Bei Mbaya
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 2,262
- 843
Nilikuwa nasoma habari iliyochapishwa katika gazeti moja kuhusu wananchi wa Kata ya Mwakibete jijini Mbeya ambao, chini ya Kamati ya Maendeleo ya Kata (KAMAKA) hiyo ya Mwakibete inayoongozwa na Diwani Lucas Mwampiki kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA, waliamua kiwango cha michango kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa shule za sekondari kiwe shilingi 3,000/= badala kiwango kilichozoeleka cha shilingi 10,000/=, kiwango ambacho Mkuu wa Wilaya hiyo, Evans Balama anakitambua .Sasa katika habari hiyo, ndipo nikabaki nastaajabia kauli hizi:Mimi nimezaliwa ndani ya CCM, nimekulia ndani ya CCM, nimesomea ndani ya CCM, ninafanya kazi ndani ya CCM, hivyo sitakuwa tayari kuona vyama uchwara na sera zake uchwara ndani ya mamlaka yangu.Nina uwezo wa kukufanyia kitu chochote na jambo lolote kwa kuwatumia Usalama wa Taifa ili kukuondoa katika nafasi hiyo ya udiwani, japokuwa kufanya hivyo ni dhambi mbele za Mungu lakini nitamuomba Mungu anisamehe.