Kauli ya 'Bora Jiwe kuliko CCM'

Losambo

JF-Expert Member
Nov 8, 2011
2,612
864
Wanajamvi kauli ya ni keri kuchagua jiwe kuliko kuichagua CCM imekuwa mwiba maana imesambaa kwa kasi sana na kuwa kampeni tosha kwa CDM!!!!!

Mlio Arusha ni mashahidi wa hilo, kila unayemuuliza anasema Lema kaonewa lakini wanajisumbua tu sisi tupo tayari kulipia jiwe kura kuliko CCM!!!!

Hali hii inaashiria anguko kubwa sana la CCM na kibaya zaidi pandikizi la chuki ambao sidhani kama litaisha leo.

Ushauri kama CCM ina macho basi iachane na mizengwe hii ya kijinga iangalie hali ya taifa letu jinsi inavyokwenda.

Nawasilisha.
 
Hiyo ni kufuru kwa wapiga kura wa jimbo la Arusha . Wanastahli kupata mwakilishi imara bungeni na siyo jive la Chadema kama alichokiamini Godbless Lema.
 
Mimi si mwana chama wa chama chochote officially,though ni miongoni mwa maelfu ya watz wanao amini ktk CHADEMA na mageuzi!

Ushauri wangu kwa CCM ni kama ifuatavyo:

1/Jitahidini kutumia hata sehemu ndogo ya masaburi iliyo baki kufikiri,maana mliacha zamani kutumia Bongo zenu kiasi cha kuzoea kufikiria masaburi na muda unavyo kwenda inaonesha masaburi pia yamechoka!!!
Najua pro ccm weng mtanitukana lakini naandika haya kuweka kumbukumbu kwa vijazi vijavyo!
Hali ya nchi ni mbaya!
Nakumbuka:
-Mlijaribu kutumia dola kulinda CCM enz za Mkapa mkakwama!
-Mmepambana kufa na kupona kwenye sanduku la kura,imeshindikana!
-Mmejaribu kuiba kura imeshindikana, NA HUU UKAWA UKOMO WA MASABURI KUFIKIRI!

-Kwa sasa mmeamua kutumia mahakama aidha kupora ubunge wa cdm,au kuwachelewesha wabunge wake kwa kuwa "shinda" na kuwashauri wakate rufaa ili kesi iendelee!

SINA HAKIKA Mmetumia kiungo gani baada ya UBONGO na MASABURI kufeli!
Kila kiungo kinacho nijia,sipati tafsida yake na hata nikiandika kwa mafumbo hapa na ikawa reported niko likely kula ban!
Anyway,kiungo kilichopo directly na masaburi msithubutu kufikiria maana vitu najisi hupitia hapo hasa watu wanapo "kula tunda" AKA "Kujinafasi"!
Lakini kumbukeni,hapo viburudisho "hupigwa chini" halafu "wanavimba juu miezi kumi kasoro moja"

Nimetumia Lugha kali,Lakini CCM mnaipeleka nch machinjioni!

Leo Arusha wanasema "hata jiwe tunachagua kuliko CCM",Sijui Mbeya watasemaje Sugu akiporwa ubunge,Dar,SINGIDA NK!

Scrn imelowa machozi,ngoja nilale tu!
 
Ni rahisi CCM kukurupuka kusema CHADEMA ina kejeli wananchi kusema bora JIWE. Naomba ni wa pre-empty kwamba maana ya hii kauli ni kwamba by crook and hook CCM haitakiwa kabisa na ninawaonea huruma kwani katika historia ya CCM hakuna kampeni zitakazokuwa ngumu kama za kumnadi mgombea wenu ktk jimbo la Arusha. Kwanza hata akipita tu mtaani zimwi la zomea zomea litakuwa linamwandama na kisaikolojia atakosa confidence kwani jukwaani timu za zomea zomea zitakuwa zimejipanga kisawasawa.
 
Back
Top Bottom