MENGELENI KWETU
JF-Expert Member
- May 8, 2013
- 9,557
- 24,180
Anajifanya kajitoa akiliUmeasahau kuwa anagombea jimbo la Chalinze au unajitoa akili
Anajifanya kajitoa akiliUmeasahau kuwa anagombea jimbo la Chalinze au unajitoa akili
hivi sasa hana issue.
Azungumzie pia afya ya lowassa, ya mwili sio shida ila ya akili ndio inagusa maisha yetu. Haiwezekani achaguliwe lakini thinking yote ifanywe na watu wa genge.
Sidhani na siamini kwamba ramani ya siasa ya Jamhuri yetu itabaki ilivyo ifikapo Desemba 2015. Ni ishara ya kheri na mwelekeo mwafaka kwa demokrasia ya Taifa letu
Sio kwamba wameonyesha misimamo yao hadharani bali wao wameonyesha chuki za wazi wazi kwa lowasa. Wangekuwa wakweli wangewachambua wagombea wote tukaona nani anafaa kuiongoza nchi. Wao wamejikita kwa EL tu wengine hawasemwi. Kuna kashifa nyingi lakini wao ni richmond ndio wanaifahamu. Alishasema rich ni maagizo ya wakubwa. Mwapachu hana chuki na john, ndio maana hajamtaja katika maelezo yake.
Mkuu umenena ukweli... tatizo kubwa la wasomi wetu ni unafiki na kuto kuwa wasafi... walio wengi wakipewa madaraka kuna issues wanafanya hv wanakuwa na makandokando yao na kuogopa kutoka ndani ya mfumo wa ccm na serikali yake hata kama wanaona kabisa wananchi wanaonewa au kilicho mbele yao si maslahi ya taifa.... ndo maana msigwa alisema akisimama prof bungeni, mchango wake ni kama mtu wa darasa la 7... sio kwamba hawajui bali prof anakuwa anatetea jambo ambalo haliamini.....Ukweli utadhidi kudhihiri, Lowasa ni tajiri inawezekana, mimi sina uhakika ana kiasi gani cha pesa ila ninachojua alianza utumishi miaka mingi nyuma,na hata biashara naambiwa pia alianza zamani na zingine alirithi, sina uhakika........ila kuna mtoto wa Rais anatuhumiwa pia kuwa na utajiri mkubwa wa ghafla, sina uhakika ila yanasemwa, na hata yule Dr wa Mihogo naye aliwahi kutamka siku moja kuwa dogo ana ukwasi wa ajabu wakati kamaliza chuo juzi juzi tu, kaupata wapi huo utajiri.....hili wanazuoni wetu hawalisemi, wala kina polepole hawasemi......hii Nchi imejaa unafiki na chuki za hatari.
Mwapachu anatufungua macho kuwa huko CCM kuna matajiri wa kufa mtu ila hawasemwi, anayeandamwa ni Lowasa.......wasomi jitokezeni muweke ukweli hadharani, hii Nchi inawahitaji sana wakati huu, tena kupita wakati wowote ule.
Hivi leo tukichambua nani kati yetu ni tajiri zaidi ya Lowassa tutakuwa na viongozi wanao kidhi mategemeo yetu? Kuhusu hili swala la Richmond: Hivi baada ya taarifa ya Tume ya Bunge ya Dr Mwakyembe, Serikali ilitoa majibu. Mbona kwenye tuhuma za Bunge kuhusu Tegeta Escrow imekuwapo taarifa toka kwa Chief Secretary kuhusu suala hilo?
Naamini kwa dhati kabisa kwamba Edward Lowassa atakuwa kiongozi ambaye atasaidia ramani hii kubwa na muono mpya.
Source: Ibrahim Kibopile
Mtoto wa rais ni mgombea kwenye uchaguzi huu?
Bandiko lako limejaa "sijui/sina uhakika" kibao.
Unaleta 'speculation' tu jamvini.
Sifahamu vp Huyu Mwapachu atajiita msomi kwa aliondika hapo juu. Maneno yake hayana substance wala rationale behind them.
''Lakini huyo huyo Baba wa Taifa alimpenda sana Edward na kumpa madaraka ndani ya CCM na baraza la mawaziri''
Lowassa aliwahi kuwa Waziri kwenye serikali ya Mwl. Nyerere?
Nisaidieni wanazuoni!
Enzi ya mwalimu nakumbuka Lowassa kutumwa kwenda Rome kupokea TUNZO kwa niaba ya mwalimu!!
Mtoto wa rais ni mgombea kwenye uchaguzi huu?
Bandiko lako limejaa "sijui/sina uhakika" kibao.
Unaleta 'speculation' tu jamvini.
Edward alivumilia na kumsaidia mwenzake (nasita sasa hivi kutumia neno 'rafiki') Jakaya ashinde uteuzi wa mgombea wa CCM hapo 2005. Aliamua hivyo baada ya makubaliano ya 1995.
Wapo wengi wa Tanzania waliyojitolea muhanda, wa hali na mali kuungana na Edward kumwezesha Jakaya Kikwete kuwa Rais 2005. Kati yao, ndiyo wamekuwa karibu na Edward katika kinyang'anyiro cha majuzi Dodoma. Imani yao ilikuwa kwamba pamoja na mkanganyiko wa Februari 2008 wa Richmond ambao hauna mashiko yoyote ya ufisadi kwa maana ya rushwa, Rais Kikwete angemfungulia mlango mwenzake Edward kuwa mgombea wa CCM. Badala yake Edward bado akajengewa mzengwe wa utajiri kama Baba wa Taifa alivyofanya 1995.
Sidhani na siamini kwamba ramani ya siasa ya Jamhuri yetu itabaki ilivyo ifikapo Desemba 2015. Ni ishara ya kheri na mwelekeo mwafaka kwa demokrasia ya Taifa letu.Naamini kwa dhati kabisa kwamba Edward Lowassa atakuwa kiongozi ambaye atasaidia ramani hii kubwa na muono mpya.
Juma Volter Mwapachu
Source: Ibrahim Kibopile
sifahamu vp huyu mwapachu atajiita msomi kwa aliondika hapo juu. Maneno yake hayana substance wala rationale behind them.
Nimeguswa!.
Pasco
Naamini utakua team lowassa,umeguswa nini? hayo makubaliano ni kwa sababu lowassa mwenyewe anajua hakubaliki, na aliona mbali kwa kujua akimbeba mkwele mambo yatakaa sawa,kwamba ataendelea kubaki kwenye system ,yeye always ni mipango tu ya ufisadi,lowassa anajijua ni fisadi na hakubaliki! anachofanya sasa hivi ni Jeuri na dharau kwa wa tz kwa sababu ya pesa zake za ufisadi, anatafuta nini mtu mgonjwa kabisa,hakubaliki analazimisha,fisadi, halafu wazee walioheshimika miaka yote Leo wanajivua nguo hadhalani,hata sijui wamepewa nini, big up mkapa malofa hao.
Balozi Juma Mwapachu ni Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma UDOM.
Mwapachu ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Airtel Tanzania.
​
Mhe.Balozi Juma Mwapachu amewahi kushika nyadhifa mbalimbali ndani na nje ya nchi zikiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya AfrikaMashariki.
Aliwahi kuwa Balozi Mwakilishi Ufaransa na UNESCO ikijumuisha nchi za Uhispania, Ureno, Tunisia, Morocco na Algeria.
Aidha Mhe. Balozi Juma Mwapachu amekuwa mjumbe wa Bodi mbalimbali hapa nchini na amewahi kushika nyadhifa za juu katika Taasisi za Umma na binafsi. Kwa muda mrefu alikuwa naibu Mwenyekiti wa baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mhe. Balozi Juma Mwapachu amehitimu shahada ya Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki na alikuwa Mtanzania wa kwanza mwenye shahada ya Chuo Kikuu kujiungana Jeshi la Polisi nchini.
Ni mhitimu wa Diploma ya Juu ya Sheria ya Kimataifa, masuala ya Diplomasia ya Kimataifa kutoka chuo kikuu cha Sheria za Kimatatifa na Diplomasia huko New Dehli India.
Mhe.Balozi Juma Mwapachu aliwahi kutunukiwa shahada mbili za heshima ya udaktari wa falsafa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Rwanda, na amewahi kuhariri na kuchapisha majarida na vitabu mbalimbali.
Kauli ya Barozi Juma Mwapachu Kuhusu Lowassa nimekuwa kimya kwa muda mrefu katika mabadilishano ya fikra kwenye mtandao huu ambao kwa hakika, kwa maoni yangu, haubidi kuwa ni wa fikra pevu zisizo shawishika na misimamo ya 'kimalaya ya siasa'. Kama tutaserereka katika msingi huu, basi ni bora Chambi ukafunga virago na kusitisha huu mtandao.
Nimesoma mabadilishano na mabishano ya fikra kuhusu hali ya siasa nchini mwetu na hususa ni baada ya Mhe Lowassa kuamua kujiunga na Chadema na kuwa mwakilishi wa UKAWA katika kinyang'anyiro cha nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano. Sijui nyie wenzangu mmesimamia wapi katika suala hili. Naomba niseme mwanzoni kabisa kwamba nchi yetu hii leo imefikia mahali ambapo wasomi, wanazuoni kama sisi katika mtandao huu, Hatuna budi kujitokeza na kuhesabika tunamuunga nani mkono katika uchaguzi ujao wa Rais wa Tanzania.
Tuwe wakweli na siyo kuendelea kuegemea katika kificho cha 'uhuru' wa wanazuoni katika kutoa maomi na fikra kama vile sisi si wapiga kura au wananchi wanaothamini umuhimu kuhusu uongozi wa nchi yetu. Wakati huo umepitwa na hali halisi ya itikadi na maana muhimu ya uongozi wa Taifa. Sasa, Mimi binafsi, namuuunga mkono Edward Ngoyai Lowassa.
Yako mengi ambayo kazuliwa huyu ndugu yetu; tunaambiwa tangu 1995 wakati Mwalimu Julius Nyerere alipotamka kwamba 'huyu kijana ninalo faili lake, ana utajiri usiyoelezeka. Ana nyumba kadhaa.' Lakini huyo huyo Baba wa Taifa alimpenda sana Edward na kumpa madaraka ndani ya CCM na baraza la mawaziri. Kama Edward alikuwa 'corrupt' swali ni kwanini Baba wa Taifa hakumchukulia hatua za kisiasa na kisheria?
Kwanini aseme hayo aliyoyasema mwaka 1995 wakati Edward Lowassa alikuwa akiongoza kupendwa ndani ya CCM, ngazi zote na akitarajiwa ndiye angependekezwa kuwa mgombea wa Urais? Jamani, wanazuoni, lazima mtafakari historia na hali halisi ilivyokuwa. Mhe Jakaya Kikwete hakuwa 'the favourite' candidate in 1995.
Na Mwalimu alimtaka Ben Mkapa wakati ule awe Rais. Ilibidi Lowassa atoswe kinamna! Mimi namfahamu Edward, Ninyi mnaujua huo utajiri wake au basi akitoa michango hapa na pale ni pesa zake? Kati yenu mna utajiri zaidi ya Edward. Edward alivumilia na kumsaidia mwenzake (nasita sasa hivi kutumia neno 'rafiki') Jakaya ashinde uteuzi wa mgombea wa CCM hapo 2005. Aliamua hivyo baada ya makubaliano ya 1995.
Wapo wengi wa Tanzania waliyojitolea muhanda, wa hali na mali kuungana na Edward kumwezesha Jakaya Kikwete kuwa Rais 2005. Kati yao, ndiyo wamekuwa karibu na Edward katika kinyang'anyiro cha majuzi Dodoma. Imani yao ilikuwa kwamba pamoja na mkanganyiko wa Februari 2008 wa Richmond ambao hauna mashiko yoyote ya ufisadi kwa maana ya rushwa, Rais Kikwete angemfungulia mlango mwenzake Edward kuwa mgombea wa CCM. Badala yake Edward bado akajengewa mzengwe wa utajiri kama Baba wa Taifa alivyofanya 1995.
Hivi leo tukichambua nani kati yetu ni tajiri zaidi ya Lowassa tutakuwa na viongozi wanao kidhi mategemeo yetu? Kuhusu hili swala la Richmond: Hivi baada ya taarifa ya Tume ya Bunge ya Dr Mwakyembe, Serikali ilitoa majibu. Mbona kwenye tuhuma za Bunge kuhusu Tegeta Escrow imekuwapo taarifa toka kwa Chief Secretary kuhusu suala hilo?
Nani aliyejaribu kutoa maelezo ambayo yangemfungisha Lowassa au kumkomboa kwa kitendo chake cha kujiuzuru kisiasa? Badala yake, wanazuoni wenzangu ambao sidhani kama tunazo facts za kutosha tunaendelea kumshutumu Lowassa na kumwona kama vile ni corrupt na kiongozi asiyefaa. It is not fair. Mimi simlaumu Lowassa kujitoa CCM. Ni haki yake na kajieleza vipasavyo kuhusu maamuzi yake.
Je, ni uamuzi wa uroho kuhusu Urais? Jamani, wanazuoni, hivi kweli tumefikia hatua ya kumwona mtu ana uroho wa Urais? Ili awe au afanye nini ambacho sisi tufunge macho, na siyo tu kutoona, bali pia kuto chukua hatua? Ikifikia hapo, basi hatuna Taifa tena!! Taifa letu limebahatika kufika hapa lilipofika mwaka huu. Wengi hatukutarajia kwamba yale ambayo tumekuwa tukitafakari na hata kusali ghafla yameibuka.
Sidhani na siamini kwamba ramani ya siasa ya Jamhuri yetu itabaki ilivyo ifikapo Desemba 2015. Ni ishara ya kheri na mwelekeo mwafaka kwa demokrasia ya Taifa letu.Naamini kwa dhati kabisa kwamba Edward Lowassa atakuwa kiongozi ambaye atasaidia ramani hii kubwa na muono mpya.
Juma Volter Mwapachu
Source: Ibrahim Kibopile
Huko kwenu kuitwa mwana zuoni hadi uwe na degree ngapi?Kumbe yoote haya ana kabachelor degree tu ndiyo anajiita Mwanazuoni? Kwa maana mtaani kwetu kuna madogo kibao wana bachelor degrees pia nao niwaite Wanazuoni?