Katika suala zima la mahari ya mwanamke bado Dini ya Kiislamu wameendelea kuupiga mwingi

karv

JF-Expert Member
Dec 26, 2019
1,799
3,221
Nawasalimu kwa jina la jamuhuri

Bado naendelea kufuatilia masuala mazima ya ndoa hasa katika nyanja kuu 3 kimila, kidini na kiserikali.

Suala la kulipa mahari kwa mwanamke lipo na limeelezwa katika vitabu vya dini za imani zote. Kama kuna mtu anapinga hilo hebu arudi kwa mwalimu wake wa dini amfundishe vizuri.

Kimila kuna baadhi ya makabila mahali hutozwa kutokana na elimu ya binti, kwingine ubikira /kigoli (sio kwa sasa), Rangi ya ngozi, shepu, Urafiki, koo na mambo mengine.

Katika upande wa serikali bado sijafahamu kama wanaruhusu mwanamke kulipiwa mahari au la na kama ipo ni kwa misingi gani na sheria ipi (wanasheria mtatusaidia hapa).

Naomba nije kwenye swala zima la mahari kwa upande wa kidini na hapa naomba kuzungumzia katika dini ya kiislamu ambapo katika hili wapo wazi sana licha ya kwa upande wa pili WAKRISTO biblia imeelezwa kuhusu mahari pia. Lakini kama upo ufafanuzi mzuri katika hilo wanaweza kuuleta hapa tukaangalia pia sheria za ndoa ya kikristo wanazungumziaje swala hilo.

Katika dini ya kiislamu japokuwa mimi sio muumini wao nimekuwa nikisikia na kufuatilia pia katika kusikia kwaku nimenukuu vitu viwili ambavyo vinafanya niwape hongera na pongezi.
Vitu hivyo ni
~Mwanamke ndiye anayetaja mahari yake.
~Mahari ni ile iliyokuwa nyepesi kulipwa.
~Kulipa mahari ni lazima kama isipolipwa ni ruksa mwanamke kukataa ndoa.


KWANINI WAMEUPIGA MWINGI?

Ndoa nyingi zimeshindwa kufungwa sababu tu ya mwanaume kutajiwa mahari kubwa na wazazi wa mwanamke na kwamba mfanya yeye ashindwe kulipa.

Kama mwanamke anakupenda kweli hawezi kukutajia mahari ya kukukomoa maana anajua anaweza kumkosa ampendaye hivyo atataja mahari kutokana na uwezo wako.

Mtu atatajiwa mahari ambayo ipo ndani ya uwezo wake wa kulipa hivyo kupunguza malalamiko na mambo mengine.

Kuna baadhi ya wanawake huwasaidia waume zao kulipa mahari ili tu mambo yaende sawa

~Kama kuna mengine mnaweza kuongeza kwa kugusia pande zote yani kimila, kidini na kiserikali.
Ili tujue swala zima la ulipaji mahari lipoje katika makabila yetu

.................AHSANTENI.................
IMG_20220130_162237.jpg
 
Fight for the fittest of your future but not only crying about the religion issues that based God's word writings.

You have to know that there is no the God's kingdom celebrating without good actions on your historical background life styles comprised with strong faith.
 
Kwa sisi waislam na Uislam ni kwamba, Mahari ni zawadi itokayo kwa anaeowa ambayo ni makubaliano ya anaeowa na anaeolewa, kwa chochote mtakacho kubaliana.
Hivyo basi kwa mujibu wa Uislam, mahari ni mali ya mwanamke na sio mtaji kwa wazazi/wazee wa mwanamke.
HEKIMA YA MAHARI KUA HAFIFU:-
Ikitokea ktk ndoa hio hakuna tena maelewana, na imeshindikana kabisa ndoa hio kuendelea kuwepo, basi Mke kama akitaka kuachika na Mume hataki kutoa talaka, basi hapo Mke atalazimika kutoa/kurudisha mahari aliyotolewa kwa thamani ya muda husika, nahapo ataweza kupata talaka yake kisheria kutoka sehemu husika. Eg. Kutoka kwa mume au vyombo husika kama Mahakama ya kadhi au Bakwata.
 
Kwa sisi waislam na Uislam ni kwamba, Mahari ni zawadi itokayo kwa anaeowa ambayo ni makubaliano ya anaeowa na anaeolewa, kwa chochote mtakacho kubaliana.
Hivyo basi kwa mujibu wa Uislam, mahari ni mali ya mwanamke na sio mtaji kwa wazazi/wazee wa mwanamke.
HEKIMA YA MAHARI KUA HAFIFU:-
Ikitokea ktk ndoa hio hakuna tena maelewana, na imeshindikana kabisa ndoa hio kuendelea kuwepo, basi Mke kama akitaka kuachika na Mume hataki kutoa talaka, basi hapo Mke atalazimika kutoa/kurudisha mahari aliyotolewa kwa thamani ya muda husika, nahapo ataweza kupata talaka yake kisheria kutoka sehemu husika. Eg. Kutoka kwa mume au vyombo husika kama Mahakama ya kadhi au Bakwata.
 
Mi nilishangaa bro kaolea ntwara huko Mahari fourty tu halafu mtoto bado mbichiiiiiii..arooo japokuwa sisi ni wagalatia lakini akina mudi mko vizuri
 
Tutafte pesa tusipende vya dezo,yaani nioze binti yangu kwa vindizi??? What on earth!
Ndio maana talaka zimeshamiri ukanda ambao Una waislamu kwa wingi, yaani,
"Easy come, easy gone"
Hayo mambo ya ndizi yamesemwa lkn ktk Hali halisi ni kuwa dhana kubwa ni mahari kuwa hafifu ili isiwe kikwazo Kwa vijana kushindwa kuoa......na wanawake wachache Sana huenda wakahitaji juzuu au msahafu lkn wengi wao ni kiasi cha hela ambacho sio cha kumuumiza muoaji....kwahiyo kama muoaji na muolewaji wameelewana na muoaji anaweza kutoa kiasi Kikubwa zaidi kutokana na uwezo na mapenzi yake hakuna ubaya....

Ndoa kuvunjika haihusiana na mahari kuwa ndogo Ila kuna mambo mengi ndani yake...ikiwemo kutokuwepo Kwa uvumilivu ndani ya ndoa,usaliti na kadhalika.

Sasa kuonekana Kwa ndoa nyingi Kwa waislamu kuvunjika ni kwasababu Sheria inaruhusu hivyo....ingawa Mwenyezi Mungu hapendezewi na mambo ya talaka lkn inapobidi basi ni Bora watu kuachana Kwa wema kuliko wakaishi ktk uadui na kukosa Amani....kwani lengo la ndoa ni kupatikana utulivu ndani yake.

Sasa wakristo sio kwamba hawapendi kuachana Ila ni Sheria ya kanisa inasema hivyo....lkn nyuma ya pazia kuna maumivu makubwa Sana Kwa wanandoa....wengi wao wapo ktk kifungo Kikubwa ingawa hawapo gerezani lkn kama nyumba imekuwa kama gereza....watu wanatengana vyumba Kwa nembo ya ndoa ya kudumu lkn kiuhalisia inawaangiza ktk dhambi kwasababu kila mwanandoa anatafuta mtu wa pembeni kupunguza machungu ambao unapelekea kumuasi Mola wao.

Lkn Kwa upande mwengine mahari kubwa si Tu kwamba inamfanya muoaji akamuliwe uchumi wake lkn ni kukomoana pia...Kwa mfano kuna Uzi mmoja kuna mtu anadaiwa mahari ya shilingi milioni (7)...unajiuliza je anauziwa mwanamke au anamuoa? Lkn kama haitoshi mahari kubwa zinachangia Sana wanawake wengi kunyanyasika ktk ndoa kwasababu ametolewa mahari nyingi na hivyo mume kujiona ana uwezo wa kufanya chochote kwakuwa amemnunua mwanamke husika.

Naamini kabisa kama wakristo nao masharti ya kuachana yangekuwa mepesi tungeshuhudia talaka nyingi Tu kwasababu changamoto zinazo zikumba ndoa za kimila na kiislamu ni hizo hizo.
 
Hayo mambo ya ndizi yamesemwa lkn ktk Hali halisi ni kuwa dhana kubwa ni mahari kuwa hafifu ili isiwe kikwazo Kwa vijana kushindwa kuoa......na wanawake wachache Sana huenda wakahitaji juzuu au msahafu lkn wengi wao ni kiasi cha hela ambacho sio cha kumuumiza muoaji....kwahiyo kama muoaji na muolewaji wameelewana na muoaji anaweza kutoa kiasi Kikubwa zaidi kutokana na uwezo na mapenzi yake hakuna ubaya....

Ndoa kuvunjika haihusiana na mahari kuwa ndogo Ila kuna mambo mengi ndani yake...ikiwemo kutokuwepo Kwa uvumilivu ndani ya ndoa,usaliti na kadhalika.

Sasa kuonekana Kwa ndoa nyingi Kwa waislamu kuvunjika ni kwasababu Sheria inaruhusu hivyo....ingawa Mwenyezi Mungu hapendezewi na mambo ya talaka lkn inapobidi basi ni Bora watu kuachana Kwa wema kuliko wakaishi ktk uadui na kukosa Amani....kwani lengo la ndoa ni kupatikana utulivu ndani yake.

Sasa wakristo sio kwamba hawapendi kuachana Ila ni Sheria ya kanisa inasema hivyo....lkn nyuma ya pazia kuna maumivu makubwa Sana Kwa wanandoa....wengi wao wapo ktk kifungo Kikubwa ingawa hawapo gerezani lkn kama nyumba imekuwa kama gereza....watu wanatengana vyumba Kwa nembo ya ndoa ya kudumu lkn kiuhalisia inawaangiza ktk dhambi kwasababu kila mwanandoa anatafuta mtu wa pembeni kupunguza machungu ambao unapelekea kumuasi Mola wao.

Lkn Kwa upande mwengine mahari kubwa si Tu kwamba inamfanya muoaji akamuliwe uchumi wake lkn ni kukomoana pia...Kwa mfano kuna Uzi mmoja kuna mtu anadaiwa mahari ya shilingi milioni (7)...unajiuliza je anauziwa mwanamke au anamuoa? Lkn kama haitoshi mahari kubwa zinachangia Sana wanawake wengi kunyanyasika ktk ndoa kwasababu ametolewa mahari nyingi na hivyo mume kujiona ana uwezo wa kufanya chochote kwakuwa amemnunua mwanamke husika.

Naamini kabisa kama wakristo nao masharti ya kuachana yangekuwa mepesi tungeshuhudia talaka nyingi Tu kwasababu changamoto zinazo zikumba ndoa za kimila na kiislamu ni hizo hizo.
 
Tutafte pesa tusipende vya dezo,yaani nioze binti yangu kwa vindizi??? What on earth!
Ndio maana talaka zimeshamiri ukanda ambao Una waislamu kwa wingi, yaani,
"Easy come, easy gone"
Na mauwaji ya mahusiano yanatokea kwa upande gani bora kuachana kwa amani kuliko kufa kuzikana mwisho mnauana.
 
Tutafte pesa tusipende vya dezo,yaani nioze binti yangu kwa vindizi??? What on earth!
Ndio maana talaka zimeshamiri ukanda ambao Una waislamu kwa wingi, yaani,
"Easy

Tutafte pesa tusipende vya dezo,yaani nioze binti yangu kwa vindizi??? What on earth!
Ndio maana talaka zimeshamiri ukanda ambao Una waislamu kwa wingi, yaani,
"Easy come, easy gone"
Kwani binti yako unamuuza? Sidhani kama kuvunjika kwa ndoa ni suala la kulipa mahari kubwa au kidogo. Wahindi wao mke ndie anatoa mahari, ulaya hamna mahari.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom