Katika siasa hamtutendei haki sisi wa aina hii. Mnadhani mpo peke yenu tu!

GuDume

JF-Expert Member
Jan 18, 2015
6,652
14,247
Akili,mfumo na mawazo ya watanzania wengi wanaamini kama wewe si ccm basi ni cdm au cuf n.K wanashindwa kuelewa kuna watu ambao hatuja uza utu,akili na fikra zetu. Kuna watanzania huru ambao wao wamegoma kudumisha fikra za mwenyekiti au za chama husika.

Hili kundi ipo na lina watu wengi pia.Na vyama karibia vyote vimeshindwa kulitumia kundi hili sababu utakuta kwenye kampeni,kwenye mikutano na mihadhara kundi hil linatengwa.Tofauti na nchi za wenzetu zilizoendelea. Hizi huwa na kundi kubwa la wananchi ambao si wanachama wa chama chochote na hawa wanategemea sera za mgombea uongozi.

Nchi za kiafrika hasa tanzania ni tofauti. Its either with us or against us.Ndo maana kwa mwono huu ukiipinga ccm watakuita wewe cdm. Ukiipinga cdm watakuita wewe CCM. Kwanini? Sababu hawaamini katika fikra huru au demokrasia ya kweli.Ukishakuwa wewe ccm basi unatakiwa upinge kila linalosemwa na cdm. And the vice versa is true. Unadhan hapa inchi itawezeje kuendelea?

Kama mtu atatoa wazo hatutaliangalia wazo. Tutaangalia aliyesema ni chama gani,wakati flani inaweza kuwa dini gani au kabila gani. Halafu ndo tunaamua tuunge au tupinge hiyo hoja kwa kuzingatia vigezo hafifu kama hivyo.

Ufuasi wa chama au mtu ni utumwa, ni kuuza nafsi, akili ,fikra na utambuzi wa mambo. Na hiki ni kigezo kikubwa cha kuwa na fikra duni,dhaifu au kondefu.Maana tunajikuta kuwa tumejizungushia wigo katika kufikiri.Hatufikiri nje ya wigo huo.

Binafsi niliacha kuwa mfuasi wa mtu au chama mwaka 2000.Miaka 19 baadaye watu bado wanakumbatia ufuasi, utumwa wa kifikra. Na hawa huwa wanakuwa waliosoma (lakini hawajaelimika) na wasiosoma hivyo wana ujinga bado. Tanzania itabadilika ikiwa kuna siku mtu ndani ya cdm atakosoa jambo na kuheshimiwa au mawazo yake kutendewa kazi na mwingine ndani ya ccm atakosoa na pia kaendelea kuheshimiwa na mawazo yake yakafanyiwa kazi.

Tunajiweka kazi hali ya u-mbwa pale tunapoteua kuwa na bwana wa kumtumikia na kumuunga mkono katika kila jambo. Huu si ubinadamu. Mbwa humsikiliza bwana ake yu asemaje au yu ataka nini naye huunga mkono jambo hilo au hulitenda pasipo kuhoji.Hii ni hali mbaya kwa taifa hasa kwa vijana ambao kwa sasa ndo wamekuwa wafuasi wa vyama na watu mpaka wanakinaisha.

Ombi langu:

Mkiwa kwenye vyama vyenu, ufuasi wenu na mabwana zenu, hali ninyi mkiwa watwana basi msisahau tupo na sisi ambao tumegoma kuwa wafuasi, tumegoma kuuza nafsi, tumegoma kulaza ubongo. Sisi ambao tumeamua kuita nyeupe nyeupe na nyeusi nyeusi pasipo kujali anayetuoesha anapendelea hizo rangi ziitwe nini.

Mimi sihitaji kuwa mwanachama au mfuasi wa kiongozi flani ili nitoe mawazo yangu. Nitabaki kuwa mtanzania asiye na chama wala mfuasi wa mtu yeyote ili niweze kutizama na kuona mambo katika mwanga bora.

"Ufuasi ni upofu wa kifikra, ukada ni upumbavu" tukatae kutumika.... Wanaowatumia wanawadhalilisha sana. Kiakili,kifikra,kiimani na kimwili.

"Tanzania kwanza, vyama baadaye"
 
bro wewe ni mmoja nifanya watu walionifanya nijiunga jamiiforums. unachosema ni kweli nami nakubaliana nawe kwa asilimia 100. watanzania hawataki kabisa demokrasia ndo maana haraka sana wakiona unampinga mtu flani hawaamini kuwa hiyo ndo demokrasia na ni haki yako kisheria badala yake wanaamua kukuunganisha na chama flani.hii si haki. mimi simkubali rais magufuli kwa kila jambo kuna mambo nayapinga sana tena nayachukia kwa chuki yote. lakini yakiwepo ya msingi nitayaunga mkono kwa nguvu zote. na ndo maana ninawaambia watu wapinzani wanaanza kupoteza uelekeo kwa sasa. tena wanapoteza sana uelekeo ni kama jahazi lililokata kamba.so linajiendea tu kutegemeana na upepo uendako.
 
daaah... hapa nimejifunza kitu GuDume huwa ukitulia unakuwa na madini sana. hii aione Pascal Mayalla . we jamaa nilikuja kugundua una akili sema basi tu sometime unapenda kujichengua. haya mawazo yako kama vijana wengi tungekuwa nayo inchi ingeendelea. lakini hatupo hivyo. nakwambia kwa huu uzi subiri haya mawili.
1. watakuja kukutukana sana
2. watakustahi na kuamua kutosema lolote. maana ulivyokaa ni kuwa hauja base washabiki wowote humu JF hivyo utakosa wa kukuunga mkono.kwa sababu hujawasema vibaya chadema na hujawasema vibaya ccm hivyo hauna faida. ila mimi binafsi nimekuelewa sana.
 
Kuwa "neutral" ni unafki.

Kuwa mfuasi wa chama sio lazima uwe na kadi.
 
unalosema ni kweli. binafsi sioni mabadiliko makubwa kwangu sababu sikunufaika na utawala uliopita na huu pia hauninufaishi pia.

Na ndio kundi pekee ambalo haliumizwi na huu utawala,sababu halijawahi kunufaishwa na utawala wowote.

Asante mkuu.
 
naheshimu pia mawazo yako. ndo uzuri wa demokrasia. kila mtu anapaswa aheshimiwe kwa kile anachoamini.
Kuwa "neutral" ni unafki.

Kuwa mfuasi wa chama sio lazima uwe na kadi.
 
Subiri waje nyumbu wa ufipa na lumumba buku saba.

Hawataona hoja zako, wataishia kutoana mapovu tu!

# VIVA FIKRA HURU
 
Kama sio simba basi yanga wanatuonea sana sisi mashabiki wa Ruvu shooting.
 
bro wewe ni mmoja nifanya watu walionifanya nijiunga jamiiforums. unachosema ni kweli nami nakubaliana nawe kwa asilimia 100. watanzania hawataki kabisa demokrasia ndo maana haraka sana wakiona unampinga mtu flani hawaamini kuwa hiyo ndo demokrasia na ni haki yako kisheria badala yake wanaamua kukuunganisha na chama flani.hii si haki. mimi simkubali rais magufuli kwa kila jambo kuna mambo nayapinga sana tena nayachukia kwa chuki yote. lakini yakiwepo ya msingi nitayaunga mkono kwa nguvu zote. na ndo maana ninawaambia watu wapinzani wanaanza kupoteza uelekeo kwa sasa. tena wanapoteza sana uelekeo ni kama jahazi lililokata kamba.so linajiendea tu kutegemeana na upepo uendako.
Kama wanazuiwa kuhutubia wananchi unasemaje wamepoteza uelekeo?
Au akili zako ndio zimepoteza umakini.
 
Na ndio kundi pekee ambalo haliumizwi na huu utawala,sababu halijawahi kunufaishwa na utawala wowote.

Asante mkuu.
Hakuna mtanzania hata mmoja hajaumizwa na utawala wa Magu. Unataka kuniambia hao wote waliobomolewa nyumba zao, malaki kwa malaki, wote ni wa vyama vya siasa? Unataka kuniambia kwamba waathirika wa kudhoofu kwa mzunguko wa pesa ni makada peke yao? unataka kuniambia kwamba wafanyabiashara wote waliofunga/kufungiwa biashara zao ni makada wa vyama? Lakini pia, Kikwete aliboresha sana hospitali ya Muhimbili, pamoja kuboresha sana kitengo cha EMERGENCY. Unataka kutuambia kwamba walionufaika ni wanachama na mashabiki wa vyama vya siasa? au miradi iliyoanzishwa na JK ambayo Magufuli anaitekeleza, mfano maji, flyover, nk, wanufaika ni makada wa vyama vya siasa?

Akili,mfumo na mawazo ya watanzania wengi wanaamini kama wewe si ccm basi ni cdm au cuf n.K wanashindwa kuelewa kuna watu ambao hatuja uza utu,akili na fikra zetu. Kuna watanzania huru ambao wao wamegoma kudumisha fikra za mwenyekiti au za chama husika.

Hili kundi ipo na lina watu wengi pia.Na vyama karibia vyote vimeshindwa kulitumia kundi hili sababu utakuta kwenye kampeni,kwenye mikutano na mihadhara kundi hil linatengwa.Tofauti na nchi za wenzetu zilizoendelea. Hizi huwa na kundi kubwa la wananchi ambao si wanachama wa chama chochote na hawa wanategemea sera za mgombea uongozi.

Nchi za kiafrika hasa tanzania ni tofauti. Its either with us or against us.Ndo maana kwa mwono huu ukiipinga ccm watakuita wewe cdm. Ukiipinga cdm watakuita wewe CCM. Kwanini? Sababu hawaamini katika fikra huru au demokrasia ya kweli.Ukishakuwa wewe ccm basi unatakiwa upinge kila linalosemwa na cdm. And the vice versa is true. Unadhan hapa inchi itawezeje kuendelea?

Kama mtu atatoa wazo hatutaliangalia wazo. Tutaangalia aliyesema ni chama gani,wakati flani inaweza kuwa dini gani au kabila gani. Halafu ndo tunaamua tuunge au tupinge hiyo hoja kwa kuzingatia vigezo hafifu kama hivyo.

Ufuasi wa chama au mtu ni utumwa, ni kuuza nafsi, akili ,fikra na utambuzi wa mambo. Na hiki ni kigezo kikubwa cha kuwa na fikra duni,dhaifu au kondefu.Maana tunajikuta kuwa tumejizungushia wigo katika kufikiri.Hatufikiri nje ya wigo huo.

Binafsi niliacha kuwa mfuasi wa mtu au chama mwaka 2000.Miaka 19 baadaye watu bado wanakumbatia ufuasi, utumwa wa kifikra. Na hawa huwa wanakuwa waliosoma (lakini hawajaelimika) na wasiosoma hivyo wana ujinga bado. Tanzania itabadilika ikiwa kuna siku mtu ndani ya cdm atakosoa jambo na kuheshimiwa au mawazo yake kutendewa kazi na mwingine ndani ya ccm atakosoa na pia kaendelea kuheshimiwa na mawazo yake yakafanyiwa kazi.

Tunajiweka kazi hali ya u-mbwa pale tunapoteua kuwa na bwana wa kumtumikia na kumuunga mkono katika kila jambo. Huu si ubinadamu. Mbwa humsikiliza bwana ake yu asemaje au yu ataka nini naye huunga mkono jambo hilo au hulitenda pasipo kuhoji.Hii ni hali mbaya kwa taifa hasa kwa vijana ambao kwa sasa ndo wamekuwa wafuasi wa vyama na watu mpaka wanakinaisha.

Ombi langu:

Mkiwa kwenye vyama vyenu, ufuasi wenu na mabwana zenu, hali ninyi mkiwa watwana basi msisahau tupo na sisi ambao tumegoma kuwa wafuasi, tumegoma kuuza nafsi, tumegoma kulaza ubongo. Sisi ambao tumeamua kuita nyeupe nyeupe na nyeusi nyeusi pasipo kujali anayetuoesha anapendelea hizo rangi ziitwe nini.

Mimi sihitaji kuwa mwanachama au mfuasi wa kiongozi flani ili nitoe mawazo yangu. Nitabaki kuwa mtanzania asiye na chama wala mfuasi wa mtu yeyote ili niweze kutizama na kuona mambo katika mwanga bora.

"Ufuasi ni upofu wa kifikra, ukada ni upumbavu" tukatae kutumika.... Wanaowatumia wanawadhalilisha sana. Kiakili,kifikra,kiimani na kimwili.

"Tanzania kwanza, vyama baadaye"
Kwa taarifa yako, binadamu wote ni watumwa wa serikali. serikali ni kikundi cha watu kilichojipatia mamlaka ya kukusanya fedha kutoka kwa watawaliwa, "raia", na kufanya yale wanayoona wao kwamba yanafaa. wapi utakwenda hapa duniani uwe free tu kama hewa? popote utakapokwenda wewe ni mtumwa wa serikali ya mahali hapo. Ni kweli serikali zinatofautiana, lakini kimsingi serikali zote ni za kimabavu, kwa viwango tofauti. Hii habari ya vyama ni kama danganya toto hivi. lakini unaweza ku-influence kwa kiasi fulani, katika mfumo ambao vyama vinachuana kwa viwango vya usawa. Lakini kwa nchi yetu, Hapa ni chama kimoja tu, asikudanganye mtu. kwa hiyo ukiwa "chama cha upinzani", angalau unapata nafasi ya kukipiga madongo hicho "chama kimoja tawala", ili kipunguze sera za kukukandamiza.

"Presha" inasaidia, hata katika mifumo ya kidikteta. lakini cha ajabu na kushangaza kuhusu hii dunia yetu, hata ukikaa kimya na kujifanya "haupo chama chochote", kama unavyosema, bado utafaidika na matunda ya juhudi za "vyama vya upinzani". Ni presha ya CHADEMA kwa miongo miwili iliyopita ambayo inafanya CCM wajitahidi angalau kufanya wanayofanya sasa hivi. ni presha kupinga kanuni za mafao ya wastaafu ndio zitapelekea mabadiliko katika kanuni hizo.
 
DAH! Nipe 5 mwanangu.
Akili,mfumo na mawazo ya watanzania wengi wanaamini kama wewe si ccm basi ni cdm au cuf n.K wanashindwa kuelewa kuna watu ambao hatuja uza utu,akili na fikra zetu. Kuna watanzania huru ambao wao wamegoma kudumisha fikra za mwenyekiti au za chama husika.

Hili kundi ipo na lina watu wengi pia.Na vyama karibia vyote vimeshindwa kulitumia kundi hili sababu utakuta kwenye kampeni,kwenye mikutano na mihadhara kundi hil linatengwa.Tofauti na nchi za wenzetu zilizoendelea. Hizi huwa na kundi kubwa la wananchi ambao si wanachama wa chama chochote na hawa wanategemea sera za mgombea uongozi.

Nchi za kiafrika hasa tanzania ni tofauti. Its either with us or against us.Ndo maana kwa mwono huu ukiipinga ccm watakuita wewe cdm. Ukiipinga cdm watakuita wewe CCM. Kwanini? Sababu hawaamini katika fikra huru au demokrasia ya kweli.Ukishakuwa wewe ccm basi unatakiwa upinge kila linalosemwa na cdm. And the vice versa is true. Unadhan hapa inchi itawezeje kuendelea?

Kama mtu atatoa wazo hatutaliangalia wazo. Tutaangalia aliyesema ni chama gani,wakati flani inaweza kuwa dini gani au kabila gani. Halafu ndo tunaamua tuunge au tupinge hiyo hoja kwa kuzingatia vigezo hafifu kama hivyo.

Ufuasi wa chama au mtu ni utumwa, ni kuuza nafsi, akili ,fikra na utambuzi wa mambo. Na hiki ni kigezo kikubwa cha kuwa na fikra duni,dhaifu au kondefu.Maana tunajikuta kuwa tumejizungushia wigo katika kufikiri.Hatufikiri nje ya wigo huo.

Binafsi niliacha kuwa mfuasi wa mtu au chama mwaka 2000.Miaka 19 baadaye watu bado wanakumbatia ufuasi, utumwa wa kifikra. Na hawa huwa wanakuwa waliosoma (lakini hawajaelimika) na wasiosoma hivyo wana ujinga bado. Tanzania itabadilika ikiwa kuna siku mtu ndani ya cdm atakosoa jambo na kuheshimiwa au mawazo yake kutendewa kazi na mwingine ndani ya ccm atakosoa na pia kaendelea kuheshimiwa na mawazo yake yakafanyiwa kazi.

Tunajiweka kazi hali ya u-mbwa pale tunapoteua kuwa na bwana wa kumtumikia na kumuunga mkono katika kila jambo. Huu si ubinadamu. Mbwa humsikiliza bwana ake yu asemaje au yu ataka nini naye huunga mkono jambo hilo au hulitenda pasipo kuhoji.Hii ni hali mbaya kwa taifa hasa kwa vijana ambao kwa sasa ndo wamekuwa wafuasi wa vyama na watu mpaka wanakinaisha.

Ombi langu:

Mkiwa kwenye vyama vyenu, ufuasi wenu na mabwana zenu, hali ninyi mkiwa watwana basi msisahau tupo na sisi ambao tumegoma kuwa wafuasi, tumegoma kuuza nafsi, tumegoma kulaza ubongo. Sisi ambao tumeamua kuita nyeupe nyeupe na nyeusi nyeusi pasipo kujali anayetuoesha anapendelea hizo rangi ziitwe nini.

Mimi sihitaji kuwa mwanachama au mfuasi wa kiongozi flani ili nitoe mawazo yangu. Nitabaki kuwa mtanzania asiye na chama wala mfuasi wa mtu yeyote ili niweze kutizama na kuona mambo katika mwanga bora.

"Ufuasi ni upofu wa kifikra, ukada ni upumbavu" tukatae kutumika.... Wanaowatumia wanawadhalilisha sana. Kiakili,kifikra,kiimani na kimwili.

"Tanzania kwanza, vyama baadaye"
 
Kuwa kada mwanachama ni utumwa uliotukuka binafsi stowahi kufungwa kengere shingoni Kwa utumwa wa vyama vya siasa
 
Heko, leo nimejijua niko wap. 'fikra huru' thanks sina kadi wala chama,NITAPONDA ATAKAYEBORONGA NA NTASIFIA ATAKAYEFANYA VIZURI.... (FIKRA HURU)
 
Back
Top Bottom