Kwa maelezo uliyotoa ya uvumilivu woote huo sasa sijui unataka mke wa aina gani, shauri yako makurumbembe yapo tena yatakudaka kwa mikono miwili...angalia sana pia sali huwezi jua ya dunia
Jamani tuambizane ukweli; kuna mtu anaoa mwanamke au anaolewa na mtu ambaye penzi ni la mashaka na maisha yanasonga bila tatizo???. Naogopa saana kukwambia kaka uendelee na mpango wa ndoa. Jamani mapenzi mapenzi pekee ndio yawe sababu ya kuoa/ kuolewa na si kingine; vinginevyo tutaendelea kulia na cheating.
Huyo mke atageuka mashine ya kukuzalia na kukulelea watoto wewe utakuwa unapiga nje kwa unao wapenda. Please stop!!!! Ndoa si suala dogo; ni uamuzi unatakiwa ufanye without any doubt kama unataka ku enjoy maisha ya ndoa.
Hapo hamjaoana tayari una mapenzi ya kuvuta kwa manati; mkikaa miaka mitano si utaama chumba.
Hii ndiyo inafanya watu wabeze ndoa za siku hizi kuwa zimekaa kibiashara zaidi.
ndo maana mimi nimemwambia ajipe mda kabla hajaamua
inaweza kuwa ni just a phase au kumbe ni serious
Nahisi jamaa keshaonja moja linampeleka resi maisha bwanain blue, wa2 wa hivyo mara nyingi uangukia humo...
mwisho wa siku huwa wanajilaumu maishani mwao kwa kuongozwa na tamaa...
Hata kama ni phase mi bado naona ni bad sign. What if akimuoa phase ikajirudia na ikakataa ku phase out.
Na wewe hali imekupata ushatangazia watu kibao, sasa ikiwa ni hali ya kupita sijui utajieleza vipi kwa watu tena,Wnajamvi nashukuru kwa michango yenu wote.Mungu awabariki sana.Rafiki yangu kanipigia cim kesho anataka kunipeleka nikafanyiwe cancelling..hii si balaa...hahahaha
kwani ukimuoa hata kama humpendi una hasara gani???mie naonaga kwa mwanaume haisumbui,sie wanawake ndio baada ya muda na tukishaolewa na kuachika ndio taabu kusettle tena na mtu, ila mwanaume yeye saa zote katika umri wowote akiamua kuoa anaweza kuoa,so wewe muoe hivyo hiyo hata kama humpendi with time mapenzi yatakuja na yasipokuja huna hasara unamwacha tu ukijisikia.
Wnajamvi nashukuru kwa michango yenu wote.Mungu awabariki sana.Rafiki yangu kanipigia cim kesho anataka kunipeleka nikafanyiwe cancelling..hii si balaa...hahahaha
Nimekuwa na urafiki na dada mmoja kama miaka saba hivi imepita baada ya hapo nikamwambia mie napenda huwe mpenzi wangu mungu akipenda tuwe pamoja..yule dada akakubali tuakaanza safari ya mahusiano ki kimapenzi..tumendelea kwa kipindi kirefu tukavumiliana katika kila hari na kuombeana misamaha kibao kila mmoja wetu anapokosea kwa mwenzake,tumendelea nikafikia hatua ya kutoa mahari na familia zetu zikakutana na kufahamiana na kuwa kama ndugu baada ya hapo tukatangaza rasmi ndoa,wazazi wakafurahi wakasherekea kwa sana,
Shida sasa inakuja hivi huyu dada nimetokea kumchoka ghafla na upendo umepotea ghafla..ajaniudhi wala sijamuudhi..na wala hakuna shida yoyote,yaani nikimuona namchukia si mchezo hadi najuta kwa nini nimemposa,nilikwisha kumwambia jinsi ninavyojisikia juu yake akasema siku nikimwacha tu anajiua..Je katika mazingira kama haya naweza kuvunja kila kitu?je upande wa wazazi wetu pande zote mbili itakuwaje?best wangu anasema nijipe moyo mambo yatakuwa powa baadaye lakini naona kama napoteza mda na huyu dada..na nikitaka kumwacha nimwache katika mazingira gani ambayo roho yake itabaki salama?
nilikuwa nasoma kwanza mawazo ya watu wote nione watakavyomshauri,umetoa ushauri mzuri sna coz hata mm nilitaka kutoa ushauri ambao hauna kabsa tofauti na huu,bg up mkubwa.Sogeza mbele tarehe ya harusi; kama waweza chukua likizo uwe mbali naye kwa muda. Tengeneza Mazingira ya kummiss mapenzi yatarudi.
Mimi nafikiri ni uoga tu, na hiyo huwatokea wengi tu! Pia shetani yupo, kama ni muumuni sali sana!