kauli kama hizi lazima zikutoe 'kipele kuku' neh

Bei Mbaya

JF-Expert Member
Nov 24, 2010
2,262
843
Nilikuwa nasoma habari iliyochapishwa katika gazeti moja kuhusu wananchi wa Kata ya Mwakibete jijini Mbeya ambao, chini ya Kamati ya Maendeleo ya Kata (KAMAKA) hiyo ya Mwakibete inayoongozwa na Diwani Lucas Mwampiki kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA, waliamua kiwango cha michango kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa shule za sekondari kiwe shilingi 3,000/= badala kiwango kilichozoeleka cha shilingi 10,000/=, kiwango ambacho Mkuu wa Wilaya hiyo, Evans Balama anakitambua .Sasa katika habari hiyo, ndipo nikabaki nastaajabia kauli hizi:“Mimi nimezaliwa ndani ya CCM, nimekulia ndani ya CCM, nimesomea ndani ya CCM, ninafanya kazi ndani ya CCM, hivyo sitakuwa tayari kuona vyama uchwara na sera zake uchwara ndani ya mamlaka yangu.”“Nina uwezo wa kukufanyia kitu chochote na jambo lolote kwa kuwatumia Usalama wa Taifa ili kukuondoa katika nafasi hiyo ya udiwani, japokuwa kufanya hivyo ni dhambi mbele za Mungu lakini nitamuomba Mungu anisamehe.”
 
Nilikuwa nasoma habari iliyochapishwa katika gazeti moja kuhusu wananchi wa Kata ya Mwakibete jijini Mbeya ambao, chini ya Kamati ya Maendeleo ya Kata (KAMAKA) hiyo ya Mwakibete inayoongozwa na Diwani Lucas Mwampiki kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA, waliamua kiwango cha michango kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa shule za sekondari kiwe shilingi 3,000/= badala kiwango kilichozoeleka cha shilingi 10,000/=, kiwango ambacho Mkuu wa Wilaya hiyo, Evans Balama anakitambua .Sasa katika habari hiyo, ndipo nikabaki nastaajabia kauli hizi:"Mimi nimezaliwa ndani ya CCM, nimekulia ndani ya CCM, nimesomea ndani ya CCM, ninafanya kazi ndani ya CCM, hivyo sitakuwa tayari kuona vyama uchwara na sera zake uchwara ndani ya mamlaka yangu.""Nina uwezo wa kukufanyia kitu chochote na jambo lolote kwa kuwatumia Usalama wa Taifa ili kukuondoa katika nafasi hiyo ya udiwani, japokuwa kufanya hivyo ni dhambi mbele za Mungu lakini nitamuomba Mungu anisamehe."
H kauli chafu sana ila ni ulevi mkubwa wa madaraka ikizingatiwa Diwani ni mwakilishi wa wanainchi.
Balama akajaribu kugombea udiwani tuone kama atapita mjinga mkubwa huyu.

Hivi hawa wakuu wa wilaya wana umuhimu gani given DED +mameya/wenyekiti wa halmashauri wapo?
 
Kuna baadhi ya kauli za wateule wa rais zinastaajabisha sana
 
hujiulizi watu wangapi wana uwezo wa kulipa hiyo sh 10 000 hapo kijijini?ccm haumuoni aibu mmeuza zain airtel kwa muhindi bhartel bila kuchukua kodi 450 bn?ingekua mimi hata thumni wasingelipa kama vile mrema alivyofutilia mbali kodi ya kichwa!shame on you!!
 
Mungu hasemehi watu kama wewe, mnanenepesha matumbo bure subirini siku ya kiama mtaona.
 
Back
Top Bottom