ni kama posa tu, Mchumba mwenyewe atajulikana baadae

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,555
Mwanasheria Mohamed Salum amesema kuwa Kauli ya Kusema DP World watamiliki Maeneo yote ya bandari za Bahari, Maziwa na Nchi kavu ni kama posa tu, lakini mchumba mwenyewe atajulikana wakati wa kusaini mikataba midogo ya makubaliano itakayokuja baadae.

Amebainisha kuwa hilo ni jina tu lililotumika kama kichwa cha habari cha mkataba na halimaanishi kuwa mkataba utakuwa hivyo kwa baadae.

Pia, kwa kuwa kutakuwa na awamu mbalimbali za makubaliano, mikataba ijayo ndio itabainisha ni maeneo gani hasa ambayo DP World watapewa baada ya kumalizika kwa awamu ya kwanza ya makubaliano ya awali.

Ameyasema haya wakati akijibu maswali ya wadau kwenye mjadala unaoendelea Clubhouse ukiongozwa na Msemaji Mkuu wa Serikali ndugu Gerson Msigwa.

Chanzo: Msemaji Mkuu wa Serikali (Clubhouse)
 
1. Hivi dunia ya sasa, nani anaweza akamposa mwali ambae hamjui..??
2. Je awamu ya kwanza ya mkataba, ukomo wake ni lini..??
 
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Huyo mwansheria ni zezeta tu, mkataba umeshasema hao waarabu watamiliki maeneo yote aliyoyataja, na saini ya Mbarawa tayari iko pale chini, ajabu huyo bush lawyer anasema hiyo ni posa tu, sasa haoni kama hiyo posa ndio tayari imeshawapa waarabu "mke" kwa saini ya Mbarawa?

Wasiendelee kupoteze muda kutafuta wasaliti wa kuutetea ule mkataba, wajue ule mkataba hauteteeki, ni wa kinyonyaji kwa mtanganyika, hautufai uvunjwe.
 
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Ndio tayari biashara imeshafanyika na bunge limebariki.Hakuna kelele itaweza kuwarudisha nyuma.Na waarab hawaogopi risasi wala bomu.
Ni kama wanachinja ngamia tu
 
Watu wazima mnaenda kwenye nyumba ya wazazi wa binti kuposa halafu mnaingia mitini hamuoi. Sasa kwanini msiache tu kuposa mpaka mtakapomua kuoa. Kifupi tumeshaharibu
 
kutokana na kelele wamebadilisha gia agani kuna mambo yangefanyika ila wamekwana wanatengeneza mazingira mazuri ili kuficha ahibu ambayo ingetokea
 
Mwanasheria Mohamed Salum amesema kuwa Kauli ya Kusema DP World watamiliki Maeneo yote ya bandari za Bahari, Maziwa na Nchi kavu ni kama posa tu, lakini mchumba mwenyewe atajulikana wakati wa kusaini mikataba midogo ya makubaliano itakayokuja baadae.

Amebainisha kuwa hilo ni jina tu lililotumika kama kichwa cha habari cha mkataba na halimaanishi kuwa mkataba utakuwa hivyo kwa baadae.

Pia, kwa kuwa kutakuwa na awamu mbalimbali za makubaliano, mikataba ijayo ndio itabainisha ni maeneo gani hasa ambayo DP World watapewa baada ya kumalizika kwa awamu ya kwanza ya makubaliano ya awali.

Ameyasema haya wakati akijibu maswali ya wadau kwenye mjadala unaoendelea Clubhouse ukiongozwa na Msemaji Mkuu wa Serikali ndugu Gerson Msigwa.

Chanzo: Msemaji Mkuu wa Serikali (Clubhouse)
Yuko Kati 526 waliofeli law school.
 
"Maliasili zetu Watanzania zinachukuliwa bure haya ni maajabu,sitaruhusu hilo" Hayati Rais John Pombe Magufuli.
 

Attachments

  • VID-20230715-WA0734.mp4
    9.5 MB
Back
Top Bottom