Francis12
JF-Expert Member
- Sep 30, 2016
- 7,533
- 22,276
Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha upinzania nchini Tanzania Chadema Freeman Mbowe amesema uamuzi wa Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai la kutangaza nafasi kiti cha ubunge wa Singida Mashariki kilichokuwa kikikaliwa na Tundu Lissu kiko wazi halijawatikisa wala kuwakatisha tamaa bali kuzidi kuimarisha dhamira yao ya kushika dola.
Mbowe ambaye ni kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Tanzania alitoa msimamo huo wa chama leo jumamosi Juni 29,2019 wakati wa kikao cha ndani kilichofanyika jana Kanda ya Nyasa
Mbowe alisema chama hicho kipo tayari hata kupoteza viti vyake vyote lakini hakitaacha kufanya kwa ajili ya wananchi hivyo amewataka wanachama wa chama hicho kutokuwa na mioyo ya visasi.
"Yaani Spika leo anamfukuza ubunge Tundu Lissu anafikiria tutalia,tunamwambia mheshimiwa spika wacha Lissu chukueni viti vyote hivi , nani ana shida na ubunge , tuna shida na wananchi " alisema Mbowe
"Wanatupa sababu zaidi za kufanya kazi vitu kama hivi haviwezi kutukatisha tamaa,vinatuimarisha katika dhamira yetu,tunafanyiwa uonevu mwingi ndani ya bunge , tunafanyiwa visa vingi .
Hivi visa havituvunji moyo vinatuimarisha"
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai alisema ,"Hasira ya kufukuza wabunge wetu ,hasira ya kutoheshimu mawazo yetu , tutaimaliza kwa kupeleka wabunge wengi kuondoa wingi wa CCM ndani ya bunge na kuiongoza serikali nchi hii"
Mbowe alilalamikia pia Kamati ya Haki ,Kinga na Maadili ya Bunge kwa kushindwa kuwashughulikia wabunge wa upinzani pekee huku ikionekana kushindwa kuwagusa wabunge wa CCM.
"Uonevu huu wanaotufanyia hatuna sababu ya kuwatukana ,tunacheka lakini dhamira ya mioyo yetu inaimarishwa sana kila mbunge angesimma kueleza anafanyiwa nini sijui ingekuwaje" alisema Mbowe.
Mbowe ambaye ni kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Tanzania alitoa msimamo huo wa chama leo jumamosi Juni 29,2019 wakati wa kikao cha ndani kilichofanyika jana Kanda ya Nyasa
Mbowe alisema chama hicho kipo tayari hata kupoteza viti vyake vyote lakini hakitaacha kufanya kwa ajili ya wananchi hivyo amewataka wanachama wa chama hicho kutokuwa na mioyo ya visasi.
"Yaani Spika leo anamfukuza ubunge Tundu Lissu anafikiria tutalia,tunamwambia mheshimiwa spika wacha Lissu chukueni viti vyote hivi , nani ana shida na ubunge , tuna shida na wananchi " alisema Mbowe
"Wanatupa sababu zaidi za kufanya kazi vitu kama hivi haviwezi kutukatisha tamaa,vinatuimarisha katika dhamira yetu,tunafanyiwa uonevu mwingi ndani ya bunge , tunafanyiwa visa vingi .
Hivi visa havituvunji moyo vinatuimarisha"
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai alisema ,"Hasira ya kufukuza wabunge wetu ,hasira ya kutoheshimu mawazo yetu , tutaimaliza kwa kupeleka wabunge wengi kuondoa wingi wa CCM ndani ya bunge na kuiongoza serikali nchi hii"
Mbowe alilalamikia pia Kamati ya Haki ,Kinga na Maadili ya Bunge kwa kushindwa kuwashughulikia wabunge wa upinzani pekee huku ikionekana kushindwa kuwagusa wabunge wa CCM.
"Uonevu huu wanaotufanyia hatuna sababu ya kuwatukana ,tunacheka lakini dhamira ya mioyo yetu inaimarishwa sana kila mbunge angesimma kueleza anafanyiwa nini sijui ingekuwaje" alisema Mbowe.